Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe Hemed Suleiman Abdulla amesema Serikali ya Awamu ya Nane (8) kupitia Ilani ya Uchaguzi ya Mwaka 2020-2025, Dira ya Maendeleo ya Zanzibar ya Mwaka 2050, Sera na Mikakati mbali mbali imekuwa ikiendelea kuimarisha Sekta ya Uwekezaji nchini kwa kuweka mazingira bora ambayo yanawavutia wawekezaji kuja kuekeza Zanzibar.
Ameyasema hayo katika hafla ya uwekaji wa Jiwe la Msingi la Mradi wa Hoteli ya Mada yenye hadhi ya Nyota Tano (5) iliyoko Michanvi Kae Mkoa wa Kusini Unguja ikiwa ni katika shamra shamra za kutimia miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Amesema kuwa Serikali inaendelea kuimarisha na kujenga miundombinu ya Barabara na Viwanja vya ndege sambamba na kuimarisha upatikanaji wa huduma za nishati, maji safi na salama na huduma nyengine za kijamii ili kuendelea kuweka mazingira mazuri kwa wawekezaji.
Mhe Hemed amefahamisha kuwa Mradi wa Ujenzi wa Hotel Mada unaomilikiwa na kampuni ya MADA HOTEL TANZANIA LIMITED hadi kukamilika kwake unatarajiwa kugharimu USD 6,500 utakaokuwa na vyumba mia moja(100) vya kulaza wageni na kusaidia kuzalisha ajira zaidi ya mia mbili (200) kwa vijana ambapo amewataka wawekezaji wa mradi huo kutoa kipaumbele cha ajira kwa wakaazi wa Michanvi na vijiji jirani.
Aidha Makamu wa Pili wa Rais amewasihi vijana ambao watapata ajira katika mradi huo kuwa waaminifu na kufanya kazi kwa bidii ili waendelee kuaminika katika majukumu watakayopangiwa sambamba na kuwataka wawekezaji wa mahoteli kutekeleza wajibu wao hasa katika kulipa kodi stahiki, kuwatendea haki wafanyakazi wao pamoja na kushirikiana na wananchi wanaoishi maeneo yanayowazunguka ili kudumisha amani na utulivu uliopo nchini.
Nae Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, kazi, Uchumi na Uwekezaji Mhe Mudrik Ramadhan Soraga amewataka wale wote waliopewa maeneo kwa ajili ya shuhuli za Uwekezaji kuyatumia maeneo hayo kama walivyopangiwa na Serikali na kuacha tabia ya kutoyatumia maeneo hayo na hatimae kuwa magofu jambo ambalo linarejesha nyuma malengo ya serikali.
Soraga amesema Sheria mpya ya uwekezaji ambayo inatarajiwa kusainiwa hivi karibuni imeainisha hatua zitakazochukuliwa kwa muwekezaji ambaye atazuwia eneo la uwekezaji pasipo kulifanyia shuhuli stahiki ikiwa ni pamoja na kurudishwa serikalini eneo hilo na kupewa wawekezaji wengine kwa maslahi ya taifa.
Amesema kuwa Mamlaka ya kukuza Uwekezaji Zanzibar(ZIPA) inafanya kazi kwa haraka na ufanisi mkubwa ili kuhakikisha upatikanaji wa huduma katika mamlaka hiyo unakuwa wa rahisi na kwa wakati muafaka.
Mapema Mkurugenzi Mtendajeji wa Mamlaka ya uwekezaji Zanzibar Ndugu sharif Ali Sharif amemshukuru muwekezaji kwa kuendelea kuiamini Zanzibar na kuja kufanya uwekezaji mkubwa ambao utatoa ajira nyingi kwa wazawa na kuipatia pato Serikali ya Zanzibari jambo litakalosadia katika kukuza uchumi wa Taifa letu.
Amesema mradi huo wa hoteli yenye hadhi ya nyota tano utagharimu jumla ya Dola milioni 30 na kutoa ajira zaidi ya watu 250 jaambo ambalo utakuza kipato cha mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla.
Nae Muwekezaji wa Shukurani Palece Hotel Bwana TARLOCHAN MHANJAN amesema sababu kubwa ya kuja kuwekeza Zanzibar ni uzuri wa Visiwa vyenyewe na hali ya hewa inayopatikana, mazingira mazuri na ushirikiano wanaopatiwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar sambamba na utayari wa wananchi wake kushirikiana na wawekazaji mambo ambayo yanawapelekea kufanya kazi zao kwa utulivu mkubwa.
Amesema kuwa Shukurani Palece Hotel inathamini na kuunga mkono Mapinduzi ya Zanzibar ambayo ndio msingi wa uwepo wa Amani na Utulivu uliosababisha uwepo wao hapa Visiwani Zanzibar.
KIPINDI MAALUMU
08-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐒𝐈𝐌𝐀𝐌𝐈𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐒𝐀𝐅𝐀𝐑𝐀 𝐊𝐔𝐒𝐀𝐋𝐈𝐌𝐈𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐍𝐀 𝐊𝐈𝐉𝐈𝐖𝐄 𝐂𝐇𝐀 𝐂𝐇𝐀𝐃𝐄𝐌𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈
08-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐊𝐈𝐓𝐔𝐎 𝐂𝐇𝐀 𝐀𝐅𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐋𝐎𝐋𝐄𝐍𝐈, 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈
08-06-2026
𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐘𝐀𝐀𝐌𝐁𝐈𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐂𝐇𝐀𝐆𝐔𝐀 𝐌𝐀𝐄𝐍𝐃𝐄𝐋𝐄𝐎 𝐁𝐀𝐃𝐀𝐋𝐀 𝐘𝐀 𝐌𝐀𝐀𝐍𝐃𝐀𝐌𝐀𝐍𝐎
08-06-2026
𝐌𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐙𝐈 𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐓𝐈𝐁𝐔 𝐖𝐀 𝐍𝐄𝐂, 𝐈𝐓𝐈𝐊𝐀𝐃𝐈, 𝐔𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐍𝐀 𝐌𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐎 𝐂𝐂𝐌, 𝐍𝐃𝐔𝐆𝐔 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐋𝐀𝐁𝐀𝐍 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈, 𝐎𝐅𝐈𝐒𝐈 𝐙𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈
08-06-2026
𝐒𝐀𝐒𝐀 𝐍𝐈 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈, 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐃𝐎 𝐌𝐃𝐔𝐍𝐃𝐎!
08-06-2026
𝐀𝐑𝐔𝐌𝐄𝐑𝐔 𝐘𝐀𝐒𝐈𝐊𝐈𝐀 𝐖𝐈𝐓𝐎 𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐋𝐈𝐍𝐃𝐀 𝐌𝐀𝐀𝐃𝐈𝐋𝐈 𝐍𝐀 𝐇𝐀𝐊𝐈 𝐙𝐀 𝐖𝐀𝐓𝐎𝐓𝐎
08-06-2026
𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐒𝐀𝐌𝐁𝐀𝐙𝐀 𝐔𝐏𝐄𝐍𝐃𝐎 𝐖𝐀 𝐀𝐆𝐀𝐏𝐄 𝐊𝐖𝐄𝐍𝐘𝐄 𝐊𝐈𝐉𝐈𝐖𝐄 𝐂𝐇𝐀 𝐂𝐇𝐀𝐃𝐄𝐌𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐌𝐄𝐑𝐔
08-06-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐀𝐍𝐙𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐌𝐄𝐑𝐔 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐊𝐀𝐆𝐔𝐀 𝐔𝐇𝐀𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐇𝐀𝐌𝐀
08-06-2026
𝐌𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐎 𝐖𝐀 𝐇𝐀𝐃𝐇𝐀𝐑𝐀 𝐖𝐀 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐑𝐀𝐓𝐔 - 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀
08-06-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐓𝐔𝐍𝐔𝐊𝐈𝐖𝐀 𝐒𝐇𝐀𝐇𝐀𝐃𝐀 𝐘𝐀 𝐇𝐄𝐒𝐇𝐈𝐌𝐀 𝐔𝐑𝐔𝐒𝐈
08-06-2026
𝐀𝐑𝐔𝐌𝐄𝐑𝐔, 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐀𝐍𝐀𝐊𝐔𝐉𝐀!
08-06-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐑𝐀𝐒𝐌𝐈 𝐔𝐑𝐔𝐒𝐈, 𝐀𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐀 𝐍𝐀 𝐏𝐔𝐓𝐈𝐍
08-06-2026
𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎, 𝐓𝐔𝐍𝐀𝐊𝐔𝐉𝐀
08-06-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐃𝐊𝐓. 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐌𝐎𝐒𝐂𝐎𝐖, 𝐔𝐑𝐔𝐒𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀
08-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐒𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐈𝐑𝐎 𝐊𝐖𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐊𝐀𝐙𝐈
08-06-2026
𝐅𝐔𝐍𝐆𝐀 𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐍𝐘𝐀𝐑𝐀 𝐋𝐄𝐎!!!
08-06-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐒𝐇𝐈𝐍𝐀 𝐍𝐀. 𝟐 𝐊𝐀𝐓𝐀 𝐘𝐀 𝐁𝐎𝐍𝐆𝐀
08-06-2026
𝐁𝐀𝐁𝐀𝐓𝐈 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈 𝐋𝐄𝐎 𝐓𝐔𝐍𝐀𝐈𝐅𝐔𝐍𝐈𝐊𝐀!!!
08-06-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐀 𝐍𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐇𝐀𝐍𝐀𝐍𝐆, 𝐀𝐒𝐈𝐊𝐈𝐋𝐈𝐙𝐀 𝐍𝐀 𝐊𝐔𝐓𝐀𝐓𝐔𝐀 𝐊𝐄𝐑𝐎 𝐙𝐀𝐎
08-06-2026