UFUNGUZI WA KIKAO CHA HALMASHAURI KUU YA CCM JIMBO LA MALINDI - ZANZIBAR
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar Dk. Mohammed Said Mohammed 'Dimwa' amesema ni lazima kwa kiongozi wa CCM kuwa na msimamo sahihi wa itikadi katika maisha ya kila siku na kwamba jambo hilo lina umuhimu mkubwa kwa chama hicho.
Dk. Dimwa aliyasema hayo wakati akifungua kikao cha Halmashauri kuu ya CCM ya Jimbo la Malindi huko katika Ofisi kuu ya CCM Zanzibar Kisiwandui Mjini Unguja.
Alisema, "ikiwa viongozi hawana itikadi watakuwa si viongozi thabiti kwani Chama Cha Mapinduzi hakiongozwi kwa mabavu bali kwa kuelimisha, kueleza, kushauri, kushawishi na kushirikisha".
Alisema, hiyo ni maana ya kwamba kiongozi wa Chama hana budi kuwa na uwezo wa kushauri, kuelimisha, kushawishi na kushirikisha.
"Huyo ndiyo atakuwa ni kiongozi wetu, na mimi huwa nashangaa sana kwamba anaweza kukaa mtu Mbunge, Mwakilishi au Diwani anakaa miaka mitano lakini hajatuletea hata mwanachama mmoja, hiyo manaake hana uwezo wa kushawishi," alisema.
Alieleza kuwa, Chama Cha Mapinduzi sasa hivi kimegeuaka na kimetoka kwenye analogi na kwamba sasa wameingia kwenye digitali na kwamba hata na uongozi wao wa chini ni lazima aunze kubadilika.
Aidha aliwakumbusha wanachama wa CCM juu ya swala zima la umoja na mshikamano na kwamba hiyo ndiyo silaha kubwa ya Chama hicho.
Pia Dimwa aliwakumbusha viongozi na wanachama wa CCM kutizama mustakabali mzima wa Chama Cha Mapunduzi wapi unapokwenda na kuacha tabia ya kuchukiana bila ya sababu za msingi.
Hivyo aliwaasa viongozi wa Jimbo la Malindi kuacha ugomvi usiokuwa na tija ndani ya chama hicho na kusema kuwa kipindi hiki hakuna sababu yeyote inayopelekea wana CCM kugombana.
Aidha aliwaambia wakati wa uchaguzi utakapofika basi mtu yeyote kwa nafasi yake akiwa ni mwanachama wa CCM na amekidhi haja ya kuwa mwanachama ataruhusiwa kugombea kwa nafasi yeote anayopenda.
"Bahati nzuri sana chama chetu hakina masharti mengi katika kugombea, ikiwa Mwakilishi, Diwani na Mbunge uwe tu unajua kusoma na kuandika tena kiswahili hivyo sifa hizo ni nyepesi sana," alisema
Hivyo aliwataka viongozi na wanachama wa Jimbo hilo kumaliza tofauti zao na magomvi yasiyokuwa na tija na wote lengo lao liwe moja la kukiimarisha Chama cha Mapinduzi.
Sambamba na hayo Dk. Dimwa aliwakumbusha viongozi wa Chama Cha Mapinduzi kuwa ni lazima awe na msimamo wa kijamaa.
Alisema, itikadi ya kiongozi vitendo na tabia yake vinapaswa kujiridhisha kwa kuwaongoza wanachama wa CCM na wa wananchi kwa ujumla kuwa ni vya ujamaa.
Alisema, imani ya kiongozi inaambukiza na kuimarisha imani ya anaowaongoza hivyo kiongozi huyo anapaswa kuwa na vitendo na tabia nzuri kwa wale ambao anawaongoza.
"Lakini kiongozi anayegunduliwa na anayewaongoza kuwa ni mnafiki na kuwa msimamo wake wa uadui ni mkubwa huyo atakuwa ni adui wa Chama chetu," alisema.
Alisema, ameelezwa kuwa katika kikao hicho wajumbe watajadili taarifa za kazi kwa kipindi cha mwaka mmoja pamoja na kujadili utekelezaji wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi uliofanywa na Mbunge, Mwakilishi na madiwani wa Jimbo la Malindi.
Katika kujadili taarifa hizo aliwaomba wajumbe wa kikao hicho cha Halmashauri kuu ya Jimbo kuzingatia mambo muhimu kwa maslahi ya Jimbo, Chama na Taifa kwa ujumla.
"Taarifa nyingi ambazo zinatolewa nyengine zimekuwa watu wakizipika lakini nyengine siyo za kweli, ila nadhani Jimbo hili la Malindi tunaenda vizuri," alisema
Mahali: Kisiwandui, Zanzibar
Tarehe : 18 Febuari, 2024
𝐒𝐈𝐌𝐔 𝐈𝐌𝐄𝐈𝐓𝐀, 𝐍𝐄𝐄𝐌𝐀 𝐘𝐀 𝐔𝐓𝐀𝐓𝐔𝐙𝐈 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎!
18-06-2026
𝐑𝐔𝐀𝐇𝐀 𝐌𝐁𝐔𝐘𝐔𝐍𝐈 𝐘𝐀𝐅𝐔𝐑𝐈𝐊𝐀; “𝐂𝐇𝐈𝐄𝐅 𝐂𝐇𝐎𝐆𝐀𝐕𝐀𝐓𝐀𝐌𝐁𝐔𝐋𝐄” 𝐀𝐊𝐈𝐓𝐄𝐊𝐀 𝐌𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐎 𝐖𝐀 𝐇𝐀𝐃𝐇𝐀𝐑𝐀!
18-06-2026
𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐎 𝐂𝐇𝐀 𝐔𝐌𝐖𝐀𝐆𝐈𝐋𝐈𝐀𝐉𝐈 𝐍𝐈 𝐔𝐅𝐔𝐍𝐆𝐔𝐎 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐏𝐈𝐍𝐃𝐔𝐙𝐈 𝐘𝐀 𝐔𝐂𝐇𝐔𝐌𝐈 𝐖𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈: 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈
18-06-2026
𝐂𝐂𝐌 𝐘𝐀𝐔𝐍𝐆𝐀 𝐌𝐊𝐎𝐍𝐎 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐖𝐀 𝐍𝐉𝐎𝐌𝐁𝐄 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐙𝐀 𝐔𝐙𝐀𝐋𝐈𝐒𝐇𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐀𝐋𝐈
18-06-2026
𝐀𝐌𝐀𝐍𝐈 𝐍𝐈 𝐌𝐒𝐈𝐍𝐆𝐈 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐄𝐍𝐃𝐄𝐋𝐄𝐎: 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈
18-06-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐑𝐀𝐒𝐌𝐈 𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀!!
18-06-2026
𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀 𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐋𝐄𝐖𝐀 𝐍𝐉𝐎𝐌𝐁𝐄, 𝐀𝐇𝐈𝐌𝐈𝐙𝐀 𝐕𝐈𝐎𝐍𝐆𝐎𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐊𝐔𝐈𝐒𝐇𝐈 𝐃𝐇𝐀𝐍𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐍𝐀 𝐔𝐓𝐔 𝐊𝐖𝐀 𝐕𝐈𝐓𝐄𝐍𝐃𝐎
18-06-2026
𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀: 𝐂𝐂𝐌 𝐇𝐀𝐈𝐓𝐀𝐕𝐔𝐌𝐈𝐋𝐈𝐀 𝐔𝐙𝐄𝐌𝐁𝐄, 𝐕𝐈𝐎𝐍𝐆𝐎𝐙𝐈 𝐖𝐀𝐖𝐀𝐉𝐈𝐁𝐈𝐊𝐄 𝐊𝐔𝐓𝐀𝐓𝐔𝐀 𝐂𝐇𝐀𝐍𝐆𝐀𝐌𝐎𝐓𝐎 𝐙𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈
18-06-2026
𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀 𝐓𝐔𝐍𝐀𝐊𝐔𝐉𝐀𝐀𝐀, 𝐓𝐔𝐍𝐀𝐀𝐍𝐙𝐈𝐀 𝐑𝐔𝐀𝐇𝐀 𝐌𝐁𝐔𝐘𝐔𝐍𝐈!
18-06-2026
𝐌𝐈𝐊𝐎𝐏𝐎 𝐘𝐀 𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈𝐌𝐈𝐀 𝟏𝟎% 𝐘𝐀𝐂𝐇𝐎𝐂𝐇𝐄𝐀 𝐔𝐂𝐇𝐔𝐌𝐈 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐊𝐔𝐍𝐃𝐈 𝐌𝐀𝐀𝐋𝐔𝐌
18-06-2026
𝐍𝐃𝐆 𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀 𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐋𝐄𝐖𝐀 𝐑𝐔𝐕𝐔𝐌𝐀, 𝐀𝐇𝐈𝐌𝐈𝐙𝐀 𝐔𝐌𝐎𝐉𝐀 𝐍𝐀 𝐌𝐒𝐇𝐈𝐊𝐀𝐌𝐀𝐍𝐎 𝐍𝐃𝐈𝐎 𝐍𝐆𝐔𝐕𝐔 𝐘𝐀 𝐂𝐂𝐌
18-06-2026
𝐊𝐇𝐄𝐑𝐈 𝐘𝐀 𝐒𝐈𝐊𝐔 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐌𝐀𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐘𝐀 𝐌𝐓𝐎𝐓𝐎 𝐖𝐀 𝐀𝐅𝐑𝐈𝐊𝐀
18-06-2026
𝐌𝐇𝐄. 𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐀𝐍𝐀𝐖𝐀𝐏𝐄𝐍𝐃𝐀 𝐒𝐀𝐍𝐀 𝐖𝐀𝐓𝐀𝐍𝐙𝐀𝐍𝐈𝐀, 𝐖𝐀𝐓𝐔𝐌𝐈𝐒𝐇𝐈 𝐖𝐀 𝐔𝐌𝐌𝐀 𝐓𝐈𝐌𝐈𝐙𝐄𝐍𝐈 𝐖𝐀𝐉𝐈𝐁𝐔 𝐖𝐄𝐍𝐔 𝐊𝐈𝐊𝐀𝐌𝐈𝐋𝐈𝐅𝐔: 𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀
18-06-2026
𝐂𝐂𝐌 𝐇𝐀𝐈𝐓𝐎𝐑𝐔𝐃𝐈 𝐍𝐘𝐔𝐌𝐀 𝐊𝐔𝐋𝐈𝐍𝐃𝐀 𝐌𝐀𝐒𝐋𝐀𝐇𝐈 𝐘𝐀 𝐌𝐊𝐔𝐋𝐈𝐌𝐀 𝐖𝐀 𝐊𝐎𝐑𝐎𝐒𝐇𝐎: 𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀
18-06-2026
𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐓𝐈𝐁𝐔 𝐖𝐀 𝐍𝐄𝐂, 𝐈𝐓𝐈𝐊𝐀𝐃𝐈, 𝐔𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐍𝐀 𝐌𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐎 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀
18-06-2026
𝐂𝐂𝐌 𝐘𝐀𝐇𝐈𝐌𝐈𝐙𝐀 𝐒𝐈𝐀𝐒𝐀 𝐙𝐀 𝐊𝐈𝐒𝐓𝐀𝐀𝐑𝐀𝐁𝐔 𝐊𝐔𝐋𝐈𝐍𝐃𝐀 𝐀𝐌𝐀𝐍𝐈 𝐍𝐀 𝐔𝐓𝐔𝐋𝐈𝐕𝐔 𝐖𝐀 𝐍𝐂𝐇𝐈
18-06-2026
𝐕𝐈𝐊𝐔𝐍𝐃𝐈 𝐕𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐉𝐀𝐌𝐈𝐈 𝐋𝐈𝐍𝐃𝐈 𝐕Y𝐀𝐌𝐒𝐇𝐔𝐊𝐔𝐑𝐔 𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐊𝐖𝐀 𝐌𝐈𝐊𝐎𝐏𝐎 𝐈𝐒𝐈𝐘𝐎 𝐍𝐀 𝐑𝐈𝐁𝐀
18-06-2026
𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀: 𝐂𝐂𝐌 𝐈𝐍𝐀𝐓𝐇𝐀𝐌𝐈𝐍𝐈 𝐉𝐀𝐒𝐇𝐎 𝐋𝐀 𝐊𝐈𝐋𝐀 𝐌𝐓𝐀𝐍𝐙𝐀𝐍𝐈𝐀
18-06-2026
𝐁𝐀𝐀𝐃𝐇𝐈 𝐘𝐀 𝐍𝐔𝐊𝐔𝐔 𝐊𝐔𝐓𝐎𝐊𝐀 𝐌𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐎 𝐍𝐀 𝐖𝐀𝐀𝐍𝐃𝐈𝐒𝐇𝐈 𝐖𝐀 𝐇𝐀𝐁𝐀𝐑𝐈
18-06-2026
𝐌𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐎 𝐍𝐀 𝐖𝐀𝐀𝐍𝐃𝐈𝐒𝐇𝐈 𝐖𝐀 𝐇𝐀𝐁𝐀𝐑𝐈
18-06-2026