Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, ametoa uchambuzi wa kina kuhusu ushindi mkubwa wa chama hicho katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika Septemba 27, mwaka 2024
Dkt. Dimwa ameleza sababu, dhamira na mafanikio yaliyofikiwa na CCM, na pia kuonyesha jinsi ushindi huo unavyotoa picha ya nguvu ya chama na uwajibikaji wenye tija na dhamira ya dhati ya CCM ya kuwatumikia wananchi wote bila ubaguzi kwa muktadha wa siasa za ushindani chini ya mfumo wa vyama vingi.
Hayo ameyasema katika mahojiano maalum ya kutoa tathmini yake ya mafanikio na uimara wa CCM katika medani za kisiasa nchini.
Sababu za Ushindi wa Kishindo
Dkt. Dimwa amebainisha kuwa ushindi wa asilimia 99 wa CCM katika uchaguzi wa serikali za mitaa ni matokeo ya utendaji bora wa serikali ya Chama Cha Mapinduzi chini ya uongozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Rais Samia Suluhu Hassan pamoja na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Mwinyi .
Ameeleza kuwa CCM imeshinda kwa kiwango hicho kutokana na utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayogusa maisha ya wananchi wote mijini na vijijini, kuimarisha huduma za kijamii, na kutoa fursa za ajira kwa vijana wa rika tofauti na makundi mbalimbali ya wanawake.
"Ushindi huu ni matokeo ya uongozi thabiti na wa kujitolea wa viongozi wetu. Wananchi wameshuhudia mabadiliko ya kweli katika maisha yao. Ujenzi wa miundombinu, huduma za afya, elimu na kilimo ni baadhi ya sekta zinazoimarisha maisha ya watu wote bila ubaguzi wa kisiasa,kidini na kikabila. Hii inadhihirisha kuwa CCM ni chama kinachotekeleza ahadi zake na ni chama cha maendeleo," alisema Dkt. Dimwa.
Demokrasia na Mfumo wa Vyama Vingi
Katika mchango wake, Dkt. Dimwa alieleza kuwa ushindi wa CCM katika uchaguzi wa serikali za mitaa ni dhihirisho la nguvu ya demokrasia katika mfumo wa vyama vingi.
Alisisitiza kuwa siasa za ushindani ni muhimu katika kuleta maendeleo na kwamba CCM inaheshimu na kutambua mchango wa vyama vingine, ingawa CCM inabaki kuwa chama chenye uwezo mkubwa wa kuleta mabadiliko ya kivitendo kwa wananchi.
"Katika mfumo wa vyama vingi, ushindani ni muhimu, lakini ushindi wa CCM katika uchaguzi huu ni uthibitisho wa kwamba wananchi wanatambua juhudi za serikali yetu.
Demokrasia siyo tu kushiriki katika uchaguzi, bali ni kuhakikisha kuwa kila mwananchi anafaidika na matunda ya demokrasia hiyo," alisema Dkt. Dimwa.
Mafanikio ya Falsafa ya Rais Samia Suluhu Hassan ya 4R
Dkt. Dimwa pia alifafanua mafanikio yaliyofikiwa katika kutafsiri kwa vitendo falsafa ya Rais Samia Suluhu Hassan ya 4R imeleta matokeo chanya ya upatikanaji wa ushindi huo na kwamba mafanikio haya ni dhihirisho la jinsi serikali ya CCM inavyotoa huduma bora kwa wananchi, huku ikirudisha imani ya wananchi kwa serikali na kuimarisha umoja wa kitaifa.
" Tumeshuhudia maendeleo katika maeneo mengi, ikiwemo ujenzi wa miundombinu, upatikanaji wa huduma za afya na elimu, na uimarishaji wa uchumi wa Zanzibar. Kwa hiyo, ushindi huu unaonyesha kuwa falsafa ya Rais Samia ya 4R inatekelezwa kwa vitendo na inagusa maisha ya wananchi," alisema Dkt. Dimwa.
Ushindi wa Serikali za Mitaa kama Tathmini ya Uchaguzi Mkuu wa 2025
Dkt. Dimwa alisisitiza kuwa ushindi wa CCM katika uchaguzi wa serikali za mitaa ni tathmini halisi ya matokeo yanayoweza kutarajiwa katika uchaguzi mkuu wa dola wa mwaka 2025.
Alieleza kuwa ushindi wa kishindo katika uchaguzi huo pia unatoa picha ya kuwa CCM ni Chama kiongozi katika siasa za Tanzania na kwamba wananchi wenyewe kwa ridhaa yao wameamua kukiunga mkono kukipigia kura nyingi za ndio kupitia mfumo huru wa kidemokrasia.
"Ushindi wa serikali za mitaa ni kielelezo cha mapenzi ya wananchi kwa CCM na dhamira ya chama chetu ni kuhakikisha kuwa kila mtaa, kila kijiji, kila wilaya na kila kisiwa kinapata maendeleo.
Huu ni ushindi wa wananchi na ni uthibitisho wa kwamba uchaguzi mkuu wa 2025 utakuwa na mafanikio makubwa kwa CCM," alisema Dkt. Dimwa.
Wito kwa Wananchi na Wanachama wa CCM
Dkt. Dimwa alitoa wito kwa wananchi wote, hasa wanachama wa CCM, kujitokeza kwa wingi kushiriki zoezi la awamu ya pili ya uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura litakalofanyika hivi karibuni.
Aliwakumbusha wananchi kuwa zoezi hili ni haki yao ya kikatiba na ni muhimu kwa kuimarisha demokrasia na uhuru wa kucgagua na kuchaguliwa nchini.
"Ni muhimu kwa kila mwananchi kuhakikisha kwamba jina lake linajumuishwa katika daftari la wapiga kura.
Hii ni haki ya kikatiba ya kila Mtanzania.Tunatoa wito kwa wanachama wa CCM na wananchi kwa ujumla kujitokeza kwa wingi katika zoezi hili muhimu, ili kuimarisha ushiriki wetu katika uchaguzi mkuu wa 2025," alisisitiza Dkt. Dimwa
Pamoja na hayo Dkt.Dimwa, anaeleza kuwa CCM inaendelea kujizatiti na kuboresha huduma kwa wananchi, huku ikisisitiza kuwa uchaguzi wa 2025 utakuwa ni uthibitisho wa mafanikio ya chama na serikali katika kuleta maendeleo ya kweli kwa kila Mtanzania.
𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈 𝐘𝐀𝐌𝐏𝐀 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐌𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐙𝐈 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐇𝐈𝐒𝐓𝐎𝐑𝐈𝐀
22-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐙𝐈𝐍𝐃𝐔𝐀 𝐒𝐇𝐈𝐍𝐀 𝐋𝐀 𝐖𝐀𝐊𝐄𝐑𝐄𝐊𝐄𝐓𝐖𝐀 𝐌𝐋𝐀𝐍𝐃𝐄𝐆𝐄, 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐒𝐀-𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀
22-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐒𝐇𝐈𝐍𝐀 𝐍𝐀. 𝟏𝟎 𝐌𝐀𝐅𝐈𝐅𝐈, 𝐀𝐒𝐈𝐒𝐈𝐓𝐈𝐙𝐀 𝐀𝐌𝐀𝐍𝐈, 𝐔𝐌𝐎𝐉𝐀 𝐍𝐀 𝐌𝐒𝐇𝐈𝐊𝐀𝐌𝐀𝐍𝐎
22-06-2026
𝐌𝐑𝐀𝐃𝐈 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐎 𝐘𝐀 𝐔𝐅𝐔𝐍𝐃𝐈 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎 𝐊𝐔𝐅𝐔𝐍𝐆𝐔𝐀 𝐅𝐔𝐑𝐒𝐀 𝐙𝐀 𝐀𝐉𝐈𝐑𝐀 𝐊𝐖𝐀 𝐕𝐈𝐉𝐀𝐍𝐀
22-06-2026
𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎, 𝐙𝐀𝐌𝐔 𝐘𝐄𝐍𝐔 𝐍𝐈 𝐋𝐄𝐎!
22-06-2026
𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀: 𝐃𝐊𝐓. 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐒𝐔𝐋𝐔𝐇𝐔 𝐇𝐀𝐒𝐒𝐀𝐍 𝐍𝐈 𝐌𝐓𝐄𝐊𝐄𝐋𝐄𝐙𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐀𝐇𝐈𝐑𝐈 𝐖𝐀 𝐀𝐇𝐀𝐃𝐈 𝐙𝐀 𝐂𝐂𝐌
22-06-2026
𝐒𝐈𝐌𝐔 𝐈𝐌𝐄𝐈𝐓𝐀, 𝐍𝐄𝐄𝐌𝐀 𝐘𝐀 𝐔𝐓𝐀𝐓𝐔𝐙𝐈 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎!
22-06-2026
𝐑𝐔𝐀𝐇𝐀 𝐌𝐁𝐔𝐘𝐔𝐍𝐈 𝐘𝐀𝐅𝐔𝐑𝐈𝐊𝐀; “𝐂𝐇𝐈𝐄𝐅 𝐂𝐇𝐎𝐆𝐀𝐕𝐀𝐓𝐀𝐌𝐁𝐔𝐋𝐄” 𝐀𝐊𝐈𝐓𝐄𝐊𝐀 𝐌𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐎 𝐖𝐀 𝐇𝐀𝐃𝐇𝐀𝐑𝐀!
22-06-2026
𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐎 𝐂𝐇𝐀 𝐔𝐌𝐖𝐀𝐆𝐈𝐋𝐈𝐀𝐉𝐈 𝐍𝐈 𝐔𝐅𝐔𝐍𝐆𝐔𝐎 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐏𝐈𝐍𝐃𝐔𝐙𝐈 𝐘𝐀 𝐔𝐂𝐇𝐔𝐌𝐈 𝐖𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈: 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈
22-06-2026
𝐂𝐂𝐌 𝐘𝐀𝐔𝐍𝐆𝐀 𝐌𝐊𝐎𝐍𝐎 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐖𝐀 𝐍𝐉𝐎𝐌𝐁𝐄 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐙𝐀 𝐔𝐙𝐀𝐋𝐈𝐒𝐇𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐀𝐋𝐈
22-06-2026
𝐀𝐌𝐀𝐍𝐈 𝐍𝐈 𝐌𝐒𝐈𝐍𝐆𝐈 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐄𝐍𝐃𝐄𝐋𝐄𝐎: 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈
22-06-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐑𝐀𝐒𝐌𝐈 𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀!!
22-06-2026
𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀 𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐋𝐄𝐖𝐀 𝐍𝐉𝐎𝐌𝐁𝐄, 𝐀𝐇𝐈𝐌𝐈𝐙𝐀 𝐕𝐈𝐎𝐍𝐆𝐎𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐊𝐔𝐈𝐒𝐇𝐈 𝐃𝐇𝐀𝐍𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐍𝐀 𝐔𝐓𝐔 𝐊𝐖𝐀 𝐕𝐈𝐓𝐄𝐍𝐃𝐎
22-06-2026
𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀: 𝐂𝐂𝐌 𝐇𝐀𝐈𝐓𝐀𝐕𝐔𝐌𝐈𝐋𝐈𝐀 𝐔𝐙𝐄𝐌𝐁𝐄, 𝐕𝐈𝐎𝐍𝐆𝐎𝐙𝐈 𝐖𝐀𝐖𝐀𝐉𝐈𝐁𝐈𝐊𝐄 𝐊𝐔𝐓𝐀𝐓𝐔𝐀 𝐂𝐇𝐀𝐍𝐆𝐀𝐌𝐎𝐓𝐎 𝐙𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈
22-06-2026
𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀 𝐓𝐔𝐍𝐀𝐊𝐔𝐉𝐀𝐀𝐀, 𝐓𝐔𝐍𝐀𝐀𝐍𝐙𝐈𝐀 𝐑𝐔𝐀𝐇𝐀 𝐌𝐁𝐔𝐘𝐔𝐍𝐈!
22-06-2026
𝐌𝐈𝐊𝐎𝐏𝐎 𝐘𝐀 𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈𝐌𝐈𝐀 𝟏𝟎% 𝐘𝐀𝐂𝐇𝐎𝐂𝐇𝐄𝐀 𝐔𝐂𝐇𝐔𝐌𝐈 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐊𝐔𝐍𝐃𝐈 𝐌𝐀𝐀𝐋𝐔𝐌
22-06-2026
𝐍𝐃𝐆 𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀 𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐋𝐄𝐖𝐀 𝐑𝐔𝐕𝐔𝐌𝐀, 𝐀𝐇𝐈𝐌𝐈𝐙𝐀 𝐔𝐌𝐎𝐉𝐀 𝐍𝐀 𝐌𝐒𝐇𝐈𝐊𝐀𝐌𝐀𝐍𝐎 𝐍𝐃𝐈𝐎 𝐍𝐆𝐔𝐕𝐔 𝐘𝐀 𝐂𝐂𝐌
22-06-2026
𝐊𝐇𝐄𝐑𝐈 𝐘𝐀 𝐒𝐈𝐊𝐔 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐌𝐀𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐘𝐀 𝐌𝐓𝐎𝐓𝐎 𝐖𝐀 𝐀𝐅𝐑𝐈𝐊𝐀
22-06-2026
𝐌𝐇𝐄. 𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐀𝐍𝐀𝐖𝐀𝐏𝐄𝐍𝐃𝐀 𝐒𝐀𝐍𝐀 𝐖𝐀𝐓𝐀𝐍𝐙𝐀𝐍𝐈𝐀, 𝐖𝐀𝐓𝐔𝐌𝐈𝐒𝐇𝐈 𝐖𝐀 𝐔𝐌𝐌𝐀 𝐓𝐈𝐌𝐈𝐙𝐄𝐍𝐈 𝐖𝐀𝐉𝐈𝐁𝐔 𝐖𝐄𝐍𝐔 𝐊𝐈𝐊𝐀𝐌𝐈𝐋𝐈𝐅𝐔: 𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀
22-06-2026
𝐂𝐂𝐌 𝐇𝐀𝐈𝐓𝐎𝐑𝐔𝐃𝐈 𝐍𝐘𝐔𝐌𝐀 𝐊𝐔𝐋𝐈𝐍𝐃𝐀 𝐌𝐀𝐒𝐋𝐀𝐇𝐈 𝐘𝐀 𝐌𝐊𝐔𝐋𝐈𝐌𝐀 𝐖𝐀 𝐊𝐎𝐑𝐎𝐒𝐇𝐎: 𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀
22-06-2026