Makao Makuu - Dodoma
#CCM Imetimia KaziIendelee

Habari na Matukio Mbalimbali


๐—–๐—–๐—  ๐—ฌ๐—”๐—ฆ๐—œ๐—ฆ๐—œ๐—ง๐—œ๐—ญ๐—” ๐—ช๐—”๐—š๐—ข๐— ๐—•๐—˜๐—” ๐—ž๐—จ๐—๐—”๐——๐—œ๐—Ÿ๐—œ๐—ช๐—” ๐—ž๐—ช๐—” ๐—ž๐—จ๐—ญ๐—œ๐—ก๐—š๐—”๐—ง๐—œ๐—” ๐—จ๐—ช๐—˜๐—ญ๐—ข, ๐—จ๐—ญ๐—”๐—Ÿ๐—˜๐—ก๐——๐—ข ๐—ก๐—” ๐—จ๐—”๐——๐—œ๐—Ÿ๐—œ๐—™๐—จ, ๐—ฌ๐—”๐—ž๐—˜๐— ๐—˜๐—” ๐— ๐—”๐—ž๐—จ๐—ก๐——๐—œ - ๐—–๐——๐—˜. ๐—š๐—”๐—ฉ๐—จ

alternative

๐™‘๐™ž๐™ ๐™–๐™ค ๐™๐™–๐™ซ๐™ž๐™ง๐™ช๐™๐™ช๐™จ๐™ž๐™ฌ๐™ž ๐™ ๐™ช๐™ฌ๐™š๐™ ๐™– ๐™ข๐™จ๐™ž๐™ข๐™–๐™ข๐™ค ๐™ ๐™ฌ๐™– ๐™ฃ๐™–๐™›๐™–๐™จ๐™ž ๐™ฎ๐™ค๐™ฎ๐™ค๐™ฉ๐™š ๐™ž๐™ฃ๐™–๐™ฎ๐™ค๐™œ๐™ค๐™ข๐™—๐™š๐™ฌ๐™–

Katibu wa NEC - Oganaizesheni wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa Ndugu. ๐—œ๐˜€๐˜€๐—ฎ ๐—›๐—ฎ๐—ท๐—ถ ๐—จ๐˜€๐˜€๐—ถ ๐—š๐—ฎ๐˜ƒ๐˜‚ leo tarehe 21 Juni 2025 amefungua ๐— ๐—ฎ๐—ณ๐˜‚๐—ป๐˜‡๐—ผ ๐— ๐—ฎ๐—ฎ๐—น๐˜‚๐—บ ๐˜†๐—ฎ ๐—ช๐—ฎ๐—ท๐˜‚๐—บ๐—ฏ๐—ฒ ๐˜„๐—ฎ ๐—›๐—ฎ๐—น๐—บ๐—ฎ๐˜€๐—ต๐—ฎ๐˜‚๐—ฟ๐—ถ ๐—ž๐˜‚๐˜‚ ๐˜‡๐—ฎ ๐—–๐—–๐—  ๐˜‡๐—ฎ ๐—ช๐—ถ๐—น๐—ฎ๐˜†๐—ฎ ๐˜‡๐—ฎ ๐— ๐—ธ๐—ผ๐—ฎ ๐˜„๐—ฎ ๐—œ๐—ฟ๐—ถ๐—ป๐—ด๐—ฎ yenye lengo ya kuendelea kujenga chama katika misingi imara na thabiti yaliyofanyika katika ukumbi wa Chuo Cha UVCCM Ihemi Mkoani Iringa.

Akiziungumza na Wajumbe hao, Ndg. Gavu amewataka viongozi ngazi ya Mkoa, WIlaya na Kata kuwa wakati utakapofika wa kujadili majina ya wagombea , wajadili kwa kuzingatia uwezo, sifa nzuri, uzalendo na uadilifu na si kwa kuweka mbele ukabila, urafiki wala undugu kwakuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) akihusudu kwenye hayo.

Ndg. Gavu amesema iwapo mgombea ana sifa za kugombea na anakubalika kwa jamii basi apewe kipaumbele bila kujali ni adui kwa baadhi ya wajumbe, kikao kinatakiwa kimpendekeze kwakuwa huyo atafaa kuwa mgombea kwa maslahi ya Chama Cha Mapinduzi na Taifa kwa ujumla, lakini iwapo mgombea hana sifa na hakubaliki kwenye jamii basi hata kama ni rafiki wa wajumbe hatakiwi kupendekezwa na kikao husika.

Akitoa msisitizo zaidi kuhusiana na wagombea wenye kuhitajika, Ndg. Gavu amesema CCM inataka vikao vyake kwa ngazi zote vitoe mustakabali mzima Maendeleo kwa Watanzania kwa ujumla kwa kuwapata wagombea walio tayari wakati wowote kujikosoa, kukosolewa na kukosoana.

Aidha, Ndg. Gavu ametoa onyo kali kwa kikao chochote kile kuweka au kutangaza msimamo kwa nafasi yoyote inayogombewa iwe Ubunge ama Udiwani na badala yake misingi ya Haki, Usawa na Uwazi izingatiwe.

Vilevile, Ndg. Gavu amesema vikao vitatakiwa kuzingatia aliyeongoza kwa kura za maoni isipokuwa kama iwapo itabainika wazi kuwa kura hizo alizipata kwa njia ya rushwa basi katika mchujo kikao hakitamteua kugombea nafasi aliyoiomba na lazima aelezwe wazi tuhuma zake.

Akihitimisha katika hotuba yake, Ndg. Gavu amesema vikao vyote vya uchujaji na uteuzi vizingatie mujibu wa Katiba na Kanuni za CCM, ambapo amesema CCM inaendelea kuwasihi wajumbe kuzingatia miiko na misingi ya CCM ili kutimiza lengo la Ibara ya 5 la kushinda katika chaguzi zote.

#OktobaTunatikiโœ…
#KaziNaUtuTunasongaMbele

alternative alternative alternative
Habari Nyingine