Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inatambua mchango mkubwa Unaotolewa na Mashirika ya Umma na itaendelea kuchukua juhudi mbali mbali ili kuhakikisha Mashirika hayo yanafanya kazi kwa ufanisi mkubwa hapa nchini.
Ameyasema hayo katika hafla ya ufungaji wa wiki ya Mashirika ya Umma Zanzibar iliyofayika katika Kiwanja cha Mapinduzi Square Michenzani jijini Zanzibar.
Amesema kwa kutambua umuhimu wa Mashirika ya Umma Serikali imechukua hatua ya kuanzishwa kwa Afisi ya Msajili wa Hazina Zanzibar chini ya Sheria Namba 6 ya mwaka 2021 na kupewa jukumu la kuwa msimamizi mkuu na mmiliki pekee wa uwekezaji wa Mashirika ya Umma kwa niaba ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Makamu wa Pili wa Rais amesema kuwepo kwa Afisi ya Msajili wa Hazina Zanzibar kumechangia kuleta mabadiliko makubwa ya uendeshaji wa Mashirika ya Umma, utoaji wa huduma kwa wananchi na kuchangia kuongezeka kwa kwa mapato ya Serikali ambapo kwa mwaka 2022- 2023 Mashirika ya Umma yameweza kuchangia gawio la Shilingi za Kitanzania Bilioni 13.7.
Mhe.Hemed amesema Shirika la Bandari limeweza kuongeza ufanisi wa utoaji wa huduma kwa meli za mizigo katika bandari ya Malindi kupitia muwekezaji Afrikan Global Logistic(AGL) na kuchochea kuongezeka kwa mapato kutoka shilingi za Kitanzania Bilioni 5.5 hadi kufikia Bilioni 6 kwa mwezi kwa mwaka 2024.
Aidha, Mhe Hemed amefahamisha kuwa Shirika la Bima la Zanzibar limepata mafanikio makubwa kwa kuendelea kutoa huduma bora na za kisasa kwa wananchi kwa kupitia Mifumo ya Tehama na kuchangia kukua kwa mapato kutoka Bilioni 19 kwa mwaka 2021 na kufikia Bilioni 130.74 kwa mwaka 2024.
Sambamba na hayo amewaagiza viongozi wa Mashirika ya Umma kuendelea kuboresha Mifumo ya utendaji katika utoaji wa huduma ili kuleta ufanisi zaidi katika utekelezaji wa majukumu na kuendelea kukuza ushirikiano wa karibu kati ya viongozi na Afisi ya msajili wa Hazina kwa kutatua chamgamoto mbali mbali zinapotokezea.
Nae Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Fedha na Mipango Zanzibar Mhe Dkt. Saada Salum Mkuya amesema kumekuwa na mabadiliko makubwa ya kimaendeleo kwenye Mashirika ya Umma hasa katika kutoa huduma bora kwa wananchi ili kuhakikisha yanakamilisha malengo na mikakati ya Serikali iliyojiwekea.
Dkt. Mkuya amesema azma ya Rais Dkt. Mwinyi ni kuhakikisha kupitia Shirika la Nyumba na Mashirika mengine Zanzibar inakuwa na mji wenye majengo ya kisasa yenye kukidhi huduma zote stahiki ambayo yataufanya Mji wa Zanzibar kuwa wenye haiba na muonekano mzuri utakaoitangaza Zanzibar ndani na nje ya nchi.
Dkt. Saada amewataka wananchi kupuuza uvumi unaotolewa na wasioitakia mema Zanzibar na badala yake kuyatangaza mambo mazuri ya kimaendeleo yanayofanywa na Rais Dkt Hussein Mwinyi kwa Wazanzibari wote.
Kwa upande wake Msajili wa Hazina Zanzibar Bwana WAHIDI MOHAMMED SANYA amesema Afisi ya Msajili wa Hazina Zanzibar imefanikiwa kuyaunganisha Mashirika 18 ya Umma yaliyopo Zanzibar ambayo yanafanya kazi kwa ushirikiano mkubwa jambo ambalo linaifanya Afisi ya Msajili wa Hazina kupiga hatua kimaendeleo katika kipindi kifupi tangu kuanzishwa kwake.
Bwana. WAHIDI amesema Wiki ya Mashirika ya Umma itakuwa endelevu na itafanyika kila mwaka lengo ikiwa ni kuyaweka pamoja Mashirika na kujadili mafanikio lakini pia kutafuta njia muafaka za kupata utatuzi wa changamoto mbali mbali zinazoyakabili mashirika hayo.
Mapema Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar ametembelea mabanda ya maonesho ya Mashirika ya Umma yaliyojotokeza katika kuadhimisha Wiki ya Mashirika ya Umma Zanzibar iliyofayika katika Kiwanja cha Mapinduzi Square Michenzani jijini Zanzibar.
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
05-01-2026
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
05-01-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
05-01-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
05-01-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
05-01-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
05-01-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
05-01-2026
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
05-01-2026
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
05-01-2026
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
05-01-2026
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
05-01-2026
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
05-01-2026
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
05-01-2026
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
05-01-2026
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
05-01-2026
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
05-01-2026
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
05-01-2026
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
05-01-2026
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
05-01-2026
TAARIFA KWA UMMA
05-01-2026