RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI, AL HAJJ DK. HUSSEIN ALI MWINYI, AMEENDELEA KUIHIMIZA JAMII JUU YA UMUHIMU WA KUDUMISHA AMANI
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Al hajj Dk. Hussein Ali Mwinyi, ameendelea kuihimiza jamii juu ya umuhimu wa kudumisha amani na kubeba imani ya dhati ndani ya mioyo yao kwa mustakbali wa taifa na ustawi wa jamii bora kwa maendeleo ya uchumi endelevu nchini.
Al hajj Dk. Mwinyi, alitoa nasaha hizo kwenye Msikiti Mabuluu Mfereji wa Wima, Mkoa wa Mjini Magharibi, alikojumuika pamoja na waumini wa dini ya Kiislamu kwenye ibada ya sala ya Ijumaa.
Rais, Al hajj Mwinyi, aliieleza Imani na amani ni vitu viwili vinavyokwenda sambamba na kutegemeana wakati wote, hivyo aliisihi jamii kadri wanapokusanyika pamoja kwenye maisha yao ya kila siku, wasichoke kuamini na kuendelea kuhimiza amani ya nchi na kuidumisha muda wote katika kuyaendea mazuri yote kwa ustawi wa jamii njema na taifa kwa ujumla.
“Imani na amani vinakwenda sambamba, amani ndio dini yetu, Uislamu unatutaka tueneze amani wakati wote, amani ikikosekana mambo mengine yote hayawezekani na hili tunalijua kutokana na wenzetu wanayoyapitia huko kwenye mataifa ya wenzetu, tunaona sehemu zenye vita hata ibada hazifanyiki, ili ipatikane amani lazima tuwe na Imani ndani ya nyoyo zetu” alisisitiza Al hajj Mwinyi.
Al hajj Dk Mwinyi alieleza, kila mmoja anawajibu wa kuitunza na kueneza amani kwa mustakbali wa taifa na ustawi wa jamii iliyobora.
Pia, aliwahimiza waumini hao kuendelea kuliombea taifa na viongozi kwa ujumla ili kuendelea kuwaongoza vyema na kuyatekeleza yote waliyowaahidi wananchi.
Rais Al Hajj Mwinyi alieleza, viongozi wanamajukumu makubwa na kubeba dhima kubwa hivyo, aliwasihi wanaumini hao na jamii kwa ujumla wasichoke kuwaombea mazuri na kuzidi kuwaombea kheir kwa Mwenyezi Mungu (S. W).
Akitoa nasaha za Ijumaa, Katibu Mtendaji kutoka Ofisi ya Mufti Zanzibar, Sheikh Khalid Ali Mfaume, alisifu juhudi za Rais Al Hajj Dk. Mwinyi kwa Imani aliyoijenga kwa waumini wa dini ya kiislamu na taifa kwa ujumla ikiwemo kujumuika nao pamoja kwenye ibada katika misikiti mbalimbali nchini sambamba na kuwaboresha ustawi wa maendeleo na uchumi wananchi wote.
Alisema juhudi zote hizo ni Imani yake kwa Wazanzibari na taifa lote, hasa jitihada za kuendelea kuimarisha huduma za jamii, uchumi na maendeleo ikiwemo ujenzi wa miundombinu imara na kuboresha mawasiliano.
Naye, Khatibu wa sala ya Ijumaa msikitini hapo, Sheikh Abdul Karim Said Abdulla aliihusia jamii kuendelea kupendana na kutendeana mema kwa kujizuia kuudhiana na kutendea mabaya.
Aliwashajihisha waumini hao kuendeleza mshikamo kwa kudumisha amani, umoja na upendo baina yao kwa ustawi wa jamii iliyo njema.
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
10-03-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
10-03-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
10-03-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
10-03-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
10-03-2026
πππ¦πππ‘ππ’ πππ πππ§. π ππππ₯π’ ππππ£π’πππππͺπ ππͺπ π¦πππ‘ππͺπ πππ₯ ππ¦ π¦πππππ
10-03-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
10-03-2026
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
10-03-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
10-03-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
10-03-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
10-03-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
10-03-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
10-03-2026
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
10-03-2026
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
10-03-2026
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
10-03-2026
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
10-03-2026
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
10-03-2026
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
10-03-2026
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
10-03-2026