BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
Awahakikishia viongozi wa dini, taasisi za kijamii na kimila
Awapongeza wanawake kusimamia amani
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi amesema kuwa maoni yoyote yanayolenga kuhakikisha Tanzania inaendelea kudumisha amani na utulivu, hayajawahi kupuuzwa na hayatapuuzwa.
Aidha, Balozi Nchimbi amemwelezea Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa ni kiongozi mwanamke ambaye uongozi wake, umeongeza heshima kubwa kwa wanawake na Tanzania, akiendeleza safari iliyoanzishwa na viongozi wengine wanawake jasiri, tangu wakati wa kudai uhuru na kuiweka Tanzania katika ramani ya dunia.
Balozi Dkt. Nchimbi amesema hayo alipokuwa akifungua Jukwaa la Wanawake wa Arusha 2025, lililowakutanisha wanawake katika kujadili maada ya ‘Safari ya Mwanamke Arusha 2025’, katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Arusha (AICC), jijini Arusha, Jumanne, tarehe 24 Juni 2025.
“Hivyo ndivyo wanawake wanalitazama taifa letu (kama wanavyotazama watoto wao). Wanataka nchi yetu iendelee kuwa na amani, nchi yetu iendelee kuwa tulivu. Nataka nitumie nafasi hii, kuwahakikishia wanawake wa Tanzania, kwamba CCM inatambua dhamana yake ya kulinda amani ya nchi yetu.
“Nataka niwahakikishie viongozi wa mila, viongozi wa dini, viongozi wa taasisi za kijamii, niwahakikishie Watanzania wote, kwamba maoni yenu yanayohusu kuendeleza amani na utulivu katika nchi yetu, hatujawahi kuyapuuza kama Chama Cha Mapinduzi,” alisema Balozi Nchimbi na kuongeza;
“Na tukitambua kuwa amani ndiyo kipaumbele cha kwanza cha mwanamke wa Tanzania…akitambua kwamba kuilinda amani ni kuilinda nchi yetu, kukilinda kizazi cha sasa na kizazi kijacho, tutaendelea kuisimamia amani ya nchi yetu kwa nguvu zetu zote.”
Jukwaa hilo ambalo wazungumzaji wakuu wa mada hiyo walikuwa ni pamoja na Mama Fatma Karume, mjane wa Hayati Mzee Abeid Amani Karume, Mama Anne Makinda, Dkt. Asha-rose Migiro, Bi. Zakhia Meghji, na wanawake wengine vijana, lililenga kuzungumzia safari ya mwanamke katika nyanja mbalimbali za maisha, kisiasa, kiuchumi na kijamii nchini.
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
27-02-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
27-02-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
27-02-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
27-02-2026
πππ¦πππ‘ππ’ πππ πππ§. π ππππ₯π’ ππππ£π’πππππͺπ ππͺπ π¦πππ‘ππͺπ πππ₯ ππ¦ π¦πππππ
27-02-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
27-02-2026
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
27-02-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
27-02-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
27-02-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
27-02-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
27-02-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
27-02-2026
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
27-02-2026
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
27-02-2026
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
27-02-2026
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
27-02-2026
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
27-02-2026
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
27-02-2026
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
27-02-2026
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
27-02-2026