๐๐๐ ๐ฌ๐๐ฆ๐๐ฆ๐๐ง๐๐ญ๐ ๐ช๐๐๐ข๐ ๐๐๐ ๐๐จ๐๐๐๐๐๐๐ช๐ ๐๐ช๐ ๐๐จ๐ญ๐๐ก๐๐๐ง๐๐ ๐จ๐ช๐๐ญ๐ข, ๐จ๐ญ๐๐๐๐ก๐๐ข ๐ก๐ ๐จ๐๐๐๐๐๐๐จ, ๐ฌ๐๐๐๐ ๐๐ ๐ ๐๐๐จ๐ก๐๐ - ๐๐๐. ๐๐๐ฉ๐จ
๐๐๐ ๐๐ค ๐๐๐ซ๐๐ง๐ช๐๐ช๐จ๐๐ฌ๐ ๐ ๐ช๐ฌ๐๐ ๐ ๐ข๐จ๐๐ข๐๐ข๐ค ๐ ๐ฌ๐ ๐ฃ๐๐๐๐จ๐ ๐ฎ๐ค๐ฎ๐ค๐ฉ๐ ๐๐ฃ๐๐ฎ๐ค๐๐ค๐ข๐๐๐ฌ๐
Katibu wa NEC - Oganaizesheni wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa Ndugu. ๐๐๐๐ฎ ๐๐ฎ๐ท๐ถ ๐จ๐๐๐ถ ๐๐ฎ๐๐ leo tarehe 21 Juni 2025 amefungua ๐ ๐ฎ๐ณ๐๐ป๐๐ผ ๐ ๐ฎ๐ฎ๐น๐๐บ ๐๐ฎ ๐ช๐ฎ๐ท๐๐บ๐ฏ๐ฒ ๐๐ฎ ๐๐ฎ๐น๐บ๐ฎ๐๐ต๐ฎ๐๐ฟ๐ถ ๐๐๐ ๐๐ฎ ๐๐๐ ๐๐ฎ ๐ช๐ถ๐น๐ฎ๐๐ฎ ๐๐ฎ ๐ ๐ธ๐ผ๐ฎ ๐๐ฎ ๐๐ฟ๐ถ๐ป๐ด๐ฎ yenye lengo ya kuendelea kujenga chama katika misingi imara na thabiti yaliyofanyika katika ukumbi wa Chuo Cha UVCCM Ihemi Mkoani Iringa.
Akiziungumza na Wajumbe hao, Ndg. Gavu amewataka viongozi ngazi ya Mkoa, WIlaya na Kata kuwa wakati utakapofika wa kujadili majina ya wagombea , wajadili kwa kuzingatia uwezo, sifa nzuri, uzalendo na uadilifu na si kwa kuweka mbele ukabila, urafiki wala undugu kwakuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) akihusudu kwenye hayo.
Ndg. Gavu amesema iwapo mgombea ana sifa za kugombea na anakubalika kwa jamii basi apewe kipaumbele bila kujali ni adui kwa baadhi ya wajumbe, kikao kinatakiwa kimpendekeze kwakuwa huyo atafaa kuwa mgombea kwa maslahi ya Chama Cha Mapinduzi na Taifa kwa ujumla, lakini iwapo mgombea hana sifa na hakubaliki kwenye jamii basi hata kama ni rafiki wa wajumbe hatakiwi kupendekezwa na kikao husika.
Akitoa msisitizo zaidi kuhusiana na wagombea wenye kuhitajika, Ndg. Gavu amesema CCM inataka vikao vyake kwa ngazi zote vitoe mustakabali mzima Maendeleo kwa Watanzania kwa ujumla kwa kuwapata wagombea walio tayari wakati wowote kujikosoa, kukosolewa na kukosoana.
Aidha, Ndg. Gavu ametoa onyo kali kwa kikao chochote kile kuweka au kutangaza msimamo kwa nafasi yoyote inayogombewa iwe Ubunge ama Udiwani na badala yake misingi ya Haki, Usawa na Uwazi izingatiwe.
Vilevile, Ndg. Gavu amesema vikao vitatakiwa kuzingatia aliyeongoza kwa kura za maoni isipokuwa kama iwapo itabainika wazi kuwa kura hizo alizipata kwa njia ya rushwa basi katika mchujo kikao hakitamteua kugombea nafasi aliyoiomba na lazima aelezwe wazi tuhuma zake.
Akihitimisha katika hotuba yake, Ndg. Gavu amesema vikao vyote vya uchujaji na uteuzi vizingatie mujibu wa Katiba na Kanuni za CCM, ambapo amesema CCM inaendelea kuwasihi wajumbe kuzingatia miiko na misingi ya CCM ili kutimiza lengo la Ibara ya 5 la kushinda katika chaguzi zote.
#OktobaTunatikiโ
#KaziNaUtuTunasongaMbele