Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Alhajj Hemed Suleiman Abdulla amesema Mashindano ya Kuhifadhisha Qur-an yana mchango mkubwa katika kuwajenga vijana kimaadili, kifkra na kinidhamu pamoja na kumjua Allah (S.W) na sifa zake
Ameyasema hayo katika uzinduzi wa mashindano ya Kimataifa ya Qur-an Tukufu uliofanyika katika Ukumbi wa Madinatul Bahar Bweni jijini Zanzibar.
Amesema kuwepo kwa Mashindano ya Qur-an yanawasaidia vijana kujitenga na matendo maovu na macahfu kwa vile hutumia muda mwingi wa kusoma na kujiandaa kushiriki katika mashindano mbali mbali ndani ya nchi na nje ya nchi.
Alhajj Hemed amesema endapo vijana hawatowekewa misingi imara ya kitabia na kuifahamu dini yao watakuwa rahisi kufuata tamaduni za kigeni ambazo zinakwenda kinyumae na mila, silka na desturi za Kizanzibari.
Sambamba na hayo ameikumbusha jamii kuwa kila mmoja ana jukumu la kuhimiza na kusimamia maadili mema kuanzia ngazi ya familia, mashule, madrasa na maeneo ya Ibada ambapo kufanya hivyo kutawasaidia vijana na vizazi vijavyo kuishi katika mazingira ya kumcha Mungu.
Amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inatambua kazi kubwa na nzuri inayofanywa na ZBC na Ofisi ya Mufti katika kujenga jamii yenye maadili mame, hivyo Serikali itaendelea kuunga mkono harakati za kidini ambazo dhamira yake ni kuiendeleza dini ya kiislamu na kuimarisha maadili mema ambayo ni nguzo kwa jamii katika kudumisha amani na umoja uliopo.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa ZBC Bwana RAMADHAN BUKINI ameishukuru Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inayoongozwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la mapinduzi Alhajj Dkt. Hussein Ali Mwinyi kwa kuridhia na kusaidia kufanyika kwa mashindano hayo jambo ambalo linadhihirisha mapenzi ya viongozi kwa wananchi wake.
Bukini ameeleza kuwa lengo la mashindano hayo ni kuunganisha pamoja Umma wa kiislamu katika mambo ya kheri, kuwaandaa vijana kiroho na kuitambua dini yao sambamba na kupunguza mmong'onyoko wa maadili katika jamii zetu.
Nao wadau wa kuhifadhisha Qur- an wakiongozwa na SHEIKH OTHMAN MAALIM wamewataka waumini wa dini ya kiislam kulipa umuhimu suala la kuhifadhi Qur-an tukufu kwa viajna wao sambamba na kuisoma kwa wingi hasa katika mwezi mtukufu wa Ramadhan jambo ambalo linamkurubisha mja na mola wake.
Wamesema mikusanyiko ya kuhifadhisha Qur-an inasaidia kuwabadilisha vijana na jamii kwa ujumla katika kuitambua dini yao ambapo amewaomba viongozi kwa nafasi zao kuunga mkono juhudi zinazofanywa na taasi za Dini kwa maslahi mapana ya Taifa.
Aidha wamewataka watu wenye uwezo kuweza kuzisaidia kwa hali na mali taasisi zenye kuhifadhisha Qur-an kwani kufanya hivyo watapata ujira mkubwa kutoka kwa Allah (S.W) sambamba na kuwataka wafanya biashara kuacha tabia ya kupandisha bei za vyakula hasa katika mwezi wa Ramadhani kwa kutarajia faida mara dufu jambo ambalo ni kinyume na maagizo ya Dini ya kiislamu na Serikali kwa ujumla.
Mashindano hayo yaliyoandaliwa na Ofisi ya Mufti kwa kushirikiana na Shirika la Utangazaji Zanzibar na Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar yanatarajiwa kufanyika tarehe 30.03.2024 katika Uwanja wa Amaani Complex Zanzibar na jumla ya Nchi nane (8) zinatarajiwa kushiriki ktk mashindano hayo.
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
02-01-2026
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
02-01-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
02-01-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
02-01-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
02-01-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
02-01-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
02-01-2026
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
02-01-2026
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
02-01-2026
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
02-01-2026
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
02-01-2026
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
02-01-2026
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
02-01-2026
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
02-01-2026
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
02-01-2026
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
02-01-2026
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
02-01-2026
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
02-01-2026
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
02-01-2026
TAARIFA KWA UMMA
02-01-2026