Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Ndugu Hemed Suleiman Abdulla amesema kuna kila sababu ya Jimbo la Mtambwe kubaki katika Ngome ya Chama cha Mapinduzi katika ngazi zote za Uongozi ifikapo Uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.
Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Ndugu Hemed Suleiman Abdulla amesema kuna kila sababu ya Jimbo la Mtambwe kubaki katika Ngome ya Chama cha Mapinduzi katika ngazi zote za Uongozi ifikapo Uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.
Akizungumza na wana CCM na wananchi wa Jimbo la Mtambwe huko katika viwanja vya kisiwani Mhe. Hemed amesema Chama kinahitaji kuimarishwa na kusimamiwa vizuri katika Jimbo hilo kwa kuongeza nguvu za kuwashawishi wananchi wa Mtambwe ili waweze kuendelea kujiunga kwa wingi na CCM.
Ameeleza kuwa Chama Cha Mapinduzi kina dhima kwa wazanzibari kuwatumukia kupitia ahadi walizoweka kama maelekezo ya Ilani ya Uchaguzi inavyoeleza ambapo SMZ chini ya Rais Dkt. Hussein Ali Mwinyi itatatua changamoto zote zinazowakabili wazanzibari.
Amewataka Viongozi wa Mkoa wa Kaskazini Pemba kuendelea kutangaza mazuri yanayofanywa na Chama cha Mapinduzi na kuachana na siasa za chuki na uhasama badala yake washirikiane katika kuinadi Ilani ya Chama Cha Mapinduzi na kuitekeleza kwa vitendo jambo ambalo litatoa wigo mkubwa kwa wananchi wa mtambwe hususan wapinzani wavutiwe na hatimae kujiunga na CCM.
Amewataka Viongozi kuwa na uzalendo wa Nchi yao kwa kuipigania na kuitetea Nchi yao sambamba na kujipanga katika kushinda kwa kishindo katika Jimbo laTambwe na Majimbo yotess ya Zanzibar.
Amesema ili kuleta mabadiliko majimboni ni lazima Viongozi kuwa wabunifu katika kuunda miradi mbali mbali ya maendeleo ambayo itawapatia vijana kujiajiri na kuwaweka pamoja katika kukiimarisha chama.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Kaskazini Pemba Ndg Mberwa Hamad Mberwa ameeleza Mjumbe huyo wa Kamati Kuu kuwa Kamati ya Siasa Mkoa na Wilaya zitahakikisha zinasimamia maelekezo aliyoyatoa na kuyafanyia kazi kwa ngazi zote kuanzia Mkoa hadi Shina
Amemuhakikishia kuwa Mkoa wa Kaskazini Pemba utakuwa ni wa mfano kwa kura nyingi za CCM ukifika Uchaguzi wa Dola wa mwaka 2025 kutokana na utekelezaji mzuri wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM katika Majimbo yote ya Mkoa huo.
Muwakilishi wa Jimbo la Micheweni na Waziri wa Kilimo Maliasili na Mifugo Mhe. Shamata Shaame Khamis ameeleza kuwa Serikali imejenga masoko kila Mkoa ili kurahisisha uuzaji wa biashara zinazotoka mashambani kwa ubora na kwa bei za uhalisia. ss
Nae Mkuu wa Mkoa wa Kaskazi Pemba Salama Mbarouk Khatib amempongeza Mhe.Hemed kwa uamuzi wake wa kufanya ziara ya kukiimarisha chama ambapo wanaamini matunda ya ziara hiyo yataonekana kwani mabadiliko makubwa yenye tija yatatapatikana ndani ya chama cha Mapinduzi na Serikali kwa ujumla.
Ameeleza kuwa wataendelea kufanya ziara mara kwa mara ili kuhakikisha CCM inajengeka na kuendelea kuwa imara na kuingiza wanachama wengi watakaokuja kukipatia Chama hicho ushindi ifikapo mwaka 2025
𝐍𝐈 𝐍𝐙𝐀𝐌𝐔 𝐘𝐀 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐍𝐘𝐀𝐑𝐀!
01-06-2026
🔰𝐀𝐒𝐀𝐍𝐓𝐄𝐍𝐈 𝐒𝐀𝐍𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎!
01-06-2026
𝐒𝐇𝐔𝐋𝐄 𝐘𝐀 𝐌𝐒𝐈𝐍𝐆𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐒𝐀𝐃𝐀𝐋𝐀 𝐘𝐀𝐎𝐍𝐃𝐎𝐀 𝐊𝐄𝐑𝐎 𝐘𝐀 𝐊𝐔𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐀 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐌𝐄𝐓𝐀 𝟏𝟐 𝐊𝐖𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐈
01-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐀𝐀𝐍𝐙𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀𝐍𝐈 𝐇𝐀𝐈, 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
01-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐀𝐀𝐍𝐙𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐇𝐀𝐈 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
01-06-2026
𝐍𝐈 𝐌𝐔𝐃𝐀 𝐖𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐇𝐀𝐈-𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎 𝐒𝐀𝐒𝐀
01-06-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐌𝐏𝐀 𝐁𝐀𝐉𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐒𝐈𝐇𝐀 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐘𝐄 𝐔𝐋𝐄𝐌𝐀𝐕𝐔 𝐖𝐀 𝐌𝐈𝐆𝐔𝐔
01-06-2026
MAWENZI YAVUNJA REKODI: MITUNGI 3,313 YA OKSIJENI YAZALISHWA KWA MIEZI 6, ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 126 ZAOKOLEWA!
01-06-2026
MAFURIKO YA WANANCHI WA SIHA KWENYE MKUTANO MKUBWA WA HADHARA
01-06-2026
MAPOKEZI YA KATIBU MWENEZI WA CCM NDUGU KENANI L KIHONGOSI MKOANI KILIMANJARO
01-06-2026
🔰 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐒𝐇𝐈𝐍𝐃𝐎 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
01-06-2026
CCM INAWATAKIA HERI YA SIKUKUU YA EID AL ADHA
01-06-2026
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
01-06-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
01-06-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
01-06-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
01-06-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
01-06-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
01-06-2026
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
01-06-2026
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
01-06-2026