MWENYEKITI WA UMOJA WA VIJANA WA CHAMA CHA MAPINDUZI (UVCCM) TAIFA, MOHAMED ALI MOHAMED (KAWAIDA), AWATAKA VIJANA KUWALINDA VIONGOZI WAO KWA VITENDO
MWENYEKITI wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Mohamed Ali Mohamed (Kawaida), amesema vijana wa Chama hicho haitoshi kulinda Viongozi wao kwa maneno badala yake wajielekeze katika vitendo vinavyobeba dhamira, mikakati na ujasiri wa kuleta ufanisi ndani ya Chama na Jumuiya zake.
Kauli hiyo ameitoa katika ufungaji wa mafunzo elekezi ya Viongozi wa UVCCM Mkoa wa Kusini Unguja,yaliyofanyika katika Chuo cha Mafunzo na Uongozi kilichopo Tunguu Zanzibar.
Alisema kuwa Vijana wa UVCCM wamatakiwa kuwa imara wakati wote kwani ndio wenye dhamana kubwa ya kulinda kwa gharama yoyote maslahi ya Chama na Jumuiya zake pamoja na Viongozi wake.
Katika maelezo yake Mwenyekiti huyo MCC Mohamed Kawaida, alisema historia inaonyesha kuwa Umoja huo ndio chimbuko la kuwaandaa Viongozi bora nchini walioiva kimaarifa,kiujuzi,kimaadili, uaminifu, wachapakazi na wenye uzalendo wa kweli.
"Haitoshi kusema, kuimba na kuwasifu tu Viongozi wetu badala yake tuonyeshe misimamo, dhamira, utetezi na ulinzi wetu kwa vitendo na hoja imara zinazoendana mahitaji ya siasa za Sasa. ", alisema Mwenyekiti huyo Mohamed Kawaida.
Mohamed, aliwasihi washiriki wa mafunzo hayo kutumia mbunu, maelekezo na nasaha walizopewa kuleta Mabadiliko chanya katika maeneo yao ya kiutendaji.
Pamoja na hayo alikwambia washiriki hao wa mafunzo kuwa Mwenyekiti wa CCM Taifa ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, kuwa ameendelea kufanya kazi kubwa ya kufungua milango ya uwekezaji inayotoa fursa za ajira kwa vijana wa rika na fani mbalimbali nchini.
Kupitia hafla hiyo aliwasihi Vijana mbalimbali nchini kujipanga vizuri ili waweze kujitokeza kwa wingi kugombea nafasi mbalimbali za Uongozi katika Uchaguzi Mkuu ujao wa Mwaka 2025.
Naye Naibu Katibu Mkuu wa UVCCM Zanzibar ambaye pia ni Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja huo Mussa Haji Mussa, alipongeza washiriki wa mafunzo hayo kwa nidhamu na juhudi zao katika kufuatilia mada zilizotolewa katika mafunzo.
Akisoma risala Katibu wa UVCCM Mkoa wa Kusini Unguja Mohamed Ali Mohamed, alisema mafunzo hayo ya siku tatu ya kuwajengea uwezo vijana wa UVCCM Mkoa wa Kusini Unguja yamefanyika kwa ufanisi mkubwa.
Alisema katika mafunzo hayo zimetolewa mada mbalimbali zikiwemo Historia ya CCM na Jumuiya zake, muundo wa CCM na Jumuiya zake, mipaka na majukumu ya Viongozi wa CCM na Jumuiya zake, Historia ya Mapinduzi ya Zanzibar na Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Kupitia risala hiyo wamewapongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan, kwa juhudi zake za kuimarisha Uchumi kupitia mradi wa uwekezaji katika Bandari Dar es salaam utakaotekelezwa na Kampuni ya DP World kutoka Dubai.
Jumla ya Vijana Jumla 207 wanaume 124 wanawake 83 wa UVCCM Mkoa wa Kusini Unguja wamehitimu mafunzo hayo elekezi na kutunukiwa vyeti
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
06-02-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
06-02-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
06-02-2026
πππ¦πππ‘ππ’ πππ πππ§. π ππππ₯π’ ππππ£π’πππππͺπ ππͺπ π¦πππ‘ππͺπ πππ₯ ππ¦ π¦πππππ
06-02-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
06-02-2026
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
06-02-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
06-02-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
06-02-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
06-02-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
06-02-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
06-02-2026
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
06-02-2026
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
06-02-2026
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
06-02-2026
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
06-02-2026
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
06-02-2026
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
06-02-2026
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
06-02-2026
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
06-02-2026
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
06-02-2026