MABALOZI WA MAREKANI, INDIA, ALGERIA, NA UGANDA WAWAPONGEZA DKT. SAMIA, BALOZI NCHIMBI NA DKT. MWINYI
Jumuiya ya kimataifa, hususan mabalozi wa nchi mbalimbali waliopo Tanzania, ikiwa ni pamoja na Uganda, Algeria, India na Marekani, wamepongeza uteuzi wa Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa mgombea wa urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka huu.
Mbali na kumpongeza Dkt. Samia, ambaye ni Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mabalozi hao pia wamewapongeza Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi kwa kuteuliwa kuwa mgombea mwenza wa urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, pamoja na Dkt. Hussein Ali Mwinyi kwa kuthibitishwa kuwa mgombea wa urais wa Zanzibar.
Mabalozi hao walitoa pongezi hizo wakati wa mazungumzo yao na Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, yaliyofanyika kwa nyakati tofauti leo, tarehe 12 Februari 2025, katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, jijini Dar es Salaam.
Katika mazungumzo yake na Katibu Mkuu wa CCM, Balozi wa Algeria nchini Tanzania, Mhe. Ahmed Djellal, aliangazia pia uhusiano wa kihistoria kati ya Tanzania na Algeria, hususan mchango wa Tanzania katika harakati za ukombozi wa Afrika. Aidha, alitoa pongezi kwa Rais Dkt. Samia, Rais Dkt. Mwinyi na Balozi Nchimbi kwa kuaminiwa kupeperusha bendera ya CCM katika Uchaguzi Mkuu ujao.
Balozi Nchimbi na Balozi Djellal pia walijadili umuhimu wa kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi baina ya Tanzania na Algeria kupitia sekta mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kubadilishana uzoefu wa kiuongozi na fursa za masomo.
Katika mazungumzo yake na Katibu Mkuu wa CCM, Balozi wa India nchini Tanzania, Mhe. Bishwadip Dey, alieleza kuwa uhusiano kati ya Tanzania na India umeendelea kuimarika na kunufaisha pande zote mbili, hususan katika sekta za biashara, uwekezaji, teknolojia na afya. Pia, alitoa pongezi kwa CCM kwa kuwaamini Rais Dkt. Samia, Rais Dkt. Mwinyi na Balozi Nchimbi kuwa wagombea wake katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu.
Vilevile, katika mazungumzo kati ya Balozi Nchimbi na Naibu Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Mhe. Andrew Lentz, pande zote zilisisitiza umuhimu wa kuendeleza uhusiano wa muda mrefu kati ya Tanzania na Marekani katika nyanja mbalimbali. Mhe. Lentz pia alitoa pongezi zake na kuwatakia kila la heri Rais Dkt. Samia, Rais Dkt. Mwinyi na Balozi Nchimbi kufuatia maamuzi ya Mkutano Mkuu Maalum wa CCM.
Kwa upande wake, Balozi wa Uganda nchini Tanzania, Mhe. Kanali Mstaafu Fred Mwesigye, alifikisha salamu za pongezi kutoka kwa Serikali ya Uganda na chama tawala cha NRM, akieleza kuwa Uganda inatambua na kuheshimu mchango wa Tanzania na CCM katika harakati za ukombozi wa Afrika. Alimhakikishia Balozi Nchimbi kuwa uhusiano wa kidugu kati ya Tanzania na Uganda utaendelea kuimarika kwa manufaa ya wananchi wa pande zote mbili.
Mhe. Balozi Mwesigye alisisitiza kuwa urafiki wa kihistoria kati ya Tanzania na Uganda umejengwa juu ya misingi imara ya mshikamano wa kikanda, ushirikiano wa kisiasa na maendeleo ya kiuchumi, ambao utaendelea kuimarika kwa ustawi wa mataifa hayo mawili.
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
04-11-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
04-11-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
04-11-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
04-11-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
04-11-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
04-11-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
04-11-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
04-11-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
04-11-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
04-11-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
04-11-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
04-11-2025
TAARIFA KWA UMMA
04-11-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
04-11-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
04-11-2025
MONGELLA AONGOZA MAZISHI YA KADA WA CCM JIJINI MWANZA
04-11-2025
ASIYETII SHERIA, KATIBA NA KUWA TAYARI KUUA KWA MASLAHI BINAFSI HUO NI UGAIDI’
04-11-2025
πππ π¬ππ¦ππ¦ππ§πππ πͺπππ’π πππ ππ¨πππππππͺπ ππͺπ ππ¨πππ‘πππ§ππ π¨πͺπππ’, π¨πππππ‘ππ’ π‘π π¨πππππππ¨, π¬ππππ ππ π πππ¨π‘ππ - πππ. πππ©π¨
04-11-2025
KAENI KIMYA KAMA HAMJUI NCHI ILIKOTOKA - WASIRA
04-11-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amefungua kiwanda cha kutengeneza mabomba ya maji na uchakataji pamba cha MOLI Oil Mills Co. Ltd kilichopo Bariadi Mkoani Simiyu tarehe 16 Juni, 2025.
04-11-2025