Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla amesema Viwanja vya ndege ni sehemu muhimu sana kwa ukuwaji wa uchumi wa Zanzibar ambayo inategemea zaidi shuhuli za utalii ambazo zinakwenda sambamba na uwepo wa miundombinu mizuri ya viwanja hivyo.
Ameyasema hayo wakati alipofanya ziara ya kutembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa miradi mbali mbali inayojengwa na Mamlaka ya Viwanja vya ndege Zanzibari.
Mhe. Hemed amesema kuwa viwanja vya ndege ni milango mikuu ya nchi yoyote ile duniani inayotumika kwa kusafirishia wageni ambao huchangia kwa kiwango kikubwa kukuwa kwa uchumi na kuongezeka kwa pato la nchi husika.
Amesema kuwa utakapokamilika ujenzi wa Miradi ya Viwanja vya ndege vya Terminal One na terminal two na eneo la biashara lililopo terminal three vitaondoa changamoto ya msongamano wa abiria wanaokaa muda mrefu kusubiri kuhudumiwa sambamba na kuongezeka kwa uwezo wa kutoa huduma bora na za haraka jambo ambalo litapelekea wageni wengi kuendelea kuitembelea Zanzibar mara kwa mara.
Makamu wa Pili wa Rais amemuagiza Mkurugenzi wa Mamlaka ya Viwanja vya ndege kuhakikisha kila penye uwezekano wa kupatikana kwa kodi kuhakikisha kodi hio inakusanywa na kuingia Serikalini ili kuendelea kuimarisha na kuboresha huduma mbali mbali za kijamii kwa wananchi wa Zanzibar.
Aidha amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendelea kutoa ushirikano kwa kampuni zote zinazojenga miradi mbali mbali nchini ikiwemo kampuni ya Estim Constraction Ltd inayojenga miradi ya Viwanja vya ndege vya Zanzibar ili kuhakikisha wanakabidhi miradi hio kwa wakati uliopangwa na kwa kuzingatia viwango na ubora wa hali ya juu.
Nae Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji Mhe. Dkt Khalid Salum Muhammed amesema uchumi wa Zanzibar unategemea zaidi Utalii hivyo ni lazima kuimarisha miundombinu ya kimkati ikiwemo viwanja vya ndege ili kuhakikisha Utalii unakuwa kwa kasi zaidi na pato la nchi linaongezeka kupitia wagemi wanaoingia Zanzibar.
Dkt. Khalid amesema ujenzi wa miradi hio inaendelea vizuri na hakuna changamoto yoyote hadi sasa ambayo itasabisha kuchelewa kukamilika kwa ujenzi wa miradi hiyo sambamba na kuahidi kuwa uongozi wa wizara utahakikisha miradi yote inakamilika kwa wakati na kwa kiwango kilichokusidiwa ili kufikia malengo ya Serikali iliyojiwekea.
Kwa upande wake mshauri elekezi kutoka kampuni ya Anova Consult Ltd Muhandisi IBRAHIM GASPER amesema kuwa hadi sasa miradi yote inakwenda vizuri na ipo ndani ya wakati ambapo amemuhakikishia Makamu makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar kuwa watakabidhi miradi hiyo ndani ya muda uliopangwa na kwa kuzingatia viwango vya hali juu.
Gasper ameushukuru uongozi wa Wizara ya Ujenzi Mawasiliano na Usafirishaji pamoja na Mamlaka ya Viwanja vya ndege kwa ushirikiano mkubwa wanaowapatia jambo ambalo linawapa ari ya kufanya kazi kwa haraka na kukamilisha ujenzi huo kabla ya wakati uliopangwa kwa maslahi mapana ya wananchi wa Zanzibar.
Katika ziara hio Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amekagua UKARABATI WA JENGO LA TERMINAL ONE , UJENZI WA GENGO LA TERMINAL TWO pamoja NA UJENZI WA SEHEMU YA BIASHARA ILIYOPO TERMINAL THREE.
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
09-12-2025
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
09-12-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
09-12-2025
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
09-12-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
09-12-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
09-12-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
09-12-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
09-12-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
09-12-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
09-12-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
09-12-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
09-12-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
09-12-2025
TAARIFA KWA UMMA
09-12-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
09-12-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
09-12-2025