MAKONDA AMTEMBELEA ASKOFU DKT MALASUSA, AMHAKIKISHIA VIONGOZI WA KIROHO KUMWOMBEA RAIS SAMIA
Katibu wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (NEC) Taifa, Ndugu Paul Christian Makonda amemtembelea Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Askofu Mkuu Dkt. Alex Gehaz Malasusa, kwa lengo la kumsalimia na kumpongeza kwa kuchaguliwa kwake kuliongoza kanisa hilo, kwa mara nyingine.
Katika mazungumzo yao yaliyofanyika leo Jumamosi, Disemba 2, 2023, Askofu Mkuu Dkt. Malasusa ambaye pia ni Askofu wa KKKT Dayosisi ya Mashariki na Pwani (DMP), amesema viongozi wa dini na kiroho wataendelea kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ili aendelee kuwa na busara, where hekima anapoendelea kuliongoza taifa, kama ambavyo tayari ameonesha uimara, tangu alipobeba dhamana na Mamlaka ya Kiongozi Mkuu wa Nchi.
Mbali ya kumpongeza Ndugu Makonda kwa kuteuliwa kuwa Mkuu wa Idara ya NEC, Uenezi, Itikadi na Mafunzo na kumtakia heri anapotimiza wajibu huo, Baba Askofu Dkt. Malasusa ameongeza nasaha zake kwa kutoa wito kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuendelea kusimamia misingi yake, ikiwemo kuhakikisha Watanzania wote wanatendewa haki, kuwa sikio lao la wananchi wanyonge na kuwasemea changamoto zao mbalimbali kila inapojitokeza, ili zifanyiwe kazi na kubadili hali zao.
Kwa upande wake Ndugu Makonda, pamoja na kumshukuru Baba Askofu Dkt. Malasusa kwa ushirikiano wake na utayari wake na viongozi wenzake wa KKKT, muda wote kuendelea kuliombea taifa na Watanzania wote kuendelea kudumisha upendo, amani, utulivu na mshikamano bila kujali tofauti za kiitikadi, pia alitumia fursa hiyo kumpongeza kwa kuchaguliwa kwake kuwa Mkuu wa KKKT, hivyo amemtakia kila la heri katika majukumu yake na kumuahidi ushirikiano wake na Chama Cha Mapinduzi, ambacho amepewa wajibu wa kuwa msemaji wake.
Ziara hiyo ya Ndugu Makonda ofisini kwa Askofu Dkt. Malasusa ni mwendelezo wa ziara zake za kuwatembelea viongozi mbalimbali wa dini na kiroho, kwa ajili ya kwenda kuwasalimia, kujitambulisha na kuwaomba ushirikiano wa kikazi.
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
05-01-2026
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
05-01-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
05-01-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
05-01-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
05-01-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
05-01-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
05-01-2026
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
05-01-2026
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
05-01-2026
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
05-01-2026
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
05-01-2026
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
05-01-2026
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
05-01-2026
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
05-01-2026
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
05-01-2026
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
05-01-2026
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
05-01-2026
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
05-01-2026
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
05-01-2026
TAARIFA KWA UMMA
05-01-2026