RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE.DKT HUSSEN ALI MWINYI AMESEMA SERIKALI ZOTE MBILI ZITAENDELA KUWAWEKA MAZINGIRA MAZURI KWA VIJANA IKIWEMO KUWAPATIA ELIMU, MIKOPO NA FURSA MBALI MBALI MBALI ILI KUWEZA KUFIKIA MALENGO WALIOJIWEKEA.
Ameyasema hayo katika Hotuba iliyosomwa kwa niaba yake na Mjumbe wa kamati kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa ambae pia ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe Hemed Suleiman Abdulla katika uzinduzi wa Matembezi ya Umoja wa Vijana yenya Mnasaba na Sherehe za kutimia miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar Hafla iliyofanyika katika Uwanja wa Makombeni Mkoa wa Kusini Pemba.
Amesema Matembezi haya yanaendana na fikra na falsafa za waasisi wa Mapinduzi hivyo ni lazima Vijana kuyatumia matembezi haya katika kuyatangaza mambo mazuri yanayofanywa na viongozi wakuu wa nchi ambayo ni kuwaletea maendeleo wananchi wake bila ya kubagua Dini, Rangi wala Itikadi ya chama chochote.
Rais Dkt. Mwinyi amesema mapinduzi ya mwaka 1964 yaliyofanywa na viongozi waliopita yalikuwa na lengo la kuwakomboa wananchi kutoka katika mikono ya wakoloni hivyo ni lazima vijana kwa kushirikiana na viongozi wa serikali zote mbili kuyaenzi kwa vitendo katika kuwaletea maendeleo wananchi wake na kuwaondolea changamoto zote zinazowakabili.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Braza la Mapinduzi Mhe.Dkt Hussein Ali Mwinyi amesema kuwa wajibu wa Vijana ni kulisaidia Taifa katika kupiga vita Rushwa, ubadhirifu wa mali za Umma, Udhalilishaji na Madawa ya kulevya kwa kuwapa Elimu vijana wenzao ili Taifa liweze kusonga mbele pamoja na kuweza kutoa ushirikiano kwa vyombo husika ili kuweza kuchukuliwa hatua za kisheria wwale wote wanaoenda kinyume na sheria .
Sambamba na hayo amewataka Viongozi wa matembezi hayo na Vijana kwa ujumla kusimamia nidhamu ili kufikia lengo la kuwepo kwa jumuiya hio kwani Jumuiya ya Vijana ndio Tegemeo kubwa la Chama na Taifa kwa Ujumla katika kupata viongozi bora wa sasa na baadae.
Akizungumzia Uandikishaji wa daftari la kudumu la Wapiga Kura Rais Dkt. Mwinyi amewataka vijana wenye sifa kujitokeza kujiandikisha ili wapate nafasi ya kukichagua Chama Cha Mapinduzi kwa kura nyingi katika Uchaguzi Mkuu ujao wa mwaka 2020-2025.
Nae Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM Taifa Ndugu Mohamed Ali Mohamed (KAWAIDA ) amesema ndani ya Miaka 60 ya Mapinduzi, Zanzibar imepiga hatua kubwa ya maendeleo ambapo Serikali ya Awamu ya nane(8) na serikali ya awamu ya Sita (6) zinaendelea kuwawekea mazingira mazuri ya kimaendeleo kwa kujenga miradi mbali mbali pamoja na kuwaodolea changamoto zote wananchi wake.
Ndugu Mohammed Kawaida amefahamisha kuwa matembezi ya vijana yana azma ya kuyalinda na kuyaenzi Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ambapo kupitia matembezi hayo vijana watafanya kazi ya kuyatangaza yale mambo makubwa na mazuri yaliyofanywa na Viongozi wakuu wa Nchi yenye tija na wananchi wa Tifa hili.
Amesema kuwa dhamira ya Mapinduzi ni kuwaletea wananchi maendeleo na kuwapa nafasi Vijana kuweza kujitawala wenyewe hivyo Jumuia ya Umoja wa Vijana itaendelea kukitumikia chama cha Mapinduzi na kuwalinda viongozi wakuu wa nchi kwa kuhakikisha wanawaweka tena madarakani ifikapo mwaka 2025.
Akizungmza kwa niaba ya Naibu Katibu Mkuu CCM Zanzibar, Katibu wa CCM Idara ya Itikadi na Uwenezi na Mafunzo ya CCM Zanzibar Comred Khamis Mbeto amesema kuwa wajibu wa Vijana ni kuyalinda Mapinduzi kwa kuzienzi na kuzidumisha falsafa na fikra za waasisi wa mapinduzi ambao walijotoa kwa ajili ya wazanzibari.
Amesema kuwa Vijana ndio hazina ya Chama cha Mapinduzi ambao wana mchango mkubwa katika kuhakikisha wanapambania maendeleo ya Nchi na kutokuwapa nafasi ya kuwapotosha Vijana wale wote ambao hawana dhamira njema na CCM na Serikali kwa ujumla.
Maapema mkuu wa mkoa wa Kusini Pemba Mhe. Matar Zahor Maoud amesema kuwa kupitia mapinduzi matukufu ya Mwaka 1964 Zanzibar tumepata maendeleo makubwa ambayo yanaletwa na viongozi wakuu waliopo sasa na waliopita hivyo ni wajibu wa kila mmoja kuyapigania na kuyaenzi maendeleo hayo kwa faida ya vizazi vya sasa na baadae.
Amesema Zanzibar inaendelea kunufaika na matunda ya Mapinduzi kwa kupitia viongozi wakuu wa nchi hivyo amewashukuru viongozi wakuu wa nchi kwa kuwaletea miradi mingi ya kimaendeleo ikiwemo maji safi na salama, Afya, ujenzi wa Skuli za ghorofa pamoja na kutatua changamoto zote zinazowakabili wananchi wa mkoa wa kusini pemba na mikoa mengine.
KIPINDI MAALUMU
08-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐒𝐈𝐌𝐀𝐌𝐈𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐒𝐀𝐅𝐀𝐑𝐀 𝐊𝐔𝐒𝐀𝐋𝐈𝐌𝐈𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐍𝐀 𝐊𝐈𝐉𝐈𝐖𝐄 𝐂𝐇𝐀 𝐂𝐇𝐀𝐃𝐄𝐌𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈
08-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐊𝐈𝐓𝐔𝐎 𝐂𝐇𝐀 𝐀𝐅𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐋𝐎𝐋𝐄𝐍𝐈, 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈
08-06-2026
𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐘𝐀𝐀𝐌𝐁𝐈𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐂𝐇𝐀𝐆𝐔𝐀 𝐌𝐀𝐄𝐍𝐃𝐄𝐋𝐄𝐎 𝐁𝐀𝐃𝐀𝐋𝐀 𝐘𝐀 𝐌𝐀𝐀𝐍𝐃𝐀𝐌𝐀𝐍𝐎
08-06-2026
𝐌𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐙𝐈 𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐓𝐈𝐁𝐔 𝐖𝐀 𝐍𝐄𝐂, 𝐈𝐓𝐈𝐊𝐀𝐃𝐈, 𝐔𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐍𝐀 𝐌𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐎 𝐂𝐂𝐌, 𝐍𝐃𝐔𝐆𝐔 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐋𝐀𝐁𝐀𝐍 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈, 𝐎𝐅𝐈𝐒𝐈 𝐙𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈
08-06-2026
𝐒𝐀𝐒𝐀 𝐍𝐈 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈, 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐃𝐎 𝐌𝐃𝐔𝐍𝐃𝐎!
08-06-2026
𝐀𝐑𝐔𝐌𝐄𝐑𝐔 𝐘𝐀𝐒𝐈𝐊𝐈𝐀 𝐖𝐈𝐓𝐎 𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐋𝐈𝐍𝐃𝐀 𝐌𝐀𝐀𝐃𝐈𝐋𝐈 𝐍𝐀 𝐇𝐀𝐊𝐈 𝐙𝐀 𝐖𝐀𝐓𝐎𝐓𝐎
08-06-2026
𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐒𝐀𝐌𝐁𝐀𝐙𝐀 𝐔𝐏𝐄𝐍𝐃𝐎 𝐖𝐀 𝐀𝐆𝐀𝐏𝐄 𝐊𝐖𝐄𝐍𝐘𝐄 𝐊𝐈𝐉𝐈𝐖𝐄 𝐂𝐇𝐀 𝐂𝐇𝐀𝐃𝐄𝐌𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐌𝐄𝐑𝐔
08-06-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐀𝐍𝐙𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐌𝐄𝐑𝐔 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐊𝐀𝐆𝐔𝐀 𝐔𝐇𝐀𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐇𝐀𝐌𝐀
08-06-2026
𝐌𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐎 𝐖𝐀 𝐇𝐀𝐃𝐇𝐀𝐑𝐀 𝐖𝐀 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐑𝐀𝐓𝐔 - 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀
08-06-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐓𝐔𝐍𝐔𝐊𝐈𝐖𝐀 𝐒𝐇𝐀𝐇𝐀𝐃𝐀 𝐘𝐀 𝐇𝐄𝐒𝐇𝐈𝐌𝐀 𝐔𝐑𝐔𝐒𝐈
08-06-2026
𝐀𝐑𝐔𝐌𝐄𝐑𝐔, 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐀𝐍𝐀𝐊𝐔𝐉𝐀!
08-06-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐑𝐀𝐒𝐌𝐈 𝐔𝐑𝐔𝐒𝐈, 𝐀𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐀 𝐍𝐀 𝐏𝐔𝐓𝐈𝐍
08-06-2026
𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎, 𝐓𝐔𝐍𝐀𝐊𝐔𝐉𝐀
08-06-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐃𝐊𝐓. 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐌𝐎𝐒𝐂𝐎𝐖, 𝐔𝐑𝐔𝐒𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀
08-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐒𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐈𝐑𝐎 𝐊𝐖𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐊𝐀𝐙𝐈
08-06-2026
𝐅𝐔𝐍𝐆𝐀 𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐍𝐘𝐀𝐑𝐀 𝐋𝐄𝐎!!!
08-06-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐒𝐇𝐈𝐍𝐀 𝐍𝐀. 𝟐 𝐊𝐀𝐓𝐀 𝐘𝐀 𝐁𝐎𝐍𝐆𝐀
08-06-2026
𝐁𝐀𝐁𝐀𝐓𝐈 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈 𝐋𝐄𝐎 𝐓𝐔𝐍𝐀𝐈𝐅𝐔𝐍𝐈𝐊𝐀!!!
08-06-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐀 𝐍𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐇𝐀𝐍𝐀𝐍𝐆, 𝐀𝐒𝐈𝐊𝐈𝐋𝐈𝐙𝐀 𝐍𝐀 𝐊𝐔𝐓𝐀𝐓𝐔𝐀 𝐊𝐄𝐑𝐎 𝐙𝐀𝐎
08-06-2026