CCM ISIHUSISHWE NA VURUGU ZA IGUNGA, CHADEMA IJITAFAKARI
KILIMANJARO: Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimeeleza kuwa hakihusiki na tukio la kuvamiwa kwa mkutano wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) uliokuwa ukifanyika Igunga hapo jana, kwani hawana sababu zozote za kushiriki tukio hilo.
Makalla ameeleza hayo leo Juni 10, 2025 wakati akizungumza na wannachi katika eneo la Himo Wilaya ya Mosho Vijinini mkoani Moshi akiendelea na ziara yake katika mikoa ya Kanda ya Kaskazini.
Makalla ameeleza hayo akijibu kilichoandikwa na Makama Mwenyekiti wa Chadema, John Heche kupitia katika mtandao wa kijamii wa X kuwa mkutano wao wamefanyiwa vurugu na vijana wa CCM, hivyo Makalla amesema wasihusishwe na tukio hilo kwani ni la kitoto.
“Leo walikuwa Igunga mkutano nafikiri wamefanyiwa vuruga nafizkiri na nyie mmeona kwenye vyombo vya habari lakini bila busara Makamu wao Mwenyekiti John Heche ameandika kwamba mkutano wetu vurugu hizi tumefanyiwa na vijana wa Chama Cha Mapinduzi,” amesema Makalla.
Pia Makalla amesema Chadema sio mshindani tena wa CCM kwa sababu wao hawashiriki uchaguzi, hivyo CCM haiwezi kuwa na maslahi yoyote na mkutano huo.
Makalla amewataka Chadema wafanye tafakuri ndani ya chama chao wasikimbilie kusema ni CCM badala yake wajitafakari.
Pia amesema CCM wanayokazi wanayoiendea ambayo ni kushiriki uchaguzi na kushinda kwa kishindo, hivyo wajitafakari wamalize migogoro yao binafsi ya ndani ya chama na kuacha kuwahusisha na tukio hilo.