CHAMA Chama Cha Mapinduzi(CCM)Zanzibar kimesema kinahitaji viongozi wachapakazi,wazalendo na waadilifu katika kuwatumikia Wananchi ambao ndio wenye nguvu ya mamlaka ya kukiweka madarakani kupitia michakato ya Uchaguzi wa kidemokrasia
Kauli hiyo imetolewa na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dkt.Mohamed Said Dimwa wakati akikabidhi nyumba iliyojengwa na Mbunge wa Jimbo la Magomeni Mhe.Mwanakhamis Kassim Said kwa Mwananchi wa shehia ya Nyerere ndugu Mussa Juma Hemed huko Magomeni Zanzibar.
Dkt.Dimwa,alisema viongozi wanaotekekeza kwa vitendo ahadi walizoahidi kupitia Uchaguzi mkuu uliopita wanaenda sambamba na malengo ya Chama Cha Mapinduzi katika kuwatumikia Wananchi na kwamba wanatakiwa kuongeza Kasi ya utekelezaji wa ilani ya Uchaguzi Ili CCM ishinde kwa ngazi mbali mbali katika Uchaguzi mkuu ujao.
Alieleza kuwa Wananchi wanahitaki kuona maendeleo katika majimbo yao ikiwemo huduma Bora za maji safi na salama,hospitali,skuli,barabara zenye ubora,umeme na makaazi bora ya kuishi.
Katika maelezo yake Dkt.Dimwa,alisema kuwa CCM inaendelea kutathmini na kufuatilia utendaji wa kila kiongozi wakiwemo madiwani,Wabunge na wawakilishi kwa lengo la kujiridhisha kama wanakidhi vigezo vya kuendeleza kuongoza kuwatumikia wananchi.
Kupitia hafla hiyo alimpongeza Mbunge huyo wa Jimbo la Magomeni kwa juhudi zake za kuhakikisha Mwananchi huyo anapata nyumba nzuri ya kuishi na kwamba sio kuwa ametekeleza ilani ya CCM pia ametoa sadaka kubwa itanayoongeza baraka kwa Mwenyezi Mungu.
Alisema kuwa Chama Cha Mapinduzi hakitowavumilia baadhi ya viongozi wasiotekeleza ilani ya Uchaguzi ya CCM badala yake kitatoa nafasi za kuendeleza kuongoza kutokana na uchapakazi wa kiongozi na sio umaarufu wake.
"Tunapowatumikia Wananchi kwa uadilifu kwa kutatua changamoto zao inasadia kutengeneza mazingira bora ya ushindi wa CCM wa ngazi mbali mbali katika Uchaguzi Mkuu ujao.
Nitumie nafasi hii tu kuwaeleza kuwa CCM kwa awamu hii ya Mwenyekiti wetu Rais Dkt.Samia npamoja na Rais Dk.Mwinyi,haitomuonea mtu bali tutaenda na kutoa kipaumbele kwa wale tuliolima nao mazao juani ndio tutakaovuna na kula nao kivulini.",alisisitiza Dkt.Dimwa.
Alisemea tabia za baadhi ya makada na wanachama kupita majimbo kuanza kampeni za kuharibu sifa za viongozi waliopo madarakani kwa sasa na kueleza kuwa viongozi hao waachwe na kupewa nafasi za kuwatumikia Wananchi na kwamba wanaotaka kuwania Uongozi wasubiri muda wa Uchaguzi ufike mwaka 2025.
Naye Mbunge wa Jimbo la Magomeni Zanzibar Mhe.Mwanakhamis Kassim Said, alipongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan pamoja na Rais wa Zanzibar Dk.Hussein Mwinyi kwa utendaji wao mzuri wa kuwaletea wananchi maendeleo.
Alisema maendeleo yaliyopatikana katika Jimbo Hilo yametokana na ushirikiano mzuri ulipo baina ya wanachama,viongozi wa ngazi za mashina hadi Mkoa ikiwemo Kamati ya Jimbo na Wananchi wote kwa ujumla.
Akizungumzia ujenzi wa nyumba ya Mwananchi huyo ndugu Mussa Juma,alisema imegharimu kiasi cha shilingi milioni 17,357,000.
Mhe.Mwanakhamis,amesema lengo la kujenga nyumba hiyo ni kuhakikisha Mwananchi huyo anaishi katika maakazi Bora kama ilivyo kwa Wananchi wengine wa Jimbo hilo.
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
28-02-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
28-02-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
28-02-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
28-02-2026
πππ¦πππ‘ππ’ πππ πππ§. π ππππ₯π’ ππππ£π’πππππͺπ ππͺπ π¦πππ‘ππͺπ πππ₯ ππ¦ π¦πππππ
28-02-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
28-02-2026
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
28-02-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
28-02-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
28-02-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
28-02-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
28-02-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
28-02-2026
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
28-02-2026
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
28-02-2026
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
28-02-2026
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
28-02-2026
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
28-02-2026
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
28-02-2026
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
28-02-2026
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
28-02-2026