CCM YACHANGIA TSH MILIONI 10 KWA WANANCHI WALIOPATWA NA MAAFA YA MAPOROMOKO YA MLIMA - ITEZI MKOANI MBEYA
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi , amewatembelea wananchi waliopatwa na maafa ya kuharibikiwa kwa nyumba na mali zao mara baada ya mvua kubwa zinazoendelea kunyesha Nchini na kusababisha maporomoko ya matope kutoka kwenye mlima hali iliyopelekea uharibifu wa nyumba katika makazi ya wananchi wa mtaa wa Gomba kaskazini katika Kata ya Itezi.
Mara baada ya kufika katika kambi waiishio kwa muda katika shule ya msingi ya Tambukareli , Balozi Dkt. Nchimbi ametanguliza salamu za pole za Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan , na kuwapatia kiasi cha Tsh Milioni 10 wahanga hao ilikusudi kuendelea kuwawezesha katika nyakati hizi ngumu za mpito pesa ambazo zilikabidhiwa kwa mwanamama mmoja kati ya waliopatwa na maafa hayo pamoja na Diwani wa kata hiyo ya Itezi Ndugu. Sambweshi Tambala ambaye pia amepatwa na maafa hayo.
Akizungumza na Wananchi hao, Balozi Dkt. Nchimbi amesema lengo la kufika hapo ni kuwapa pole na kuwaomba kuendelea kumtanguliza na kumshukuru Mwenyezi Mungu bila kuacha kuomba usiku na mchana.
" Tumshukuru Mungu wote mpo salama, tujaribu kufikiria maporomoko haya yangetokea saa 8 usiku leo tungekuwa tunazungumza nini ? Tumtangulize Mungu sana "
" CCM inatoa shukrani kwa watu wote walioguswa na kuja kusaidia jambi hili, Shukrani pia kwa Serikali, Taasii mbalimbali na Mbunge wenu Dkt. Tulia Ackson "
" Niwaombe sana ndugu zangu, zingatieni tahadhari za serikali wakati uchunguzi unaendelea, wananchi tuwe na subira tusiharakie kurudi huko "
Naye Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Ndugu. Beno Malisa, amemueleza Katibu Mkuu kuwa maporomoko ya matope kutoka mlimani yalitokea siku ya jumapili tarehe 14 Aprili, 2024 na kusababisha uharibifu wa nyumba 21 na mali pekee bila kupelekea majeruhi wala vifo. Mafuriko hayo yamesababisha kaya zaidi ya 96 kukosa makazi hali iliyopelekea serikali kufanya juhudi za kuwapa makazi ya muda kwa kuweka kambi katika shule ya msingi ya Tambukareli.
DC Malisa ameendelea kusema kuwa wananchi hao wamepewa misaada ya huduma za kibanadamu kutoka serikali ya mkoa Mbeya na wadau mbalimbali.
Vilevile , DC Malisa amesema wananchi hao wamekuwa wakipatiwa huduma za afya na msaada wa kisaikolojia, Aidha shughuli zinazoendelea kwasasa ni kuweka sawa miundombinu ya umeme, maji na barabara.
Pia, DC Malisa amesema ofisi ya mratibu wa Taifa wanaendelea na uchunguzi wa kina katika jambo hilo ili kupata muelekeo wa eneo hilo lililoathirika.
ποΈ17 Aprili, 2024
πJijini Mbeya
ZIARA YA RAIS WA MISRI-TANZANIA
19-07-2026
π° CCM NA ACT-WAZALENDO WASAINI MARIDHIANO YA PAMOJA YA KISIASA ZANZIBAR
19-07-2026
π ππππ ππ ππππ ππ ππππππππ, πππ. ππππ-ππππ ππππππ! π°
19-07-2026
π°πππππ ππππππ ππππ ππ πππ ππππ ππππππππ πππππ πππ πππππππππππ πππ ππ πππ ππππ ππ ππππππ
19-07-2026
π°ππππ ππ πππππππππππ ππ ππππ ππππ ππππ!
19-07-2026
ππππ ππ ππππ ππ πππππ; πππππ ππ ππππππππ, πππππππ πππππππ!!!!!
19-07-2026
ππππππ πππππ πππππ ππππππ ππππππππ ππ ππππππππππ
19-07-2026
πππππππ ππππππ πππππππ πππππ ππ πππππππππππ ππππππππ, ππππππ-ππππππ
19-07-2026
πππππππ ππππππ πππππππππ πππππ ππ. ππ πππ
ππ
π, πππππππππ πππππ, πππππ ππ ππππππππππ
19-07-2026
πππππ ππ πππ
ππππ ππ ππ
ππππ ππππππ πππ
πππππ π
ππππ ππ πππππ πππ ππππππ
19-07-2026
ππππππ, ππππ ππππ ππ πππ!
19-07-2026
πππππ: πππ. πππππ ππππππ ππππππ ππ πππππππππππ ππππππ ππ πππππ ππ πππ
19-07-2026
ππππ ππππππ, πππππ ππ πππππππ ππππππ!
19-07-2026
πππππ πππππππ πππ
πππππ; βπππππ
ππππππππππππππβ πππππππ πππππππ ππ πππππππ!
19-07-2026
ππππππ πππ πππππππππππ ππ ππ
πππππ ππ πππππππππ ππ ππππππ ππ ππππππππ: πππππππππ
19-07-2026
πππ ππππππ πππππ ππππππππ ππ ππππππ πππ ππππ ππ ππππππππππ ππππ
19-07-2026
πππππ ππ ππππππ ππ πππππππππ: πππππππππ
19-07-2026
πππππππππ πππππ ππππππ!!
19-07-2026
πππππ πππππππππ ππππππ, πππππππ ππππππππ ππ πππ ππππππ πππππ ππ ππππ ππ πππ πππ πππππππ
19-07-2026
πππππ: πππ ππππππππππππ ππππππ, ππππππππ ππππππππππ πππππππ ππππππππππ ππ ππππππππ
19-07-2026