Makao Makuu - Dodoma
#CCM Imetimia KaziIendelee

Habari na Matukio Mbalimbali


𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐒𝐇𝐈𝐍𝐀 𝐍𝐀. 𝟏𝟎 𝐌𝐀𝐅𝐈𝐅𝐈, 𝐀𝐒𝐈𝐒𝐈𝐓𝐈𝐙𝐀 𝐀𝐌𝐀𝐍𝐈, 𝐔𝐌𝐎𝐉𝐀 𝐍𝐀 𝐌𝐒𝐇𝐈𝐊𝐀𝐌𝐀𝐍𝐎

alternative

Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM Taifa, Ndugu Kenani Laban Kihongosi, ametembelea Shina Na. 10, Mtaa wa Mwenge, Kata ya Mafifi, Iringa Mjini, na kupata fursa ya kuzungumza na wanachama pamoja na wananchi wa eneo hilo. Akiwa mzawa wa Iringa, Ndugu Kihongosi amewashukuru wananchi kwa malezi, upendo na mshikamano waliomjengea tangu utotoni, huku akiwapongeza viongozi wa CCM kwa kazi kubwa wanayoendelea kuifanya katika kuimarisha Chama na kusimamia maendeleo ya wananchi. Katika ujumbe wake, amesisitiza kuwa Watanzania hawana nchi nyingine zaidi ya Tanzania, hivyo ni wajibu wa kila mmoja kulinda amani, umoja na utulivu wa Taifa. Amewataka wananchi kuwakataa na kuwakemea wote wanaohubiri machafuko, migawanyiko na vurugu zinazoweza kuhatarisha maendeleo ya nchi. Aidha, amewafikishia wananchi salamu za Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, na kuwashukuru kwa kuendelea kuiamini CCM. Amesema CCM itaendelea kulea, kuandaa na kuwawezesha vijana kuwa viongozi bora na watumishi wa Taifa lao. Akihitimisha, Ndugu Kihongosi amewahimiza wananchi kuendelea kudumisha umoja, upendo na mshikamano, akieleza kuwa hizo ndizo nguzo kuu za CCM na msingi wa nguvu ya Taifa la Tanzania. "Tanzania ni yetu sote; tuilinde, tuiimarishe na tuiache salama kwa vizazi vijavyo." Tembelea: www.ccm.or.tz --- #KaziNaUtuTunasongaMbele #CCMIpoKazini #KenaniLabanKihongosi #MtumishiWaWote #Iringa #Mafifi

alternative alternative alternative alternative alternative alternative alternative alternative alternative
Habari Nyingine