DK NCHIMBI: TUTAWAENZI WAASISI KWA KUENDELEZA UTUMISHI KWA WATU
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) , Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amezuru kaburi la Hayati Mzee Constantine Osward Millinga, aliyekuwa mmoja wa waasisi na wapigania uhuru kuanzia wakati wa Tanganyika African Association (TAA), Tanganyika African National Union (TANU), hadi CCM, katika makaburi ya familia yaliyopo, Mtaa wa Mhekela, Mbinga Mjini, mkoani Ruvuma, leo Jumatatu, Aprili 22, 2024.
Katibu Mkuu wa CCM Dk Nchimbi, na viongozi aliombatana nao katika msafara wa ziara yake mkoani humo, mbali ya kuweka shada ya maua, walipata nafasi ya kumsalimia Mjane wa Hayati Millinga, Bi. Maria Orign Mapunda (88), na kushiriki ibada ya kumuombea marehemu iliyoongozwa na Padri Andrea Silimbo.
Hayati Mzee Millinga ambaye alikuwa mmoja wa viongozi waandamizi wa TAA, TANU hadi CCM, akishirikiana na wenzake, wakiwemo viongozi wakuu na wanachama, wakiongozwa na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, akiwa sehemu ya waasisi wa vyama hivyo vya ukombozi vilivyobeba chimbuko na kuweka misingi ya uhuru na maendeleo ya Tanganyika, baadaye kuipata Tanzania, na kuzaliwa kwa CCM, alifariki dunia Machi 5, 2018.
Akizungumza wakati wa kutoa salaam za pole kwa wanafamilia na wananchi wengine, Dk Nchimbi amesema Chama Cha Mapinduzi kitaendelea kuenzi na kujifunza kupitia mema yote yaliyofanywa na waasisi wake wa vyama vya TANU na ASP, ikiwa ni sehemu ya njia ya kuendelea kulijenga Taifa letu kwa misingi imara ya kisiasa, uchumi na kuimarisha umoja na mshikamano wa kitaifa.
Dk Nchimbi aliambatana na Katibu wa NEC - Oganaizesheni Ndugu Issa Haju Gavu na Katibu wa NEC - Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM Taifa Ndugu Amos Makalla.
ποΈ22 Aprili, 2024
πMbinga Mjini - Ruvuma
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
08-12-2025
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
08-12-2025
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
08-12-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
08-12-2025
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
08-12-2025
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
08-12-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
08-12-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
08-12-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
08-12-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
08-12-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
08-12-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
08-12-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
08-12-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
08-12-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
08-12-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
08-12-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
08-12-2025
TAARIFA KWA UMMA
08-12-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
08-12-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
08-12-2025