DKT MWINYI AONGOZA SHEREHE ZA MAADHIMISHO YA MIAKA 60 YA MAPINDUZ
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi ameongoza sherehe za maadhimisho ya miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Amesema Miaka 60 ya Mapinduzi ni hatua kubwa katika mshikamano na umoja na kuwasisitiza Watanzania kuendelea kuenzi umoja huo ulioasisiwa na viongozi waliotangulia.
Rais Dkt.Mwinyi amesema hayo katika sherehe za Maadhimisho ya Miaka 60 ya Mapinduzi zilizofanyika uwanja wa Amaan, Mkoa wa Mjini Magharibi tarehe: 12 Januari 2024.
Rais Dkt.Mwinyi amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kushiriki kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Mapinduzi pamoja na shughuli mbalimbali alizopangiwa katika kufanikisha sherehe hizi.
Aidha , Rais Dkt.Mwinyi ametoa shukrani kwa wananchi wote,viongozi mbalimbali wa Serikali, Vyama vya siasa pamoja na Viongozi wakuu wastaafu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ambao wameshiriki katika Maadhimisho hayo.
Vilevile katika kufanikisha sherehe hizo amemshukuru Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe.Masoud Othman na kuipongeza Halmashauri ya Sherehe na Maadhimisho inayoongozwa na Makamu wa Pili wa Rais Mhe.Hemed Suleiman Abdalla kwa kuyaratibu Maadhimisho hayo.
Halikadhalika amewapongeza Makamanda na Wapiganaji wa vikosi vya Ulinzi na Usalama vya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Idara Maalum za SMZ kwa kuonesha hamasa na gwaride la ukakamavu katika sherehe hizo.
Kwa upande mwingine Rais Dkt.Mwinyi ametoa shukrani kwa wageni kutoka nje ya Tanzania wakiwemo Waheshimiwa Mabalozi pamoja na wawakilishi wa mashirika ya kimaendeleo kwa kushiriki sherehe hizo pamoja na viongozi mbalimbali wa Serikali ya SMZ na SMT waliohudhuria.
Hafla hiyo imehudhuriwa na Rais wa Uganda Mhe.Yoweri Museveni, Rais wa Rwanda Mhe.Paul Kagame, Naibu Rais wa Kenya Mhe.Rigathi Gachagua, Waziri Mkuu wa Burundi Mhe.Gervais Ndirakobucha pamoja na Viongozi Wakuu Wastaafu wa Serikali ya SMT na SMZ.
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
09-11-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
09-11-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
09-11-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
09-11-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
09-11-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
09-11-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
09-11-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
09-11-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
09-11-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
09-11-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
09-11-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
09-11-2025
TAARIFA KWA UMMA
09-11-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
09-11-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
09-11-2025
MONGELLA AONGOZA MAZISHI YA KADA WA CCM JIJINI MWANZA
09-11-2025
ASIYETII SHERIA, KATIBA NA KUWA TAYARI KUUA KWA MASLAHI BINAFSI HUO NI UGAIDI’
09-11-2025
πππ π¬ππ¦ππ¦ππ§πππ πͺπππ’π πππ ππ¨πππππππͺπ ππͺπ ππ¨πππ‘πππ§ππ π¨πͺπππ’, π¨πππππ‘ππ’ π‘π π¨πππππππ¨, π¬ππππ ππ π πππ¨π‘ππ - πππ. πππ©π¨
09-11-2025
KAENI KIMYA KAMA HAMJUI NCHI ILIKOTOKA - WASIRA
09-11-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amefungua kiwanda cha kutengeneza mabomba ya maji na uchakataji pamba cha MOLI Oil Mills Co. Ltd kilichopo Bariadi Mkoani Simiyu tarehe 16 Juni, 2025.
09-11-2025