Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla amesema uwepo wa Maonesho ya Wiki ya elimu ya juu nchini yamekuwa yakiziweka pamoja Taasisi, vyuo na wadau wa elimu ya juu kwa lengo la kutangaza fursa mbali mbali kwa wanafunzi wanaosoma na wanaotarajia kujiunga na vyuo vikuu vya ndani na nje ya Nchi
Ameyasema hayo wakati wa ufunguzi wa maonesho ya Tano(5) ya wiki ya elimu ya juu Zanzibar yaliyofanyika katika viwanja vya Maisara Mkoa wa Mjini Magharibi.
Mhe. Hemed amesema kupitia maonesho ya wiki ya elimu ya juu wanafunzi hupatiwa fursa mbali mbali za kimasomo ikiwemo upatikanaji wa mikopo, namna ya kujiunga na vyuo vya ndani na nje ya nchi na kutoa hamasa kwa wanafunzi kusoma kwa bidii na kujiendeleza katika ngazi ya elimu ya juu.
Amesema kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2020-2025, Sera na Dira ya Maendeleo ya mwaka 2050, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar imekuwa ikichukua hatua mbali mbali za uboreshaji wa elimu ikiwemo kuweka mageuzi makubwa kuanzia ngazi ya maandalizi hadi elimu ya juu kwa kuwawezesha wanafunzi kupata ujuzi na maarifa baada ya kumaliza masomo yao.
Aidha Serikali imeongeza Bajeti ya Bodi ya Mikopo ya elimu ya juu Zanzibar kutoka fedha za Kitanzania shilingi Bilioni 26.95 kwa mwaka wa fedha 2024 hadi kufikia Bilioni 30.5 kwa mwaka 2025 ambazo zitakwenda kuwanufaisha wanafunzi zaidi ya 7,367 ambapo kwa mara ya kwanza wanafuzi 1,000 wa ngazi ya Diploma watanufaika pia na mikopo hio.
Amefahamisha kuwa Serikali imeendelea kuimarisha huduma kwa wanafunzi wa vyuo vikuu ikiwemo kuwapatia Bima ya Afya pamoja na kuongeza fedha za kujikimu kwa wanafunzi wote wanaosoma Vyuo vya Zanzibar na vyuo vya Tanzania Bara.
Sambamba na hayo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar ametoa wito kwa wanafunzi na wananchi kwa ujumla kujitokeza na kuitumia vyema wiki ya maonesho kwa kujielimisha juu ya upatikanaji wa fursa mbali mbali za elimu ndani na nje ya nchi na kuwasisitiza wanafunzi kusoma kwa bidiii na kuzitumia vyema fursa wanazozipata pamoja na kuepuka kutumika kwa misingi yoyote ambayo itapelekea kuvuruga umoja na amani iliyopo nchini
Nae Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe. Lela Mohamed Mussa amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inayoongozwa na Rais Dkt Hussen Mwinyi inafanya kazi kubwa na nzuri katika kuimarisha miundombinu ya elimu inayopelekea kuongezeka kwa kiwango cha ufaulu jambo ambalo linaendelea kuiletea heshima zanzibar.
Mhe. Lela amesema ufaulu wa wanafunzi wa kidato cha sita unaongezeka mwaka hadi mwaka na kufikia asilimia 99.5% kwa mwaka 2024, ambapo zaidi ya wanafuzi 3,387 wamepata ufaulu wa daraja la kwanza hadi la tatu na wote wanatarajiwa kujiunga na vyuo vikuu mbali mbali ndani na nje ya nchi, hivyo kupitia maonesho ya juma la elimu ya juu yatawasaidia katika kufanya udahili wa vyuo na kupata taaluma juu ya kupata mikopo ya elimu juu iatakayowawezesha kusoma pasipo na changamoto ya aina yoyote.
Akisoma taarifa ya kitaaluma kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Naibu katibu Mkuu Utawala (WEMA) Khalid Massoud Waziri amesema lengo kuu la maonesho hayo ni kuimarisha mashirikiano baina ya Taasisi za Elimu, Vyuo na Mabenki ili kuhakikisha Sekta ya Elimu nchini inaendelea kuimarika na kiwango cha ufaulu kuzidi kuongezeka siku hadi siku.
Khalid amesema maonesho hayo ya juma la Elimu ya juu yanazidi kuimarika mwaka hadi mwaka ambapo kwa mwaka huu washiriki wameongezeka kutoka washiriki 17 mwaka 2020 hadi washiriki 77 mwaka 2024 na kutoa fursa kwa wanafunzi kupata kujua ni namna gani wanaweza kujiunga na vyou vikuu vya ndani na nje ya nchi samabamba na kupata kujua ni namna gani mwanafuzni anapata fursa ya kufanya maombi ya mikopo kwa taasisi husika.
Mapema Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar ametembelea Mbanda ya washiriki wa maonesho ya juma la Elimu ya juu na kupata elimu na huduma zinazotolewa katika mabanda hayo
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
19-03-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
19-03-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
19-03-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
19-03-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
19-03-2026
πππ¦πππ‘ππ’ πππ πππ§. π ππππ₯π’ ππππ£π’πππππͺπ ππͺπ π¦πππ‘ππͺπ πππ₯ ππ¦ π¦πππππ
19-03-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
19-03-2026
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
19-03-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
19-03-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
19-03-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
19-03-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
19-03-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
19-03-2026
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
19-03-2026
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
19-03-2026
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
19-03-2026
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
19-03-2026
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
19-03-2026
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
19-03-2026
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
19-03-2026