MAKONDA AMTEMBELEA ASKOFU DKT MALASUSA, AMHAKIKISHIA VIONGOZI WA KIROHO KUMWOMBEA RAIS SAMIA
Katibu wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (NEC) Taifa, Ndugu Paul Christian Makonda amemtembelea Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Askofu Mkuu Dkt. Alex Gehaz Malasusa, kwa lengo la kumsalimia na kumpongeza kwa kuchaguliwa kwake kuliongoza kanisa hilo, kwa mara nyingine.
Katika mazungumzo yao yaliyofanyika leo Jumamosi, Disemba 2, 2023, Askofu Mkuu Dkt. Malasusa ambaye pia ni Askofu wa KKKT Dayosisi ya Mashariki na Pwani (DMP), amesema viongozi wa dini na kiroho wataendelea kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ili aendelee kuwa na busara, where hekima anapoendelea kuliongoza taifa, kama ambavyo tayari ameonesha uimara, tangu alipobeba dhamana na Mamlaka ya Kiongozi Mkuu wa Nchi.
Mbali ya kumpongeza Ndugu Makonda kwa kuteuliwa kuwa Mkuu wa Idara ya NEC, Uenezi, Itikadi na Mafunzo na kumtakia heri anapotimiza wajibu huo, Baba Askofu Dkt. Malasusa ameongeza nasaha zake kwa kutoa wito kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuendelea kusimamia misingi yake, ikiwemo kuhakikisha Watanzania wote wanatendewa haki, kuwa sikio lao la wananchi wanyonge na kuwasemea changamoto zao mbalimbali kila inapojitokeza, ili zifanyiwe kazi na kubadili hali zao.
Kwa upande wake Ndugu Makonda, pamoja na kumshukuru Baba Askofu Dkt. Malasusa kwa ushirikiano wake na utayari wake na viongozi wenzake wa KKKT, muda wote kuendelea kuliombea taifa na Watanzania wote kuendelea kudumisha upendo, amani, utulivu na mshikamano bila kujali tofauti za kiitikadi, pia alitumia fursa hiyo kumpongeza kwa kuchaguliwa kwake kuwa Mkuu wa KKKT, hivyo amemtakia kila la heri katika majukumu yake na kumuahidi ushirikiano wake na Chama Cha Mapinduzi, ambacho amepewa wajibu wa kuwa msemaji wake.
Ziara hiyo ya Ndugu Makonda ofisini kwa Askofu Dkt. Malasusa ni mwendelezo wa ziara zake za kuwatembelea viongozi mbalimbali wa dini na kiroho, kwa ajili ya kwenda kuwasalimia, kujitambulisha na kuwaomba ushirikiano wa kikazi.
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
05-11-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
05-11-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
05-11-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
05-11-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
05-11-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
05-11-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
05-11-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
05-11-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
05-11-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
05-11-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
05-11-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
05-11-2025
TAARIFA KWA UMMA
05-11-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
05-11-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
05-11-2025
MONGELLA AONGOZA MAZISHI YA KADA WA CCM JIJINI MWANZA
05-11-2025
ASIYETII SHERIA, KATIBA NA KUWA TAYARI KUUA KWA MASLAHI BINAFSI HUO NI UGAIDI’
05-11-2025
πππ π¬ππ¦ππ¦ππ§πππ πͺπππ’π πππ ππ¨πππππππͺπ ππͺπ ππ¨πππ‘πππ§ππ π¨πͺπππ’, π¨πππππ‘ππ’ π‘π π¨πππππππ¨, π¬ππππ ππ π πππ¨π‘ππ - πππ. πππ©π¨
05-11-2025
KAENI KIMYA KAMA HAMJUI NCHI ILIKOTOKA - WASIRA
05-11-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amefungua kiwanda cha kutengeneza mabomba ya maji na uchakataji pamba cha MOLI Oil Mills Co. Ltd kilichopo Bariadi Mkoani Simiyu tarehe 16 Juni, 2025.
05-11-2025