Rais wa Zanzibar Dkt Hussein Ali Mwinyi amesema Serikali itaendelea kuweka mazingira rafiki na wezeshi ya kiuchumi ili kukuza Sekta ya Fedha nchini
Ameyasema hayo katika hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Hemed Suleiman Abdalla katika Uzinduzi wa ripoti ya Utafiti Finscope Tanzania 2023 kwa upande wa Zanzibar katika ukumbi wa Hotel ya Golden Tulip Uwanja wa Ndege jijini Zanzibar.
Rais Dkt Mwinyi amesema kuwa Serikali itaendelea kuweka mazingira rafiki ya kiuchumi ikiwemo kuunda Sera zinazozingatia mahitaji ya sekta, kuweka mfumo na kanuni wezeshi za udhibiti pamoja na kushirikiana kwa karibu na wadau wote wa sekta ya fedha ili kushuhulikia changamoto zinazokwamisha mafanikio kwenye utendaji.
Amesema kuwa wakati Serikali ikiendelea kuweka mikakati jumuishi pamoja na kuboresha miundombinu ya Msingi, FSDT ina wajibu wa kupanua wigo wa huduma za kifedha, kusaidia ukuwaji wa kampuni na Sekta binafsi pamoja na kuchangia ukuaji wa uchumi na maendeleo ya nchi.
Aidha Rais Dkt Mwinyi amesema Ripoti ya FinScope itasaidia katika kubuni mbinu zitakazotumika katika utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya Zanzibar (2023-2050) Mpango Mkakati wa Taifa wa huduma jumuishi za fedha (2023- 2028) na mipango mengine yakimaendeleo pamoja na kutatua changamoto zilizopo, hivyo amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imejipanga kuhakikisha kuwa maendeleo ya sekta ya fedha na hali ya huduma jumuishi za fedha nchini ziinaimarika.
Dkt. Mwinyi amesema bado kuna kazi kubwa ya kuhakikisha Wazanzibari wenye umri wa kufanya kazi, hususan wanawake, wanafanikiwa kupata kipato binafsi ili kupunguza hali tegemezi na kuongeza matumizi ya bidhaa na huduma mbalimbali za fedha ili kuboresha ustawi wa maisha yao ya kila siku pamoja na kukuza uchumi wa nchi.
Sambamba na hayo amewataka wadau wa Sekta ya fedha kuendelea kuunga mkono jitihada za Serikali za kuboresha hali ya huduma ya jumuishi za kifedha kama zilivyoainishwa katika Dira ya Maendeleo ya Zanzibar na kuwahakikishia kuwa Serikali iko tayari kushirikiana na wadau wa maendeleo nchini kwa lengo la kukabiliana na vikwazo vya maendeleo katika sekta ya fedha kwa kuzingatia Sera, kanuni na miongozo ya nchi
Nae Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, fedha na Mipango Dkt Saada Mkuya Salum amesema bado kuna matumizi finyu ya bima ya afya nchini hivyo Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeona umuhimu wa kuanzisha mfuko wa bima ya afya Zanzibar pamoja na kuyataka mabenki kutafuta utaratibu mwengine wa kufungua huduma za fedha kwa jamii ili kurahisisha upatikanajiwa kuweka fedha benki kwa urahisi na kupunguza gharama.
Dk. Mkuya amesema katika kutekeleza hilo kuna haja ya kusambaza matokeo ya utafiti huu kupitia njia sahihi ili kuhakikisha kunafanyika maamuzi na kubuni bidhaa na huduma zinazopatikana kirahisi, kwa gharama nafuu, na kuzingatia mapendekezo na matakwa ya watumiaji ili kuwafikia watu wengi zaidi.
Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi mfuko wa kuendeleza sekta ya fedha Tanzania Ndugu Erick Masinde amesema ripoti hii imekuwa na lengo la kuikuza sekta ya fedha na kuimarisha upatikanaji wa huduma za fedha ili kuwa jumuishi na endelevu na hatimae kurahisisha shughuli za kiuchumi, kuboresha maisha ya watanzania na kupunguza umasikini..
Mapema watoa mada katika uzinduzi wa riport hio wamesema kupitia ripoti hio kutazisaidia Serikali zote mbili kukuwa kiuchumi na kimaendeleo hivyo wameiomba serikali ya Zanzibar kuitumia ripoti hio kama ni kielelezo kikubwa cha kuondoa upatikanaji wa fedha kwa wananchi wake sambamba na kukuwa kwa maendeleo endelevu nchini.
Ripoti kama hii imekuwa ikitolewa kila baada ya miaka minne (4) kwa kushirikiana na wadau mbali mbali wa fedha hivyo ripoti hii inataarifa muhimu zinazohusu Zanzibar na upatikanaji wa wa fedha
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
09-12-2025
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
09-12-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
09-12-2025
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
09-12-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
09-12-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
09-12-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
09-12-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
09-12-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
09-12-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
09-12-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
09-12-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
09-12-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
09-12-2025
TAARIFA KWA UMMA
09-12-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
09-12-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
09-12-2025