Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Ndugu Hemed Suleiman Abdulla amesema kuna kila sababu ya Jimbo la Mtambwe kubaki katika Ngome ya Chama cha Mapinduzi katika ngazi zote za Uongozi ifikapo Uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.
Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Ndugu Hemed Suleiman Abdulla amesema kuna kila sababu ya Jimbo la Mtambwe kubaki katika Ngome ya Chama cha Mapinduzi katika ngazi zote za Uongozi ifikapo Uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.
Akizungumza na wana CCM na wananchi wa Jimbo la Mtambwe huko katika viwanja vya kisiwani Mhe. Hemed amesema Chama kinahitaji kuimarishwa na kusimamiwa vizuri katika Jimbo hilo kwa kuongeza nguvu za kuwashawishi wananchi wa Mtambwe ili waweze kuendelea kujiunga kwa wingi na CCM.
Ameeleza kuwa Chama Cha Mapinduzi kina dhima kwa wazanzibari kuwatumukia kupitia ahadi walizoweka kama maelekezo ya Ilani ya Uchaguzi inavyoeleza ambapo SMZ chini ya Rais Dkt. Hussein Ali Mwinyi itatatua changamoto zote zinazowakabili wazanzibari.
Amewataka Viongozi wa Mkoa wa Kaskazini Pemba kuendelea kutangaza mazuri yanayofanywa na Chama cha Mapinduzi na kuachana na siasa za chuki na uhasama badala yake washirikiane katika kuinadi Ilani ya Chama Cha Mapinduzi na kuitekeleza kwa vitendo jambo ambalo litatoa wigo mkubwa kwa wananchi wa mtambwe hususan wapinzani wavutiwe na hatimae kujiunga na CCM.
Amewataka Viongozi kuwa na uzalendo wa Nchi yao kwa kuipigania na kuitetea Nchi yao sambamba na kujipanga katika kushinda kwa kishindo katika Jimbo laTambwe na Majimbo yotess ya Zanzibar.
Amesema ili kuleta mabadiliko majimboni ni lazima Viongozi kuwa wabunifu katika kuunda miradi mbali mbali ya maendeleo ambayo itawapatia vijana kujiajiri na kuwaweka pamoja katika kukiimarisha chama.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Kaskazini Pemba Ndg Mberwa Hamad Mberwa ameeleza Mjumbe huyo wa Kamati Kuu kuwa Kamati ya Siasa Mkoa na Wilaya zitahakikisha zinasimamia maelekezo aliyoyatoa na kuyafanyia kazi kwa ngazi zote kuanzia Mkoa hadi Shina
Amemuhakikishia kuwa Mkoa wa Kaskazini Pemba utakuwa ni wa mfano kwa kura nyingi za CCM ukifika Uchaguzi wa Dola wa mwaka 2025 kutokana na utekelezaji mzuri wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM katika Majimbo yote ya Mkoa huo.
Muwakilishi wa Jimbo la Micheweni na Waziri wa Kilimo Maliasili na Mifugo Mhe. Shamata Shaame Khamis ameeleza kuwa Serikali imejenga masoko kila Mkoa ili kurahisisha uuzaji wa biashara zinazotoka mashambani kwa ubora na kwa bei za uhalisia. ss
Nae Mkuu wa Mkoa wa Kaskazi Pemba Salama Mbarouk Khatib amempongeza Mhe.Hemed kwa uamuzi wake wa kufanya ziara ya kukiimarisha chama ambapo wanaamini matunda ya ziara hiyo yataonekana kwani mabadiliko makubwa yenye tija yatatapatikana ndani ya chama cha Mapinduzi na Serikali kwa ujumla.
Ameeleza kuwa wataendelea kufanya ziara mara kwa mara ili kuhakikisha CCM inajengeka na kuendelea kuwa imara na kuingiza wanachama wengi watakaokuja kukipatia Chama hicho ushindi ifikapo mwaka 2025
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
26-05-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
26-05-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
26-05-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
26-05-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
26-05-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
26-05-2026
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
26-05-2026
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
26-05-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
26-05-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
26-05-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
26-05-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
26-05-2026
𝗞𝗜𝗦𝗛𝗜𝗡𝗗𝗢 𝗖𝗛𝗔 𝗗𝗞𝗧. 𝗠𝗜𝗚𝗜𝗥𝗢 𝗖𝗛𝗔𝗣𝗢𝗞𝗘𝗟𝗘𝗪𝗔 𝗞𝗪𝗔 𝗦𝗛𝗔𝗡𝗚𝗪𝗘 𝗗𝗔𝗥 𝗘𝗦 𝗦𝗔𝗟𝗔𝗔𝗠
26-05-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
26-05-2026
𝗩𝗜𝗝𝗔𝗡𝗔 𝗧𝗨𝗜𝗟𝗜𝗡𝗗𝗘 𝗔𝗠𝗔𝗡𝗜 𝗬𝗔 𝗡𝗖𝗛𝗜 𝗬𝗘𝗧𝗨 - 𝗠𝗪𝗘𝗡𝗘𝗭𝗜 𝗞𝗘𝗡𝗔𝗡𝗜
26-05-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
26-05-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
26-05-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
26-05-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
26-05-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
26-05-2026