MAKAMU WA PILI ZANZIBAR MHE. HEMED SULEIMAN AZINDUA BARAZA LA MANISPAA LA CHAKE CHAKE PEMBA
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla ameutaka uongozi wa Baraza la Mji la Chake Chake Pemba ambalo limepandishwa hadhi na kuwa Baraza la Manispaa Chake Chake kuhakikisha wanasimamia vyema vyanzo na ukusanyaji mzuri wa mapato ili kuweza kutoa huduma bora kwa wananchi.Ameyasema hayo wakati akizindua Baraza la Manispaa Chake Chake Pemba katika Viwanja vya Tibirinzi Pemba Mhe. Hemed ameipongeza Serikali ya Awamu ya nane inayoongozwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi kwa kasi kubwa ya kuimarisha utendaji kazi katika Serikali za Mitaa na kuridhia mapendekezo ya kulipandisha hadhi Baraza la Mji Chake Chake na kuwa Baraza la Manispaa Chake Chake Pemba kwa kuzingatia Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984.
Amesema kuwa matarajio ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuwa Baraza hilo jipya litahakikisha huduma za kijamii zinakuwa bora na za ufanisi zaidi ambazo zitawaondolea usumbufu wananchi kwa kupata huduma hizo pamoja na kuandaa mipango bora ya kimkakati itakayotoa tija kwa Wananchi na Serikali kwa ujumla.
Aidha Mhe. Hemed amewasisitiza Watendaji wa Baraza la Manispaa Chake Chake kusimamia vyema makusanyo kwa kutumia mifumo ya risiti za kielektroniki, kuwa na matumizi sahihi ya rasilimali watu na rasilimali fedha, kuibua Miradi mbali mbali ya maendeleo, kuimrisha usafi wa mazingira na kusimamia Amani na mshikamano katika jamii.
Amelitaka Baraza la Manispaa Chake Chake Pemba na watendaji wake kukemea vitendo vya rushwa na utumiaji mzuri wa rasilimali za Serikali, kuacha ,uhali na kutanguliza maslahi ya Taifa ili kuwa Baraza la mfano litakalotoa hamasa wa ushindani wa kimaendeleo kwa kuongeza mapato Serikalini na kuzitumia fursa mbali mbali zinazopatikana katika Wilaya hiyo.
Ameutaka Uongozi wa Serikali ya Mkoa wa Kusini Pemba kuwa na mipango shirikishi jamii kwa kuzishirikisha Kamati za mashauriano za Shehia na Mabaraza ya wadi, Kamati za Wilaya na Mikoa ili kupata mazingatio na ushauri katika maendeleo.
Sambamba hayo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amefahamisha kuwa endapo Mabaraza ya Manispaa na Miji Zanzibar yatatekeleza majukumu yao kama yalivyoainishwa katika Sheria ya Serikali za Mitaa yataleta matokeo mazuri yenye tija na kuepusha Migogoro katika jamii.
Pamoja na hayo amempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi kwa kuridhia Baraza la Mji la Chake Chake Chake kupandishwa hadhi na kuwa Baraza la Manispaa kumetokana na miongozo na maelekezo yake kwa watendaji wa Baraza hilo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Idara Maalum za SMZ Mhe. Masoud Ali Mohamed ameishukuru Serikali ya Awamu ya nane inayoongozwa na Rais Dkt. Hussein Ali Mwinyi kwa kuridhia kulipandisha hadhi Baraza la Manispaa Chake Chake ni kurahisisha kasi ya upatikanaji wa maendeleo na ukuwaji wa uchumi ndani ya Mkoa huo.
Aidha amewataka watendaji wa Baraza la Manispaa Chake Chake kwa kushirikiana na wananchi kuongeza kasi katika utendaji wao wa kazi, kuwa wabunifu wa miradi mbali mbali itakayowaongezea kipato kitakachosaidia kukuza uchumi hasa katika Mkoa huo.
Amesema mashirikiano ndio silaha katika kutimiza majukumu yetu ya kazi na kuwataka kuachana na kufanya kazi kwa utashi binafsi na kuelekeza nguvu zao katika kulitumikia Taifa.
Sambamba na hayo Mhe. Masoud amemuhakikisha makamu wa pili wa rais wa Zanzibar wizara itahakikisha inafata maelekezo na maagizo yote yanayotolewa na viongozi wakuu wa nchi katika kuwaleetea maendeleo wananchi wote pamoja na kuifata ilani ya chama cha mapinduzi ya kuwaletea maendeleo wananchi wake.
Nae Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Mhe. Mattar Zahor Massoud amesema endapo viongozi watafanya kazi kwa pamoja hasa katika shuhuli za maendeleo na kuwataka kuachana na tabia ya kukwamisha na kuzorotesha Miradi mbali mbali ya maendeleo kwani kufanya hivyo ni kuikwamisha Serikali kwa ujumla.
Mhe. Mattar ameahidi kufanya kazi kwa bidii kwa kushirikiana na viongozi na wananchi kwa kufuata miongozo ya Nchi na kamwe hatokatishwa tamaa na wachache wasioitakia mema nchi yetu na amesema jitihada pekee ndio zitakazolipandisha zaidi Baraza hilo la Manispaa kuwa Jiji muda mfupi ujao.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Baraza la Manispaa chake chake Ndugu Maulid Mwalim Ali amesema kupandisha hadhi kwa baraza la manispaa la chake chake kutawajengea ari na morali wafanyakazi katika kufanya kazi kwa umakini na weledi wa hali ya juuu katika kufanikisha malengo ya serikali iliyojiwekea katika kuwaletea maendeleo wananchi wake.
Amesema Baraza la Manispaa Chake Chake litahakikisha linaendelea kuimarisha ukusanyaji wa mapato, kuimarisha usafi wa mazingira na kuendelea kutekeleza miradi mbali mbali ya kimaendeleo pamoja na kuwapatia elimu zaidi wafanyakazi ili kuleta ufanisi nzuri wa kazi.
Aidha amesema Baraza la Manispaa Chake chake litafanyakazi kwa kasi na ufanisi zaidi ili kuhakikisha linapanda hadhi Zaidi kwa maslahi ya wanachi na Taifa kwa ujumla
𝐒𝐀𝐒𝐀 𝐍𝐈 𝐙𝐀𝐌𝐔 𝐘𝐀 𝐏𝐖𝐀𝐍𝐈; 𝐀𝐑𝐃𝐇𝐈 𝐘𝐀 𝐇𝐈𝐒𝐓𝐎𝐑𝐈𝐀, 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐀𝐍𝐀𝐊𝐔𝐉𝐀!!!!!
04-07-2026
𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈 𝐘𝐀𝐌𝐏𝐀 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐌𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐙𝐈 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐇𝐈𝐒𝐓𝐎𝐑𝐈𝐀
04-07-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐙𝐈𝐍𝐃𝐔𝐀 𝐒𝐇𝐈𝐍𝐀 𝐋𝐀 𝐖𝐀𝐊𝐄𝐑𝐄𝐊𝐄𝐓𝐖𝐀 𝐌𝐋𝐀𝐍𝐃𝐄𝐆𝐄, 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐒𝐀-𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀
04-07-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐒𝐇𝐈𝐍𝐀 𝐍𝐀. 𝟏𝟎 𝐌𝐀𝐅𝐈𝐅𝐈, 𝐀𝐒𝐈𝐒𝐈𝐓𝐈𝐙𝐀 𝐀𝐌𝐀𝐍𝐈, 𝐔𝐌𝐎𝐉𝐀 𝐍𝐀 𝐌𝐒𝐇𝐈𝐊𝐀𝐌𝐀𝐍𝐎
04-07-2026
𝐌𝐑𝐀𝐃𝐈 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐎 𝐘𝐀 𝐔𝐅𝐔𝐍𝐃𝐈 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎 𝐊𝐔𝐅𝐔𝐍𝐆𝐔𝐀 𝐅𝐔𝐑𝐒𝐀 𝐙𝐀 𝐀𝐉𝐈𝐑𝐀 𝐊𝐖𝐀 𝐕𝐈𝐉𝐀𝐍𝐀
04-07-2026
𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎, 𝐙𝐀𝐌𝐔 𝐘𝐄𝐍𝐔 𝐍𝐈 𝐋𝐄𝐎!
04-07-2026
𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀: 𝐃𝐊𝐓. 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐒𝐔𝐋𝐔𝐇𝐔 𝐇𝐀𝐒𝐒𝐀𝐍 𝐍𝐈 𝐌𝐓𝐄𝐊𝐄𝐋𝐄𝐙𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐀𝐇𝐈𝐑𝐈 𝐖𝐀 𝐀𝐇𝐀𝐃𝐈 𝐙𝐀 𝐂𝐂𝐌
04-07-2026
𝐒𝐈𝐌𝐔 𝐈𝐌𝐄𝐈𝐓𝐀, 𝐍𝐄𝐄𝐌𝐀 𝐘𝐀 𝐔𝐓𝐀𝐓𝐔𝐙𝐈 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎!
04-07-2026
𝐑𝐔𝐀𝐇𝐀 𝐌𝐁𝐔𝐘𝐔𝐍𝐈 𝐘𝐀𝐅𝐔𝐑𝐈𝐊𝐀; “𝐂𝐇𝐈𝐄𝐅 𝐂𝐇𝐎𝐆𝐀𝐕𝐀𝐓𝐀𝐌𝐁𝐔𝐋𝐄” 𝐀𝐊𝐈𝐓𝐄𝐊𝐀 𝐌𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐎 𝐖𝐀 𝐇𝐀𝐃𝐇𝐀𝐑𝐀!
04-07-2026
𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐎 𝐂𝐇𝐀 𝐔𝐌𝐖𝐀𝐆𝐈𝐋𝐈𝐀𝐉𝐈 𝐍𝐈 𝐔𝐅𝐔𝐍𝐆𝐔𝐎 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐏𝐈𝐍𝐃𝐔𝐙𝐈 𝐘𝐀 𝐔𝐂𝐇𝐔𝐌𝐈 𝐖𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈: 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈
04-07-2026
𝐂𝐂𝐌 𝐘𝐀𝐔𝐍𝐆𝐀 𝐌𝐊𝐎𝐍𝐎 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐖𝐀 𝐍𝐉𝐎𝐌𝐁𝐄 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐙𝐀 𝐔𝐙𝐀𝐋𝐈𝐒𝐇𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐀𝐋𝐈
04-07-2026
𝐀𝐌𝐀𝐍𝐈 𝐍𝐈 𝐌𝐒𝐈𝐍𝐆𝐈 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐄𝐍𝐃𝐄𝐋𝐄𝐎: 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈
04-07-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐑𝐀𝐒𝐌𝐈 𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀!!
04-07-2026
𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀 𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐋𝐄𝐖𝐀 𝐍𝐉𝐎𝐌𝐁𝐄, 𝐀𝐇𝐈𝐌𝐈𝐙𝐀 𝐕𝐈𝐎𝐍𝐆𝐎𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐊𝐔𝐈𝐒𝐇𝐈 𝐃𝐇𝐀𝐍𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐍𝐀 𝐔𝐓𝐔 𝐊𝐖𝐀 𝐕𝐈𝐓𝐄𝐍𝐃𝐎
04-07-2026
𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀: 𝐂𝐂𝐌 𝐇𝐀𝐈𝐓𝐀𝐕𝐔𝐌𝐈𝐋𝐈𝐀 𝐔𝐙𝐄𝐌𝐁𝐄, 𝐕𝐈𝐎𝐍𝐆𝐎𝐙𝐈 𝐖𝐀𝐖𝐀𝐉𝐈𝐁𝐈𝐊𝐄 𝐊𝐔𝐓𝐀𝐓𝐔𝐀 𝐂𝐇𝐀𝐍𝐆𝐀𝐌𝐎𝐓𝐎 𝐙𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈
04-07-2026
𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀 𝐓𝐔𝐍𝐀𝐊𝐔𝐉𝐀𝐀𝐀, 𝐓𝐔𝐍𝐀𝐀𝐍𝐙𝐈𝐀 𝐑𝐔𝐀𝐇𝐀 𝐌𝐁𝐔𝐘𝐔𝐍𝐈!
04-07-2026
𝐌𝐈𝐊𝐎𝐏𝐎 𝐘𝐀 𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈𝐌𝐈𝐀 𝟏𝟎% 𝐘𝐀𝐂𝐇𝐎𝐂𝐇𝐄𝐀 𝐔𝐂𝐇𝐔𝐌𝐈 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐊𝐔𝐍𝐃𝐈 𝐌𝐀𝐀𝐋𝐔𝐌
04-07-2026
𝐍𝐃𝐆 𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀 𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐋𝐄𝐖𝐀 𝐑𝐔𝐕𝐔𝐌𝐀, 𝐀𝐇𝐈𝐌𝐈𝐙𝐀 𝐔𝐌𝐎𝐉𝐀 𝐍𝐀 𝐌𝐒𝐇𝐈𝐊𝐀𝐌𝐀𝐍𝐎 𝐍𝐃𝐈𝐎 𝐍𝐆𝐔𝐕𝐔 𝐘𝐀 𝐂𝐂𝐌
04-07-2026
𝐊𝐇𝐄𝐑𝐈 𝐘𝐀 𝐒𝐈𝐊𝐔 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐌𝐀𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐘𝐀 𝐌𝐓𝐎𝐓𝐎 𝐖𝐀 𝐀𝐅𝐑𝐈𝐊𝐀
04-07-2026
𝐌𝐇𝐄. 𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐀𝐍𝐀𝐖𝐀𝐏𝐄𝐍𝐃𝐀 𝐒𝐀𝐍𝐀 𝐖𝐀𝐓𝐀𝐍𝐙𝐀𝐍𝐈𝐀, 𝐖𝐀𝐓𝐔𝐌𝐈𝐒𝐇𝐈 𝐖𝐀 𝐔𝐌𝐌𝐀 𝐓𝐈𝐌𝐈𝐙𝐄𝐍𝐈 𝐖𝐀𝐉𝐈𝐁𝐔 𝐖𝐄𝐍𝐔 𝐊𝐈𝐊𝐀𝐌𝐈𝐋𝐈𝐅𝐔: 𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀
04-07-2026