RAISI WA ZANZIBAR DK HUSSEIN ALI MWINYI AMESEMA SUALA LA MSAADA WA KISHERIA SIO LA ZANZIBAR PEKEE BALI NI LA KIMATAIFA NA LINA HISTORIA KUBWA DUNIANI
Alisema, Zanzibar inawajibu wa kukeleza kwa vitendo huduma za sheria kama lilivyoelezwa kwenye Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, kifungu cha 12 pamoja na Sheria nyengine mbalimbali zilizopo nchini. Rais Dk. Mwinyi aliyasema hayo kwenye kilele cha maadhimisho ya nne ya wiki ya msaada wa Sheria, yaliyofanyika ukumbi wa Idrissa Abdul wakili, Kikwajuni Wilaya ya Mjini, Mkoa wa Mjini Magharibi.
Alisema, watoaji wa msaada wa sheria ni kiungo muhimu cha upatikanaji wa haki nchini hasa kwa wananchi wasio na uwezo wa fedha katika msada wa sheria. Dk. Mwinyi alieleza lengo la kilele cha maadhimisho hayo ni kuzifanya huduma za kisheria kuwa endelevu na zenye kuleta tija kwa jamii sambamba na kutatua changamoto nyengine zinazokwaza huduma za utoaji wa kisheria nchini. Alieleza Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Ofisi ya Rais Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora itaendelea kushirikiana na watoa msaada wa kisheria kwa kuhakikisha wanaendelea kutwaa tunzo zaidi, pia wanapata mazingira bora ya kutekeleza majukumu yao ya kazi.
Pia Dk. Mwinyi alieleza Serikali itahakikisha marekebisho ya Sera na Sheria ya Msaada wa Kisheria yanafanyika kwa ufanisi na haraka ili kukidhi matakwa yanayotakiwa.
Akizungumzia suala la upatikanaji wa vifaa na vitendelea kazi kwa wasaidizi wa wasaidizi wa kutoa msaada wa sheria, Rais Dk. Mwinyi aliwaahidi kwamba seikali inaunga mkono shughuli wanazozifanya b
upatikanaji wa vifaa vya kutendea kazi nayo ni changamoto nyengine. Mazingira wezeshi ya utoaji huduma yanahitaji kuwa na vifaa vya kutosheleza, vikiwemo vyombo vya usafiri, vifaa vya Ofisi kama vile printa, mashine za Fotokopi,
Komputa na kadhalika. Vinapokosekana vifaa hivi, ni dhahiri kuwa daraja la ufikiaji haki nalo hukosekana. Aidha, aliwataka watendaji mbalimbali wa Serikali na taasisi binafsi na vyombo vya kusimamia haki, kutoa ushirikiano wa kutosha kwa Watoaji msaada wa
kisheria ili kuwajengea uwezo wa kufanikisha kazi zao kwa uweledi. Sambamba na kuwaunga mkono na kupata ushirikiano wa kutosha.Hata hivyo alitoa kwa jamii nakuwataka kutimiza wajibu wao kila mmoja kwanafasiyake ili kuwe na mazingira bora ya upatikanaji msaada wa kisheria na kuzidi kuimarisha kiwango cha utawala bora nchini na misingi ya haki za binadamu. Akizungumza kwenye hafla hiyo, Jaji Mstafu Robert Makaramba alisema, maadhimisho ya 2023 yamekwenda sambmba na mazingira ya uboreshaji wa mifumo, miundo, sera na sheria zinazohakikisha huduma za msaada wa sheria zinatolewa katika hadhi ya zenye lengo la kufikia uwezeshaji wa Serikali kwa kushirikiana na watoa msaada ya kisheria, wadau wa maendeleo, taasisi za kiraia,
wadau wa sekta za haki wakiwemo Mahakama, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu, Polisi, Chuo cha Mafunzo na jamii husika.Nae Mkurugenzi wa Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria Zanzibar, Hanifa Ramadhan Said alieleza, watoaji wa msaada wa sheria wanafanya kazi kwa kujitolea na uzalendo kwa uhakikisha wananchi wa Zanzibar wasio na uwezo wanafikiwa na huduma za kisheria kwa sehemu zote ili kutatuliwa haja zao kisheria.
Alisema, maadhimisho hayo walishirikiana na taasisi zote zinazohusu masuala ya sheria, wakiwemo Mahakama, jeshi la Polisi, Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu, Chuo cha Mafunzo na wadau wengine. Maadhimisho hayo ya msaada wa sheria yaliyokuwa na kauli mbiu “Mazingira wezeshi kwa watoa msaada wa kisheria ni daraja la upatikanaji haki” ambayo yalianza Julai 17 na kuadhimishwa Julai 22 mwaka huu yalitanguliwa na shughuli mbalimbali za uhamasishaji ikiwemo kampeni ya vyumbo vya Habari,mkutano na vyombo vya Habari, kutembelea vyombo 21 vya Habari, kufanya program ya vijana kwa Unguja na Pemba, mihadhara na jamii, kufanya usafi wa mazingira kwenye hospitali ya wagonjwa wa Akili, Kidongochekundu, kufanya bonaza na hatimae kuadhimisha kilele halisi wiki ya msaada wa kisheria.
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
25-05-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
25-05-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
25-05-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
25-05-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
25-05-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
25-05-2026
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
25-05-2026
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
25-05-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
25-05-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
25-05-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
25-05-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
25-05-2026
𝗞𝗜𝗦𝗛𝗜𝗡𝗗𝗢 𝗖𝗛𝗔 𝗗𝗞𝗧. 𝗠𝗜𝗚𝗜𝗥𝗢 𝗖𝗛𝗔𝗣𝗢𝗞𝗘𝗟𝗘𝗪𝗔 𝗞𝗪𝗔 𝗦𝗛𝗔𝗡𝗚𝗪𝗘 𝗗𝗔𝗥 𝗘𝗦 𝗦𝗔𝗟𝗔𝗔𝗠
25-05-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
25-05-2026
𝗩𝗜𝗝𝗔𝗡𝗔 𝗧𝗨𝗜𝗟𝗜𝗡𝗗𝗘 𝗔𝗠𝗔𝗡𝗜 𝗬𝗔 𝗡𝗖𝗛𝗜 𝗬𝗘𝗧𝗨 - 𝗠𝗪𝗘𝗡𝗘𝗭𝗜 𝗞𝗘𝗡𝗔𝗡𝗜
25-05-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
25-05-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
25-05-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
25-05-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
25-05-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
25-05-2026