Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Alhajj Hemed Suleiman Abdulla amesema Mashindano ya Kuhifadhisha Qur-an yana mchango mkubwa katika kuwajenga vijana kimaadili, kifkra na kinidhamu pamoja na kumjua Allah (S.W) na sifa zake
Ameyasema hayo katika uzinduzi wa mashindano ya Kimataifa ya Qur-an Tukufu uliofanyika katika Ukumbi wa Madinatul Bahar Bweni jijini Zanzibar.
Amesema kuwepo kwa Mashindano ya Qur-an yanawasaidia vijana kujitenga na matendo maovu na macahfu kwa vile hutumia muda mwingi wa kusoma na kujiandaa kushiriki katika mashindano mbali mbali ndani ya nchi na nje ya nchi.
Alhajj Hemed amesema endapo vijana hawatowekewa misingi imara ya kitabia na kuifahamu dini yao watakuwa rahisi kufuata tamaduni za kigeni ambazo zinakwenda kinyumae na mila, silka na desturi za Kizanzibari.
Sambamba na hayo ameikumbusha jamii kuwa kila mmoja ana jukumu la kuhimiza na kusimamia maadili mema kuanzia ngazi ya familia, mashule, madrasa na maeneo ya Ibada ambapo kufanya hivyo kutawasaidia vijana na vizazi vijavyo kuishi katika mazingira ya kumcha Mungu.
Amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inatambua kazi kubwa na nzuri inayofanywa na ZBC na Ofisi ya Mufti katika kujenga jamii yenye maadili mame, hivyo Serikali itaendelea kuunga mkono harakati za kidini ambazo dhamira yake ni kuiendeleza dini ya kiislamu na kuimarisha maadili mema ambayo ni nguzo kwa jamii katika kudumisha amani na umoja uliopo.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa ZBC Bwana RAMADHAN BUKINI ameishukuru Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inayoongozwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la mapinduzi Alhajj Dkt. Hussein Ali Mwinyi kwa kuridhia na kusaidia kufanyika kwa mashindano hayo jambo ambalo linadhihirisha mapenzi ya viongozi kwa wananchi wake.
Bukini ameeleza kuwa lengo la mashindano hayo ni kuunganisha pamoja Umma wa kiislamu katika mambo ya kheri, kuwaandaa vijana kiroho na kuitambua dini yao sambamba na kupunguza mmong'onyoko wa maadili katika jamii zetu.
Nao wadau wa kuhifadhisha Qur- an wakiongozwa na SHEIKH OTHMAN MAALIM wamewataka waumini wa dini ya kiislam kulipa umuhimu suala la kuhifadhi Qur-an tukufu kwa viajna wao sambamba na kuisoma kwa wingi hasa katika mwezi mtukufu wa Ramadhan jambo ambalo linamkurubisha mja na mola wake.
Wamesema mikusanyiko ya kuhifadhisha Qur-an inasaidia kuwabadilisha vijana na jamii kwa ujumla katika kuitambua dini yao ambapo amewaomba viongozi kwa nafasi zao kuunga mkono juhudi zinazofanywa na taasi za Dini kwa maslahi mapana ya Taifa.
Aidha wamewataka watu wenye uwezo kuweza kuzisaidia kwa hali na mali taasisi zenye kuhifadhisha Qur-an kwani kufanya hivyo watapata ujira mkubwa kutoka kwa Allah (S.W) sambamba na kuwataka wafanya biashara kuacha tabia ya kupandisha bei za vyakula hasa katika mwezi wa Ramadhani kwa kutarajia faida mara dufu jambo ambalo ni kinyume na maagizo ya Dini ya kiislamu na Serikali kwa ujumla.
Mashindano hayo yaliyoandaliwa na Ofisi ya Mufti kwa kushirikiana na Shirika la Utangazaji Zanzibar na Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar yanatarajiwa kufanyika tarehe 30.03.2024 katika Uwanja wa Amaani Complex Zanzibar na jumla ya Nchi nane (8) zinatarajiwa kushiriki ktk mashindano hayo.
🔰𝐀𝐒𝐀𝐍𝐓𝐄𝐍𝐈 𝐒𝐀𝐍𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎!
01-06-2026
𝐒𝐇𝐔𝐋𝐄 𝐘𝐀 𝐌𝐒𝐈𝐍𝐆𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐒𝐀𝐃𝐀𝐋𝐀 𝐘𝐀𝐎𝐍𝐃𝐎𝐀 𝐊𝐄𝐑𝐎 𝐘𝐀 𝐊𝐔𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐀 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐌𝐄𝐓𝐀 𝟏𝟐 𝐊𝐖𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐈
01-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐀𝐀𝐍𝐙𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀𝐍𝐈 𝐇𝐀𝐈, 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
01-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐀𝐀𝐍𝐙𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐇𝐀𝐈 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
01-06-2026
𝐍𝐈 𝐌𝐔𝐃𝐀 𝐖𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐇𝐀𝐈-𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎 𝐒𝐀𝐒𝐀
01-06-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐌𝐏𝐀 𝐁𝐀𝐉𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐒𝐈𝐇𝐀 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐘𝐄 𝐔𝐋𝐄𝐌𝐀𝐕𝐔 𝐖𝐀 𝐌𝐈𝐆𝐔𝐔
01-06-2026
MAWENZI YAVUNJA REKODI: MITUNGI 3,313 YA OKSIJENI YAZALISHWA KWA MIEZI 6, ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 126 ZAOKOLEWA!
01-06-2026
MAFURIKO YA WANANCHI WA SIHA KWENYE MKUTANO MKUBWA WA HADHARA
01-06-2026
MAPOKEZI YA KATIBU MWENEZI WA CCM NDUGU KENANI L KIHONGOSI MKOANI KILIMANJARO
01-06-2026
🔰 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐒𝐇𝐈𝐍𝐃𝐎 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
01-06-2026
CCM INAWATAKIA HERI YA SIKUKUU YA EID AL ADHA
01-06-2026
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
01-06-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
01-06-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
01-06-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
01-06-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
01-06-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
01-06-2026
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
01-06-2026
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
01-06-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
01-06-2026