Utekelezaji mzuri wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi ndio kunakowavutia wananchi na wapinzani kujiunga kwa wingi na CCM ili kuzidi kukiunga mkono chama hicho.
Utekelezaji mzuri wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi ndio kunakowavutia wananchi na wapinzani kujiunga kwa wingi na Chama Chama Cha Mapinduzi ili kuzidi kukiunga mkono chama hicho.
Akikabdhi kadi za CCM kwa wanachama wapya Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Ndugu Hemed Suleiman Abdulla amewataka viongozi na watendaji wote wa CCM kuhakikisha wanatengeneza mazingira mazuri ya kukiimarisha chama, kuwaweka wanachama pamoja na kuachana na makundi ndani ya chama ambapo kufanya hivyo kutasaidia idadi ya wanachama kuongezeka na CCM kupata ushindi katika ngazi zote ifikapo mwaka 2025.
Mhe Hemed ambae pia ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amesema sifa kuu ya kiongozi bora ni kusimamia haki na usawa kwa anaowaongoza sambamba na kutatua changamoto zinazojitokeza majimboni mwao.
Aidha ameeleza kuwa Amani na utulivu ndio nguzo kubwa ya maendeleo nchini ambapo katiba ya CCM imemtaka kila mwana CCM na mtanzania kusimamia jambo hilo.
Amesisistiza suala la kulipa ada kwa wanachama ni la lazima na wasisubiri hadi wakati wa uchaguzi ndio wakalipia ada ama kulipiwa na viongozi wao wa majimbo kwani kufanya hivyo ni kuzorotesha utendaji kazi wa chama.
Mhe. Makamu amesema lazima Viongozi wa CCM wakiimarishe Chama kwa kuwaelelza wanachama juu ya umuhimu wa kulipa ada, mahusiano mema na umoja na mshikamano ndani ya chama.
Mjumbe huyo wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Amewataka viongozi kuwasimamia vijana waliofikisha umri wa miaka 18 kusajiliwa na kupatiwa kitambulisho cha Mzanzibari Mkaazi kitakachowasaidia katika shughuli mbali mbali ikiwa ni pamoja na kujiandikosha katika daftari la kupigia kura.
Ameahidi kuwa Serikali zote mbili chini ya Uongozi wa Dkt. Samia Suluhu Hassan na Dkt. Hussen Ali Mwinyi zimejiwekea utaratibu wa kupokea maoni na ushauri kutoka kwa wananchi pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili na kuahidi kuwa Serikali zitasimamia changamoto hizo ili wananchi waishi bila ya usumbufu wowote.
Akizungumza kwa niaba ya wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Sufiani Khamis amemuahidi Mhe. Hemed kuwa majimbo yote ya Zanzibar yatachukuliwa na Chama Cha Mapinduzi pasipo wapinzani kuchukua hata jimbo moja.
Nae mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mjini Kichama Talib Ali Talib amesema nguvu ya upinzani ni ndogo sana katika Majimbo ya Jang'ombe na Malindi na ndio mana katika Jimbo la Jang'ombe hakuna bendera hata moja ya chama cha upinzani inayopepea na haitapepea kamwe.
Kwa upande wao viongozi wa Majimbo ya Jang'ombe na Malindi wamesema katika kutekeleza Ilani ya CCM kwa vitendo miradi mbali mbali ya maendeleo imetekelezwa na mengine inaendelea kutekelezwa jambo ambalo linakifanya chama cha Mapinduzi kuzidi kukubalika hadi na wapinzani ambao kwa wingi wameshajiunga na CCM.
Wamesema hadi sasa tayari asilimia kubwa ya utekelezaji wa Ilani ya CCM umeshatekelezwa hivyo ni dhahiri kuwa Chama Cha Mapinduzi kitachukua ushindi mkubwa ifikapo mwaka 2025.
Nao wananchi wa majimbo hayo wampongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi kwa mapenzi yake kwa wazanzibari kwa kuwasogezea huduma mbali mbali karibu na maeneo yao hatua ambayo inawazidishia Imani kwa Chama Cha Mapinduzi.
Katika ziara yake hiyo ya kukiimarisha Chama na Jumuiya zake Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla ametembelea Jimbo la Jang’ombe na Jimbo la Malindi na amekagua miradi mbali mbali ya uwekezji, ameweka mawe ya msingi na kumeshiriki katika ujenzi wa maskani zinazojengwa katika Majimbo hayo.
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
09-12-2025
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
09-12-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
09-12-2025
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
09-12-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
09-12-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
09-12-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
09-12-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
09-12-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
09-12-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
09-12-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
09-12-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
09-12-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
09-12-2025
TAARIFA KWA UMMA
09-12-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
09-12-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
09-12-2025