MAKAMU WA PILI WA RAIS WA ZANZIBAR MHE HEMED SULEIMAN ABDULLA AMESEMA SERIKALI YA ZANZIBAR INAENDELEA KUWEKA MAZINGIRA BORA ILI KUEPUKANA NA MAGONJWA YA MIRIPUKO NA KUCHUKUA HATUA ZA MATIBABU PINDI MAGONJWA HAYO YATAKAPOJITOKEZA.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe Hemed Suleiman Abdulla amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inaendelea kuweka mazingira bora ya kuweza kuepukana na magonjwa mbali mbali ya miripuko sambamba na kuchukua hatua za matibabu pindi magonjwa hayo yatakapojitokeza.
Ameyasema hayo katika Uzinduzi wa Kituo cha Mawasiliano ya Magonjwa ya Miripuko (Zanzibar Afya Call Center) katika Viwanja vya Magomeni - Sogea Zanzibar.
Mhe. Hemed amesema Sekta ya Afya Zanzibar imekuwa ikichukua hatua mbali mbali katika kuboresha upatikanaji na utowaji wa huduma bora pamoja na kudhibiti magonjwa ya miripuko ambayo yalikuwa na changamoto kubwa kutokana na kutokuwa na njia bora za mawasiliano kutoka kwa mwananchi kwenda katika Mifumo ya Afya ili kuweza kupatiwa suluhisho la chanamoto hio.
Amefahamisha kuwa Zanzibar ni miongoni mwa nchi zilizokumbwa na Janga la COVID 19 ambalo lilipoteza maisha ya watu wengi na kuathiri mifumo ya uchumi kutokana na ugumu uliokuwepo wa kusambaza taarifa kutoka kwa wananchi kwenda Serikalini juu ya ugonjwa huo.
Amesema kuwa uzinduzi wa kituo hicho cha mawasiliano kitakuwa ni muarubaini utakaorahisisha upatikanaji wa mawasiliano baina ya wananchi na watoa huduma za Afya pindi magonjwa ya miripuko na dharura yatakapojitokeza sambamba na kuwataka wananchi kukitumia kituo hicho kama kilivyokusudiwa ili kurahisisha upatikanaji wa huduma bora na kwa wakati husika.
Aidha Mhe Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amesema kuwepo kwa kituo hicho kitatoa faida nyingi kwa wananchi ikiwa ni pamoja na mgonjwa kuelekezwa sehemu sahihi ya kupata matibabu kulingana na ugonjwa wake kwa kufuata utaratibu uliowekwa na Wizara ya Afya .
Sambamba na hayo amesema Kituo cha mawasiliano ya magonjwa ya miripuko kitawasaidia wananchi kufahamu juu ya Mfuko wa wa Huduma za Bima ya Afya Zanzibar ikiwemo namna ya kujiunga, masharti, faida na wanufaika wa amfuko huo pamoja na kuwaunganisha watalii na wageni mbali mbali ambao watapatiwa taarifa za huduma za Afya zinazopatikana hapa Zanzibar .
Mheshimiwa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar ametoa wito kwa Uongozi wa Wizara ya Afya kuendelea kukitunza kituo hicho kwa kuhakikisha mambo ya msingi yanayohitajika katika kuleta ufanisi wa utowaji wa huduma bora yanapatikana, kuwepo kwa mafundi watakaotoa msaada wa marekebisho pindi watakapohitajika na kuwa na ulinzi wa uhakika kwa masaa ishirini na nne (24) ili kufikia malengo yaliyowekwa na serikali.
Nae Waziri wa Afya Mhe. Nassor Ahmed Mazrui amesema uendeshaji wa kituo hicho unahitaji fedha na nyenzo za kutosha ili kiweze kufanya kazi kwa ufanisi na uweledi wa kuweza kuwahudumia Wazanzibari na wageni wanaoingia nchini kwa wakati.
Mhe. Mazrui amewataka wahudumu wa kituo hicho kufanya kazi kwa uaminifu na uadilifu mkubwa, Ari na kasi zaidi ili kuendana na kasi ya serikali ya awamu ya nane (8) inayoongozwa na Dkt. Hussein Ali Mwinyi ya kuwatumikia wazanzibar na kutoa huduma bora za afya kwa wote.
Kwa upande wake Mwakilishi kutoka UNICEF Bibi. AWETY ATIE amesema Shirika la UNICEF limekuwa likishirikiana kwa karibu ba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kutekeleza miradi mbali mbali ya Maendeleo ikiwemo kukikarabati kituo cha Mawasiliano ya Magonjwa ya Mripuko ili kuweza kufanya kazi kwa ufanisi na kupambana na magonjwa ya mripoko yanatotokea nchini.
Amesema UNICEF itaendelea kutoa misaada na mashirikiano kwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kukiendesha kituo hicho kwa muda wa miaka mitano (5) ambacho kitafanya kazi kwa Mfumo wa kidijitali pamoja na kutoa na kupokea taarifa mbali mbali zinazohusiana na masuala ya Afya.
Aidha Bibi. ATIE amewataka wananchi wa Zanziabar kukitumia kituo hicho pale wanapopatwa na dharura ama kutaka kupatiwa ufafanuzi na ufumbuzi juu ya masuala ya Afya kwa kupiga simu bure kwa namba 190 ama kutuma ujumbe mfupi wa maandishi kupitia namba 30 ili kuweza kupatiwa ufumbuzi juu ya tatizo linalowakabili kwa wakati husika.
KIPINDI MAALUMU
08-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐒𝐈𝐌𝐀𝐌𝐈𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐒𝐀𝐅𝐀𝐑𝐀 𝐊𝐔𝐒𝐀𝐋𝐈𝐌𝐈𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐍𝐀 𝐊𝐈𝐉𝐈𝐖𝐄 𝐂𝐇𝐀 𝐂𝐇𝐀𝐃𝐄𝐌𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈
08-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐊𝐈𝐓𝐔𝐎 𝐂𝐇𝐀 𝐀𝐅𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐋𝐎𝐋𝐄𝐍𝐈, 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈
08-06-2026
𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐘𝐀𝐀𝐌𝐁𝐈𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐂𝐇𝐀𝐆𝐔𝐀 𝐌𝐀𝐄𝐍𝐃𝐄𝐋𝐄𝐎 𝐁𝐀𝐃𝐀𝐋𝐀 𝐘𝐀 𝐌𝐀𝐀𝐍𝐃𝐀𝐌𝐀𝐍𝐎
08-06-2026
𝐌𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐙𝐈 𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐓𝐈𝐁𝐔 𝐖𝐀 𝐍𝐄𝐂, 𝐈𝐓𝐈𝐊𝐀𝐃𝐈, 𝐔𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐍𝐀 𝐌𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐎 𝐂𝐂𝐌, 𝐍𝐃𝐔𝐆𝐔 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐋𝐀𝐁𝐀𝐍 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈, 𝐎𝐅𝐈𝐒𝐈 𝐙𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈
08-06-2026
𝐒𝐀𝐒𝐀 𝐍𝐈 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈, 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐃𝐎 𝐌𝐃𝐔𝐍𝐃𝐎!
08-06-2026
𝐀𝐑𝐔𝐌𝐄𝐑𝐔 𝐘𝐀𝐒𝐈𝐊𝐈𝐀 𝐖𝐈𝐓𝐎 𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐋𝐈𝐍𝐃𝐀 𝐌𝐀𝐀𝐃𝐈𝐋𝐈 𝐍𝐀 𝐇𝐀𝐊𝐈 𝐙𝐀 𝐖𝐀𝐓𝐎𝐓𝐎
08-06-2026
𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐒𝐀𝐌𝐁𝐀𝐙𝐀 𝐔𝐏𝐄𝐍𝐃𝐎 𝐖𝐀 𝐀𝐆𝐀𝐏𝐄 𝐊𝐖𝐄𝐍𝐘𝐄 𝐊𝐈𝐉𝐈𝐖𝐄 𝐂𝐇𝐀 𝐂𝐇𝐀𝐃𝐄𝐌𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐌𝐄𝐑𝐔
08-06-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐀𝐍𝐙𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐌𝐄𝐑𝐔 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐊𝐀𝐆𝐔𝐀 𝐔𝐇𝐀𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐇𝐀𝐌𝐀
08-06-2026
𝐌𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐎 𝐖𝐀 𝐇𝐀𝐃𝐇𝐀𝐑𝐀 𝐖𝐀 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐑𝐀𝐓𝐔 - 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀
08-06-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐓𝐔𝐍𝐔𝐊𝐈𝐖𝐀 𝐒𝐇𝐀𝐇𝐀𝐃𝐀 𝐘𝐀 𝐇𝐄𝐒𝐇𝐈𝐌𝐀 𝐔𝐑𝐔𝐒𝐈
08-06-2026
𝐀𝐑𝐔𝐌𝐄𝐑𝐔, 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐀𝐍𝐀𝐊𝐔𝐉𝐀!
08-06-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐑𝐀𝐒𝐌𝐈 𝐔𝐑𝐔𝐒𝐈, 𝐀𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐀 𝐍𝐀 𝐏𝐔𝐓𝐈𝐍
08-06-2026
𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎, 𝐓𝐔𝐍𝐀𝐊𝐔𝐉𝐀
08-06-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐃𝐊𝐓. 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐌𝐎𝐒𝐂𝐎𝐖, 𝐔𝐑𝐔𝐒𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀
08-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐒𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐈𝐑𝐎 𝐊𝐖𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐊𝐀𝐙𝐈
08-06-2026
𝐅𝐔𝐍𝐆𝐀 𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐍𝐘𝐀𝐑𝐀 𝐋𝐄𝐎!!!
08-06-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐒𝐇𝐈𝐍𝐀 𝐍𝐀. 𝟐 𝐊𝐀𝐓𝐀 𝐘𝐀 𝐁𝐎𝐍𝐆𝐀
08-06-2026
𝐁𝐀𝐁𝐀𝐓𝐈 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈 𝐋𝐄𝐎 𝐓𝐔𝐍𝐀𝐈𝐅𝐔𝐍𝐈𝐊𝐀!!!
08-06-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐀 𝐍𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐇𝐀𝐍𝐀𝐍𝐆, 𝐀𝐒𝐈𝐊𝐈𝐋𝐈𝐙𝐀 𝐍𝐀 𝐊𝐔𝐓𝐀𝐓𝐔𝐀 𝐊𝐄𝐑𝐎 𝐙𝐀𝐎
08-06-2026