SERIKLI ya Mapinduzi ya Zanzibar, imesema itaendelea kutenga bajeti ya
mikopo kuwasaidia vijana wanaokosa fursa ya kujiunga na elimu ya juu
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, ameyasema hayo kwenye maadhimisho ya siku ya vijana kimataifa, viwanja vya Maisara Suleiman Wilaya ya Mjini, Mkoa wa Mjini Magharibi.
Alisema, Serikali imejipanga kufanikisha lengo lake hilo licha ya ongezeko la kila mwaka la vijana wanaopata sifa za kujiunga na elimu ya juu.
Alisema, Serikali imechukua jitihada mbali mbali kuimarisha ustawi wa vijana kwa kuwashirikisha kwenye sekta zote za Maendeleo ikiwemo Afya, Elimu, Kilimo, Uvuvi, TEHAMA, Ujasiriamali na michezo kwa kuwawesha kujiajiri na kuajiriwa.
Aidha, Dk. Mwinyi alieleza Serikali za SMZ na SMT zimeweka utaratibu maalum wa ajira, chini ya Sheria ya Utumishi wa Umma nambari 2/2008 ambayo imetoa asilimia 21% ya Ajira kwa Vijana wa Zanzibar kwenye Sekta za Muungano.
Alisema, kwa mujibu wa taarifa ya muelekeo wa Kiuchumi ya mwaka 2022 kupitia miradi ya fedha za ahueni za UVIKO 19, jumla ya vijana 13,870 walifanikiwa kupata ajira za muda kupitia miradi iliyowekezwa na Serikali kupitia sekta mbalimbali za maendeleo.
Alieleza, mbali na jitihada za kuanzisha Wizara na Idara Maalum ya kushughulikia Maendeleo ya Vijana ili kuimarisha usimamizi na uratibu wa shughuli za Maendeleo yao nchini pia Serikali imeanzisha Sera ya Maendeleo ya Vijana ya Mwaka 2005 iliyoweka miongozo ya shughuli zote za Maendeleo na Ustawi wao.
Akiizungumzia maendeleo ya sekta ya Afya kwa vijana, Rais Dk. Mwinyi alisema Serikali kupitia Wizara ya Afya imekua ikishirikiana na wadau wa maendeleo wakiwemo shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya watu ulimwengu (UNFPA) kwa pamoja wameanzisha na kuviendeleza vituo 13 vya huduma rafiki za Afya kwa Vijana kwa wilaya zote za Unguja na Pemba.
Pia, alieleza juhudi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ilivyoanza mradi wa ujenzi wa Vituo vya mafunzo ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) kwa Vijana kwa Unguja na Pemba ambavyo vitachochea maendeleo yao kwa kuitumia taaluma watakayoipata, ikiwemo kwenda sambamba na Ulimwengu wa Sayansi na Teknolojia.
Hata hivyo, Rais Dk. Mwinyi aliahidi kuanzishwa Sera mpya ya Maendeleo ya Vijana itakayozingatia mahitaji ya wakati wa sasa na ujao, alitoa wito kwa taasisi zote za Umma na binafsi, Washirika wa Maendeleo, Mabaraza ya Vijana, na Asasi za Maendeleo ya Vijana, kushiriki kikamilifu kwenye utekelezaji wa Sera hiyo kwa vitendo ili kufikia lengo lililokusudiwa na Serikali.
Akizungumza kwenye hafla hiyo, Waziri wa Habari, Vijana Utamaduni na Michezo, Tabia Maulid Mwita aliiahidi Serikali kuendeleza fursa kwa vijana, kuwasimamia, kuratibu na kupunguza changamoto zinazowakabili.
Naye, Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi, (UVCCM) Muhamed Kawaida, alipongeza juhudi za Serikali ya Dk.
Mwinyi kwa mara ya kwanza amefanikiwa kuwaweka pamoja vijana wa vyama vya mbalimbali bila kujali tofauti za itikadi zao na kueleza kuwa hatua hiyo imeendelea kuimarisha amani ya Zanzibar iliyopo.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Baraza la Vijana, Yunus Juma Ali aliwaasa vijana kuendeleza heshima kwenye jamii, kuvumiliana na kuyasema mambo yenye uhakika kwa kufanyia utafiti na kujiridhisha kabla ya kuzungumza.
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
09-12-2025
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
09-12-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
09-12-2025
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
09-12-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
09-12-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
09-12-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
09-12-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
09-12-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
09-12-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
09-12-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
09-12-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
09-12-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
09-12-2025
TAARIFA KWA UMMA
09-12-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
09-12-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
09-12-2025