Waumini wa Kiislamu wametakiwa kujipanga kwa kuendelea kuwasaidia watu wenye mahitaji maalum na mayatima, wajane na watu wasiojiweza hasa katika mwezi mtukufu wa Ramadhan unaotarajiwa kuwafikia hivi karibuni.
Hayo yamesemwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Alhajj Hemed Suleiman Abdulla wakati akiwasalimia waumini wa Masjid NOOR kwa HAJI TUMBO mara baada ya kumaliza Ibada ya Sala ya Ijumaa.
Amesema ni lazima wazanzibari na waumini wa dini ya kiislamu kuendeleza utamaduni wa kusaidiana pamoja na kuwasaidia watu wasio na uwezo ili kuweka usawa baina yao hasa katika mwezi mtukufu wa ramadhani mwezi ambao una fadhila nyingi sana ndani yake.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amesisitiza kuwa mwezi wa Ramadhani umeshakaribia hivyo ni wajibu kwa waumini wa dini ya kiisalmu na wazanzibari kwa ujumla kuuendeleza yale yote ambayo waliokuwa wakiyafanya miezi yote kumi na moja (11) ambayo yanamfurahisha mwenyezimungu ikiwemo kutoa kile ambacho wameruzukiwa na Allah (S.W) kwa wanao hitaji ili kupata fadhila zake.
Alhajj Hemed amewataka waumini na Wazanzibari kuzidisha imani kwa viongozi wao ambao wanawaongoza na kuahidi kuwa Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar inayoongozwa na Rais wa Zanzibar na Mwaenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dkt. Hussein Ali Mwinyi itaendelea kutatua changamoto zote zinazowakabili wananchi wake.
Sambamba na hayo Alhajj Hemed amewashukuru waumini na wazanzibari wote kwa ujumla kwa kuendelea kuishi kwa amani na utulivu jambo ambalo ndio dira ya maendeleo ya Taifa kwani kufanya hivyo ndio kunakopelekea Serikali kufanya yale yote iliyoyaahidi kwa wanachi wake kwa faida ya vizazi vya sasa na baadae.
Mapema akitoa Khutba katika Sala ya Ijumaa, Ustadh, TWAHIR ALI amewataka waumini wa Dini ya Kiislam kuamini kuwa kila anachokifanya mwanadamu atalitwa kulingana na matendo yake hivyo ni lazima kuzidisha Ibada hasa katika kipindi hichi Cha kuukaribisha mwezi mtukufu wa Ramadhan.
Ustadh Twahir amewasisitiza waumini kuwa na subra kwa kila jambo ambalo muumini linamtokea kwani kufanya hivyo ndio kufata nyayo za mitume wote ambalo walioletwa kuja kuitangaza dini ya mwenyezi mungu sambamba na kuyaacha yale yote ambayo yanamkirihisha Allah (S.W)
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
09-12-2025
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
09-12-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
09-12-2025
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
09-12-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
09-12-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
09-12-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
09-12-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
09-12-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
09-12-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
09-12-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
09-12-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
09-12-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
09-12-2025
TAARIFA KWA UMMA
09-12-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
09-12-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
09-12-2025