TUTUNZE AMANI-MJEMA
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Ndg. Sophia Mjema, amewasihi Watanzania kutunza amani ya nchi.
Ameyasema hayo leo tarehe 17 Oktoba, 2023 alipokuwa akihutubia mkutano wa hadhara katika kata Sudi, Lindi Vijijini.
"Amani ya nchi tuitunze ndugu zangu, kuna nchi nyingine mtoto anazaliwa hadi anazeeka ni milio ya mitutu tu, maendeleo yanapatikana katika amani," amesema Ndg. Mjema.
Ndg. Mjema ambaye alikuwa mkoani Lindi kuendesha mafunzo ya falsafa, itikadi na sera za CCM kwa viongozi na watendaji wa CCM, amesema demokrasia itumike kuimarisha amani.
Amesema fursa ya demokrasia nchini inatokana na uongozi makini wa CCM, na kimekuwa kikiitekeleza ndani ya chama kwa vitendo.
Amewataka wananchi kuchuja maneno wanayoambiwa au kuyasikia kutoka katika majukwaa ya siasa.
Amesema wako wanasiasa wanasema uongo na kuwataka wananchi waachane nao.
Amesema wananchi NI mashahidi kwamba chini ya uongozi mahiri wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, nchi inasonga mbele katika maendeleo.
Amesema katika kipindi kifupi, tangu amekuwa Rais, maendeleo makubwa katika kila sekta yamepatikana.
"Vituo vya afya, shule, maji, barabara, umeme, taja chochote, hakuna kilichosimama, mabilioni ya fedha yanashuka hadi vitongojini," amesema.
Ndg. Mjema amesema katika uchaguzi mkuu wa 2020, CCM iliahidi maendeleo kwa Watanzania na sasa inatekeleza.
"Usidanganywe na mtu, CCM imeahidi imetekeleza na kazi inaendelea," amesema na kuongeza kwamba "mtu ukimpa nafasi akakudanganya, maana yake anakudharau."
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
09-12-2025
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
09-12-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
09-12-2025
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
09-12-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
09-12-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
09-12-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
09-12-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
09-12-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
09-12-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
09-12-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
09-12-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
09-12-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
09-12-2025
TAARIFA KWA UMMA
09-12-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
09-12-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
09-12-2025