.DK.HUSSEIN MWINYI ASHUHUDUA ITIAJI WA SAINI YA MRADI WA SEKTA YA AFYA BAINA YA CHINA NA ZANZIBAR IKULU LEO
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi ameishukuru Serikali ya China kwa ushirikiano wanaoendelea kuutoa Tanzania ikiwemo Zanzibar kwenye masuala mbalimbali ya maendeleo.
Dk. Mwinyi ametoa shukurani hizo Ikulu, Zanzibar alikoshuhudia utiaji wa shaini mikataba ya miradi mitano ya ushikirikano kwenye sekta ya afya baina ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China.
Katika hafla hiyo Rais Dk. Mwinyi alisema, Zanzibar imenufaika na fursa nyingi za maendeleo kupitia misaada tofauti inayoletwa kutoka China hasa sekta za Afya na Elimu ikiwemo Tanzania kujifunza uzoefu wa masuala mbalimbali ya afya, kupokea timu za madaktari bingwa wanaofika nchini kwaajili ya kubadilishana uzoefu na wazawa hali aliyoieleza imeimarisha uhusiano mwema uliopo baina yao.
Alisema mikataba minne aliyoishuhudia sio tuu itaimarisha huduma za tiba nchini pekee, lakini itajenga ushirikiano mwema baina ya maofisa wa Afya wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na China jambo alilolieleza ni ishara ya uhusiano mwema uliopo baina ya mataifa mawili hayo.
Rais Dk. Mwinyi alieleza, uhusiano wa China na Tanzania utakumbukwa zaidi kwa kuinufaisha Zanzibar kupitia sekta ya afya katika suala zima la kuimarisha miundombinu ya afya, vifaa tiba, dawa mafunzo ya muda mrefu na mfupi kwa wataalamu wa afya wazawa, pamoja na timu za madaktari bingwa wanaofika Zanzibar kila mwaka kwa nyakati tofauti na Tanzania kwa ujumla, jambo alilolieleza kwamba limeimarisha uhusiano wa China na Tanzania.
Aidha, Dk. Mwinyi alimpongeza Balozi mdogo wa China aliepo Zanzibar, Zhang Zhisheng kwa kazi kubwa anayoifanya ya kukuza ushiriiano uliopo baina ya China na Zanzibar.
“Wenzetu China mmetusaidia sana hata tukieleza hatutomaliza, nimeshuhudia utiaji wa saini mikataba minne ya ushirikiano baina ya Zanzibar na China, kupitia sekta ya afya, miradi hii itaendelea kuimarisha ushirikiano wetu uliopo” Alisifu Dk. Mwinyi.
Naye, Rais wa taasisi ya Ushirikiano baina ya Afrika na China, (CAPFA) Dk. Li Bin ameeleza miradi hiyo itatatua maradhi sugu jamii hasa kina Mama na kutoa fursa za miradi mbalimbali itakayonufaisha pande zote za ushirikiano wa Nchi hizo na kuboresha huduma za sekta ya Afya.
Dk. Li pia aliisifu Tanzania kwa ukaribu wa kihistoria baina yake na China alioueleza ni wa mda mrefu tokea uhai wa Mwenyekiti Mao Zedong na Mwl. Julius Kambarage Nyerere, zaidi ya miaka 50 iliyopita.
Alisema, Tanzania imebarikiwa kuwa na raia wenye ukarimu, upendo na ushirikiano, ambao ni kielelezo chema kwenye kukuza uhusiano uliopo baina yao na China.
Alieleza, ushirikiano huo ni mwendelezo wa fikra njema za waasisi wa mataifa mawili hayo, Mwenyekiti Mao Zedong na Mwl. Julius Kambarage Nyerere na kueleza Serikali ya Jamhuri ya watu wa China inajivunia uhusiano huo kwa maendeleo makubwa yaliyofikiwa na watu wa China na Tanzania ikiwemo kukuza uhusiano wa jamii na uchumi.
Akizungumza kwenye hafla hiyo, Waziri wa Afya, Nassor Mazrui alisema mikataba waliyoisaini mbele ya Rais Dk. Mwinyi itagharimu dola za Marekani 4,76,000 sawa na Shilingi bilioni 1.2 za Tanzania.
Miongo mwa miradi iliyosainiwa ni pamoja na mradi wa Ushirikiano wa hospitali baina ya China na Afrika, Utafiti na udhibiti wa magonjwa ya kitropiki ikiwemo Kichocho, Uchunguzi wa saratani ya shingo ya mlango wa kizazi na kituo cha matibabu ya Mama na Mtoto pamoja na msaada wa vifaa tiba.
Aidha, hospitali zitakazonufaika na ushirikiano huo ni hospotali kuu, Mnazi Mmoja, Kivunge, Chake chake na Abdallah Mzee Pemba.
🔰𝐀𝐒𝐀𝐍𝐓𝐄𝐍𝐈 𝐒𝐀𝐍𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎!
01-06-2026
𝐒𝐇𝐔𝐋𝐄 𝐘𝐀 𝐌𝐒𝐈𝐍𝐆𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐒𝐀𝐃𝐀𝐋𝐀 𝐘𝐀𝐎𝐍𝐃𝐎𝐀 𝐊𝐄𝐑𝐎 𝐘𝐀 𝐊𝐔𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐀 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐌𝐄𝐓𝐀 𝟏𝟐 𝐊𝐖𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐈
01-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐀𝐀𝐍𝐙𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀𝐍𝐈 𝐇𝐀𝐈, 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
01-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐀𝐀𝐍𝐙𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐇𝐀𝐈 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
01-06-2026
𝐍𝐈 𝐌𝐔𝐃𝐀 𝐖𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐇𝐀𝐈-𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎 𝐒𝐀𝐒𝐀
01-06-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐌𝐏𝐀 𝐁𝐀𝐉𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐒𝐈𝐇𝐀 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐘𝐄 𝐔𝐋𝐄𝐌𝐀𝐕𝐔 𝐖𝐀 𝐌𝐈𝐆𝐔𝐔
01-06-2026
MAWENZI YAVUNJA REKODI: MITUNGI 3,313 YA OKSIJENI YAZALISHWA KWA MIEZI 6, ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 126 ZAOKOLEWA!
01-06-2026
MAFURIKO YA WANANCHI WA SIHA KWENYE MKUTANO MKUBWA WA HADHARA
01-06-2026
MAPOKEZI YA KATIBU MWENEZI WA CCM NDUGU KENANI L KIHONGOSI MKOANI KILIMANJARO
01-06-2026
🔰 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐒𝐇𝐈𝐍𝐃𝐎 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
01-06-2026
CCM INAWATAKIA HERI YA SIKUKUU YA EID AL ADHA
01-06-2026
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
01-06-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
01-06-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
01-06-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
01-06-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
01-06-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
01-06-2026
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
01-06-2026
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
01-06-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
01-06-2026