BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
Awahakikishia viongozi wa dini, taasisi za kijamii na kimila
Awapongeza wanawake kusimamia amani
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi amesema kuwa maoni yoyote yanayolenga kuhakikisha Tanzania inaendelea kudumisha amani na utulivu, hayajawahi kupuuzwa na hayatapuuzwa.
Aidha, Balozi Nchimbi amemwelezea Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa ni kiongozi mwanamke ambaye uongozi wake, umeongeza heshima kubwa kwa wanawake na Tanzania, akiendeleza safari iliyoanzishwa na viongozi wengine wanawake jasiri, tangu wakati wa kudai uhuru na kuiweka Tanzania katika ramani ya dunia.
Balozi Dkt. Nchimbi amesema hayo alipokuwa akifungua Jukwaa la Wanawake wa Arusha 2025, lililowakutanisha wanawake katika kujadili maada ya ‘Safari ya Mwanamke Arusha 2025’, katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Arusha (AICC), jijini Arusha, Jumanne, tarehe 24 Juni 2025.
“Hivyo ndivyo wanawake wanalitazama taifa letu (kama wanavyotazama watoto wao). Wanataka nchi yetu iendelee kuwa na amani, nchi yetu iendelee kuwa tulivu. Nataka nitumie nafasi hii, kuwahakikishia wanawake wa Tanzania, kwamba CCM inatambua dhamana yake ya kulinda amani ya nchi yetu.
“Nataka niwahakikishie viongozi wa mila, viongozi wa dini, viongozi wa taasisi za kijamii, niwahakikishie Watanzania wote, kwamba maoni yenu yanayohusu kuendeleza amani na utulivu katika nchi yetu, hatujawahi kuyapuuza kama Chama Cha Mapinduzi,” alisema Balozi Nchimbi na kuongeza;
“Na tukitambua kuwa amani ndiyo kipaumbele cha kwanza cha mwanamke wa Tanzania…akitambua kwamba kuilinda amani ni kuilinda nchi yetu, kukilinda kizazi cha sasa na kizazi kijacho, tutaendelea kuisimamia amani ya nchi yetu kwa nguvu zetu zote.”
Jukwaa hilo ambalo wazungumzaji wakuu wa mada hiyo walikuwa ni pamoja na Mama Fatma Karume, mjane wa Hayati Mzee Abeid Amani Karume, Mama Anne Makinda, Dkt. Asha-rose Migiro, Bi. Zakhia Meghji, na wanawake wengine vijana, lililenga kuzungumzia safari ya mwanamke katika nyanja mbalimbali za maisha, kisiasa, kiuchumi na kijamii nchini.
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
27-11-2025
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
27-11-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
27-11-2025
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
27-11-2025
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
27-11-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
27-11-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
27-11-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
27-11-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
27-11-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
27-11-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
27-11-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
27-11-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
27-11-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
27-11-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
27-11-2025
TAARIFA KWA UMMA
27-11-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
27-11-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
27-11-2025
MONGELLA AONGOZA MAZISHI YA KADA WA CCM JIJINI MWANZA
27-11-2025
ASIYETII SHERIA, KATIBA NA KUWA TAYARI KUUA KWA MASLAHI BINAFSI HUO NI UGAIDI’
27-11-2025