Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla amesema uwepo wa Maonesho ya Wiki ya elimu ya juu nchini yamekuwa yakiziweka pamoja Taasisi, vyuo na wadau wa elimu ya juu kwa lengo la kutangaza fursa mbali mbali kwa wanafunzi wanaosoma na wanaotarajia kujiunga na vyuo vikuu vya ndani na nje ya Nchi
Ameyasema hayo wakati wa ufunguzi wa maonesho ya Tano(5) ya wiki ya elimu ya juu Zanzibar yaliyofanyika katika viwanja vya Maisara Mkoa wa Mjini Magharibi.
Mhe. Hemed amesema kupitia maonesho ya wiki ya elimu ya juu wanafunzi hupatiwa fursa mbali mbali za kimasomo ikiwemo upatikanaji wa mikopo, namna ya kujiunga na vyuo vya ndani na nje ya nchi na kutoa hamasa kwa wanafunzi kusoma kwa bidii na kujiendeleza katika ngazi ya elimu ya juu.
Amesema kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2020-2025, Sera na Dira ya Maendeleo ya mwaka 2050, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar imekuwa ikichukua hatua mbali mbali za uboreshaji wa elimu ikiwemo kuweka mageuzi makubwa kuanzia ngazi ya maandalizi hadi elimu ya juu kwa kuwawezesha wanafunzi kupata ujuzi na maarifa baada ya kumaliza masomo yao.
Aidha Serikali imeongeza Bajeti ya Bodi ya Mikopo ya elimu ya juu Zanzibar kutoka fedha za Kitanzania shilingi Bilioni 26.95 kwa mwaka wa fedha 2024 hadi kufikia Bilioni 30.5 kwa mwaka 2025 ambazo zitakwenda kuwanufaisha wanafunzi zaidi ya 7,367 ambapo kwa mara ya kwanza wanafuzi 1,000 wa ngazi ya Diploma watanufaika pia na mikopo hio.
Amefahamisha kuwa Serikali imeendelea kuimarisha huduma kwa wanafunzi wa vyuo vikuu ikiwemo kuwapatia Bima ya Afya pamoja na kuongeza fedha za kujikimu kwa wanafunzi wote wanaosoma Vyuo vya Zanzibar na vyuo vya Tanzania Bara.
Sambamba na hayo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar ametoa wito kwa wanafunzi na wananchi kwa ujumla kujitokeza na kuitumia vyema wiki ya maonesho kwa kujielimisha juu ya upatikanaji wa fursa mbali mbali za elimu ndani na nje ya nchi na kuwasisitiza wanafunzi kusoma kwa bidiii na kuzitumia vyema fursa wanazozipata pamoja na kuepuka kutumika kwa misingi yoyote ambayo itapelekea kuvuruga umoja na amani iliyopo nchini
Nae Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe. Lela Mohamed Mussa amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inayoongozwa na Rais Dkt Hussen Mwinyi inafanya kazi kubwa na nzuri katika kuimarisha miundombinu ya elimu inayopelekea kuongezeka kwa kiwango cha ufaulu jambo ambalo linaendelea kuiletea heshima zanzibar.
Mhe. Lela amesema ufaulu wa wanafunzi wa kidato cha sita unaongezeka mwaka hadi mwaka na kufikia asilimia 99.5% kwa mwaka 2024, ambapo zaidi ya wanafuzi 3,387 wamepata ufaulu wa daraja la kwanza hadi la tatu na wote wanatarajiwa kujiunga na vyuo vikuu mbali mbali ndani na nje ya nchi, hivyo kupitia maonesho ya juma la elimu ya juu yatawasaidia katika kufanya udahili wa vyuo na kupata taaluma juu ya kupata mikopo ya elimu juu iatakayowawezesha kusoma pasipo na changamoto ya aina yoyote.
Akisoma taarifa ya kitaaluma kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Naibu katibu Mkuu Utawala (WEMA) Khalid Massoud Waziri amesema lengo kuu la maonesho hayo ni kuimarisha mashirikiano baina ya Taasisi za Elimu, Vyuo na Mabenki ili kuhakikisha Sekta ya Elimu nchini inaendelea kuimarika na kiwango cha ufaulu kuzidi kuongezeka siku hadi siku.
Khalid amesema maonesho hayo ya juma la Elimu ya juu yanazidi kuimarika mwaka hadi mwaka ambapo kwa mwaka huu washiriki wameongezeka kutoka washiriki 17 mwaka 2020 hadi washiriki 77 mwaka 2024 na kutoa fursa kwa wanafunzi kupata kujua ni namna gani wanaweza kujiunga na vyou vikuu vya ndani na nje ya nchi samabamba na kupata kujua ni namna gani mwanafuzni anapata fursa ya kufanya maombi ya mikopo kwa taasisi husika.
Mapema Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar ametembelea Mbanda ya washiriki wa maonesho ya juma la Elimu ya juu na kupata elimu na huduma zinazotolewa katika mabanda hayo
ZIARA YA RAIS WA MISRI-TANZANIA
19-07-2026
🔰 CCM NA ACT-WAZALENDO WASAINI MARIDHIANO YA PAMOJA YA KISIASA ZANZIBAR
19-07-2026
🎉 𝐇𝐄𝐑𝐈 𝐘𝐀 𝐒𝐈𝐊𝐔 𝐘𝐀 𝐊𝐔𝐙𝐀𝐋𝐈𝐖𝐀, 𝐃𝐊𝐓. 𝐀𝐒𝐇𝐀-𝐑𝐎𝐒𝐄 𝐌𝐈𝐆𝐈𝐑𝐎! 🔰
19-07-2026
🔰𝐍𝐀𝐈𝐁𝐔 𝐊𝐀𝐓𝐈𝐁𝐔 𝐌𝐊𝐔𝐔 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐁𝐀𝐑𝐀 𝐀𝐒𝐇𝐈𝐑𝐈𝐊𝐈 𝐊𝐈𝐊𝐀𝐎 𝐂𝐇𝐀 𝐇𝐀𝐋𝐌𝐀𝐒𝐇𝐀𝐔𝐑𝐈 𝐊𝐔𝐔 𝐘𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐌𝐖𝐀𝐍𝐙𝐀
19-07-2026
🔰𝐇𝐄𝐑𝐈 𝐘𝐀 𝐌𝐀𝐀𝐃𝐇𝐈𝐌𝐈𝐒𝐇𝐎 𝐘𝐀 𝐒𝐀𝐁𝐀 𝐒𝐀𝐁𝐀 𝟐𝟎𝟐𝟔!
19-07-2026
𝐒𝐀𝐒𝐀 𝐍𝐈 𝐙𝐀𝐌𝐔 𝐘𝐀 𝐏𝐖𝐀𝐍𝐈; 𝐀𝐑𝐃𝐇𝐈 𝐘𝐀 𝐇𝐈𝐒𝐓𝐎𝐑𝐈𝐀, 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐀𝐍𝐀𝐊𝐔𝐉𝐀!!!!!
19-07-2026
𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈 𝐘𝐀𝐌𝐏𝐀 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐌𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐙𝐈 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐇𝐈𝐒𝐓𝐎𝐑𝐈𝐀
19-07-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐙𝐈𝐍𝐃𝐔𝐀 𝐒𝐇𝐈𝐍𝐀 𝐋𝐀 𝐖𝐀𝐊𝐄𝐑𝐄𝐊𝐄𝐓𝐖𝐀 𝐌𝐋𝐀𝐍𝐃𝐄𝐆𝐄, 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐒𝐀-𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀
19-07-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐒𝐇𝐈𝐍𝐀 𝐍𝐀. 𝟏𝟎 𝐌𝐀𝐅𝐈𝐅𝐈, 𝐀𝐒𝐈𝐒𝐈𝐓𝐈𝐙𝐀 𝐀𝐌𝐀𝐍𝐈, 𝐔𝐌𝐎𝐉𝐀 𝐍𝐀 𝐌𝐒𝐇𝐈𝐊𝐀𝐌𝐀𝐍𝐎
19-07-2026
𝐌𝐑𝐀𝐃𝐈 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐎 𝐘𝐀 𝐔𝐅𝐔𝐍𝐃𝐈 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎 𝐊𝐔𝐅𝐔𝐍𝐆𝐔𝐀 𝐅𝐔𝐑𝐒𝐀 𝐙𝐀 𝐀𝐉𝐈𝐑𝐀 𝐊𝐖𝐀 𝐕𝐈𝐉𝐀𝐍𝐀
19-07-2026
𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎, 𝐙𝐀𝐌𝐔 𝐘𝐄𝐍𝐔 𝐍𝐈 𝐋𝐄𝐎!
19-07-2026
𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀: 𝐃𝐊𝐓. 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐒𝐔𝐋𝐔𝐇𝐔 𝐇𝐀𝐒𝐒𝐀𝐍 𝐍𝐈 𝐌𝐓𝐄𝐊𝐄𝐋𝐄𝐙𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐀𝐇𝐈𝐑𝐈 𝐖𝐀 𝐀𝐇𝐀𝐃𝐈 𝐙𝐀 𝐂𝐂𝐌
19-07-2026
𝐒𝐈𝐌𝐔 𝐈𝐌𝐄𝐈𝐓𝐀, 𝐍𝐄𝐄𝐌𝐀 𝐘𝐀 𝐔𝐓𝐀𝐓𝐔𝐙𝐈 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎!
19-07-2026
𝐑𝐔𝐀𝐇𝐀 𝐌𝐁𝐔𝐘𝐔𝐍𝐈 𝐘𝐀𝐅𝐔𝐑𝐈𝐊𝐀; “𝐂𝐇𝐈𝐄𝐅 𝐂𝐇𝐎𝐆𝐀𝐕𝐀𝐓𝐀𝐌𝐁𝐔𝐋𝐄” 𝐀𝐊𝐈𝐓𝐄𝐊𝐀 𝐌𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐎 𝐖𝐀 𝐇𝐀𝐃𝐇𝐀𝐑𝐀!
19-07-2026
𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐎 𝐂𝐇𝐀 𝐔𝐌𝐖𝐀𝐆𝐈𝐋𝐈𝐀𝐉𝐈 𝐍𝐈 𝐔𝐅𝐔𝐍𝐆𝐔𝐎 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐏𝐈𝐍𝐃𝐔𝐙𝐈 𝐘𝐀 𝐔𝐂𝐇𝐔𝐌𝐈 𝐖𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈: 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈
19-07-2026
𝐂𝐂𝐌 𝐘𝐀𝐔𝐍𝐆𝐀 𝐌𝐊𝐎𝐍𝐎 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐖𝐀 𝐍𝐉𝐎𝐌𝐁𝐄 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐙𝐀 𝐔𝐙𝐀𝐋𝐈𝐒𝐇𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐀𝐋𝐈
19-07-2026
𝐀𝐌𝐀𝐍𝐈 𝐍𝐈 𝐌𝐒𝐈𝐍𝐆𝐈 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐄𝐍𝐃𝐄𝐋𝐄𝐎: 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈
19-07-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐑𝐀𝐒𝐌𝐈 𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀!!
19-07-2026
𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀 𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐋𝐄𝐖𝐀 𝐍𝐉𝐎𝐌𝐁𝐄, 𝐀𝐇𝐈𝐌𝐈𝐙𝐀 𝐕𝐈𝐎𝐍𝐆𝐎𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐊𝐔𝐈𝐒𝐇𝐈 𝐃𝐇𝐀𝐍𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐍𝐀 𝐔𝐓𝐔 𝐊𝐖𝐀 𝐕𝐈𝐓𝐄𝐍𝐃𝐎
19-07-2026
𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀: 𝐂𝐂𝐌 𝐇𝐀𝐈𝐓𝐀𝐕𝐔𝐌𝐈𝐋𝐈𝐀 𝐔𝐙𝐄𝐌𝐁𝐄, 𝐕𝐈𝐎𝐍𝐆𝐎𝐙𝐈 𝐖𝐀𝐖𝐀𝐉𝐈𝐁𝐈𝐊𝐄 𝐊𝐔𝐓𝐀𝐓𝐔𝐀 𝐂𝐇𝐀𝐍𝐆𝐀𝐌𝐎𝐓𝐎 𝐙𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈
19-07-2026