.DK.HUSSEIN MWINYI ASHUHUDUA ITIAJI WA SAINI YA MRADI WA SEKTA YA AFYA BAINA YA CHINA NA ZANZIBAR IKULU LEO
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi ameishukuru Serikali ya China kwa ushirikiano wanaoendelea kuutoa Tanzania ikiwemo Zanzibar kwenye masuala mbalimbali ya maendeleo.
Dk. Mwinyi ametoa shukurani hizo Ikulu, Zanzibar alikoshuhudia utiaji wa shaini mikataba ya miradi mitano ya ushikirikano kwenye sekta ya afya baina ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China.
Katika hafla hiyo Rais Dk. Mwinyi alisema, Zanzibar imenufaika na fursa nyingi za maendeleo kupitia misaada tofauti inayoletwa kutoka China hasa sekta za Afya na Elimu ikiwemo Tanzania kujifunza uzoefu wa masuala mbalimbali ya afya, kupokea timu za madaktari bingwa wanaofika nchini kwaajili ya kubadilishana uzoefu na wazawa hali aliyoieleza imeimarisha uhusiano mwema uliopo baina yao.
Alisema mikataba minne aliyoishuhudia sio tuu itaimarisha huduma za tiba nchini pekee, lakini itajenga ushirikiano mwema baina ya maofisa wa Afya wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na China jambo alilolieleza ni ishara ya uhusiano mwema uliopo baina ya mataifa mawili hayo.
Rais Dk. Mwinyi alieleza, uhusiano wa China na Tanzania utakumbukwa zaidi kwa kuinufaisha Zanzibar kupitia sekta ya afya katika suala zima la kuimarisha miundombinu ya afya, vifaa tiba, dawa mafunzo ya muda mrefu na mfupi kwa wataalamu wa afya wazawa, pamoja na timu za madaktari bingwa wanaofika Zanzibar kila mwaka kwa nyakati tofauti na Tanzania kwa ujumla, jambo alilolieleza kwamba limeimarisha uhusiano wa China na Tanzania.
Aidha, Dk. Mwinyi alimpongeza Balozi mdogo wa China aliepo Zanzibar, Zhang Zhisheng kwa kazi kubwa anayoifanya ya kukuza ushiriiano uliopo baina ya China na Zanzibar.
“Wenzetu China mmetusaidia sana hata tukieleza hatutomaliza, nimeshuhudia utiaji wa saini mikataba minne ya ushirikiano baina ya Zanzibar na China, kupitia sekta ya afya, miradi hii itaendelea kuimarisha ushirikiano wetu uliopo” Alisifu Dk. Mwinyi.
Naye, Rais wa taasisi ya Ushirikiano baina ya Afrika na China, (CAPFA) Dk. Li Bin ameeleza miradi hiyo itatatua maradhi sugu jamii hasa kina Mama na kutoa fursa za miradi mbalimbali itakayonufaisha pande zote za ushirikiano wa Nchi hizo na kuboresha huduma za sekta ya Afya.
Dk. Li pia aliisifu Tanzania kwa ukaribu wa kihistoria baina yake na China alioueleza ni wa mda mrefu tokea uhai wa Mwenyekiti Mao Zedong na Mwl. Julius Kambarage Nyerere, zaidi ya miaka 50 iliyopita.
Alisema, Tanzania imebarikiwa kuwa na raia wenye ukarimu, upendo na ushirikiano, ambao ni kielelezo chema kwenye kukuza uhusiano uliopo baina yao na China.
Alieleza, ushirikiano huo ni mwendelezo wa fikra njema za waasisi wa mataifa mawili hayo, Mwenyekiti Mao Zedong na Mwl. Julius Kambarage Nyerere na kueleza Serikali ya Jamhuri ya watu wa China inajivunia uhusiano huo kwa maendeleo makubwa yaliyofikiwa na watu wa China na Tanzania ikiwemo kukuza uhusiano wa jamii na uchumi.
Akizungumza kwenye hafla hiyo, Waziri wa Afya, Nassor Mazrui alisema mikataba waliyoisaini mbele ya Rais Dk. Mwinyi itagharimu dola za Marekani 4,76,000 sawa na Shilingi bilioni 1.2 za Tanzania.
Miongo mwa miradi iliyosainiwa ni pamoja na mradi wa Ushirikiano wa hospitali baina ya China na Afrika, Utafiti na udhibiti wa magonjwa ya kitropiki ikiwemo Kichocho, Uchunguzi wa saratani ya shingo ya mlango wa kizazi na kituo cha matibabu ya Mama na Mtoto pamoja na msaada wa vifaa tiba.
Aidha, hospitali zitakazonufaika na ushirikiano huo ni hospotali kuu, Mnazi Mmoja, Kivunge, Chake chake na Abdallah Mzee Pemba.
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
02-01-2026
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
02-01-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
02-01-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
02-01-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
02-01-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
02-01-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
02-01-2026
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
02-01-2026
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
02-01-2026
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
02-01-2026
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
02-01-2026
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
02-01-2026
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
02-01-2026
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
02-01-2026
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
02-01-2026
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
02-01-2026
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
02-01-2026
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
02-01-2026
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
02-01-2026
TAARIFA KWA UMMA
02-01-2026