KINANA AHIMIZA SERIKALI KUHARAKISHA MISAADA ZAID KWA WAATHIRIKA WA MAFURIKO RUFIJI.
MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Ndg. Abdulrahman Kinana, amesema msaada mkubwa wa haraka unahitajika kwa wananchi walioathirika na mafuriko wilayani Rufiji, Mkoa wa Pwani.
Amesema hayo baada ya kupokea taarifa na kushuhudia hali ilivyo wilayani humo, ambapo kata 12 kati ya 13 zimeathirika, na kutaka serikali kuharakisha misaada kikiwemo chakula na malazi kwa zaidi ya watu 88,000 walioathirika.
Kinana ametoa wito huo leo, Aprili 9, 2024, alipokuwa akizungumza na wananchi wa vijiji vya Muhoro na Chumbi, baada ya kuwatembelea na kuwapa pole wananchi waliokumbwa na mafuriko hayo, yaliyotokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha na kusababisha Mto Rufiji kufurika katika makazi ya watu.
"Nimezungumza na Waziri Mkuu (Kassim Majaliwa), kwa namna nilivyojionea na nimemweleza uharaka wa Mahitaji, sina shaka hata kidogo na yeye atakuja kujionea. Haraka ameitisha kikao na mawaziri wote wanaohusika na maswala ya maafa, nina hakika akishakuja hapa kasi ya kutoa huduma itaongezeka ” amesema.
Amesisitiza kuwa, kutokana na hali hiyo anaihimiza serikali kuongeza juhudi za kutoa huduma kwa wananchi waliopatwa na maafa hayo ambayo yameathiri pia shule na zahanati.
“Nimekuja kuwapa pole kwa niaba ya Rais, kwa niaba ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Nimekuja kujionea hali ilivyo, lakini niendelee kutumia fursa hii kuihimiza serikali kuleta misaada haraka kwa wananchi walioathirika," amesisitiza Makamu Mwenyekiti Ndg. Kinana.
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
09-12-2025
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
09-12-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
09-12-2025
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
09-12-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
09-12-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
09-12-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
09-12-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
09-12-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
09-12-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
09-12-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
09-12-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
09-12-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
09-12-2025
TAARIFA KWA UMMA
09-12-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
09-12-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
09-12-2025