TUNA MTAJI WA IMANI YA WATANZANIA: NCHIMBI
Azindua kampeni Mwanza akitamba na takwimu za kura za uhakika
Awasihi wanaCCM kila mmoja kutafuta kura 10 kwa ajili ya ushindi wa kishindo
Ahamasisha kampeni za nyumba kwa nyumba na mtu kwa mtu, isiachwe kura hata moja, wakiwemo wapinzani
Awataka washindi kuwatumikia Watanzania kwa kupinga dhuluma na rushwa
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, amesema CCM inaingia kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa kikiwa na imani kubwa ya Watanzania kutokana na uimara wa chama na uongozi wa Mwenyekiti wake, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Amesema kuwa uimara wa CCM unatokana na wingi na umakini wa wanachama wake, akitoa takwimu jinsi wanachama wapatao milioni 8 wa CCM walivyojitokeza kupiga kura wakati wa mchakato wa ndani ya chama hicho kupata wagombea wa nafasi mbalimbali kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.
Balozi Nchimbi amesema mtaji wa imani ya Watanzania, utumishi wa CCM kupitia sera zake, na uongozi makini unakipatia chama hicho uhakika wa ushindi mkubwa wa kishindo katika uchaguzi huo unaotarajiwa kufanyika tarehe 27 Novemba 2024.
Katibu Mkuu huyo wa CCM aliyasema hayo alipokuwa akihutubia mkutano mkubwa wa hadhara wa uzinduzi wa kampeni za CCM kwa ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa Mkoa wa Mwanza, uliofanyika katika Viwanja vya Furahisha, jijini Mwanza, leo tarehe 27 Novemba 2024.
Katika kujihakikishia ushindi huo wa kishindo, Balozi Nchimbi alisisitiza kampeni za kuomba kura ziwalenge hata wanachama na viongozi wa vyama vya upinzani, ili kuhakikisha kila kura inapatikana kwa ajili ya CCM, akiwahamasisha kupiga kampeni “nyumba kwa nyumba na mtu kwa mtu” nchi nzima.
“Pamoja na uhakika wa kura, msiridhike na ushindi. Twendeni nyumba kwa nyumba na mtu kwa mtu. Tusiache kura hata moja. Kila mwanachama atafute kura 10. Hata wa vyama vya upinzani, wawe ACT, NCCR, Chadema, na wote, watatupigia kura. Tumalizeni huu mchezo kwa kuipatia CCM ushindi mkubwa wa kishindo.
“Wajibu wetu ni kuwakumbusha tu Watanzania kazi kubwa ambayo CCM imeendelea kufanya katika kutoa uongozi wa nchi hii. Uhakika wa kesho ya Tanzania uko CCM. Watanzania wana imani kubwa na CCM kila wanapofikiria maendeleo, umoja wa nchi yetu, utaifa wetu, amani na utulivu. Tunataka wagombea wetu mtakapochaguliwa mkalinde heshima na imani hii ya Watanzania kwa kuwatumikia vizuri, mkijiepusha na dhuluma na rushwa,” alisema Balozi Nchimbi.
Aidha, akisisitiza kuhusu uimara wa CCM, Balozi Nchimbi alisema CCM ndiyo chama pekee ambacho wanachama wake, kwa mamilioni, walijitokeza kushiriki mchakato wa ndani wa kupata wagombea, hasa kupitia kura za maoni. Hii ndiyo sababu kimesimamisha wagombea maeneo yote nchi nzima katika uchaguzi huo, kwa kuwa kimeenea nchi nzima, tofauti na vyama vingine vya upinzani.
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
09-12-2025
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
09-12-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
09-12-2025
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
09-12-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
09-12-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
09-12-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
09-12-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
09-12-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
09-12-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
09-12-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
09-12-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
09-12-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
09-12-2025
TAARIFA KWA UMMA
09-12-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
09-12-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
09-12-2025