SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar imesema inahitaji uwekezaji mkubwa katika sekta ya Maji na Umeme ili kuongeza ufanisi wa hali ya juu wa huduma ya uhakika kwenye sekta hizo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi ameyasema hayo alipozungumza na uongozi wa Kampuni ya “WAPCOS Limited” ya nchini India, uliofika Ikulu Zanzibar.
Dk. Mwinyi amesema hadi sasa Zanzibar inapokea megawati 110 za nishati ya umeme, ambao pia inapata msaada kutoka Tanzania Bara, hivyo alisema, Serikali inadhamira ya kuzalisha umeme wake mwenyewe na iko tayari kushirikiana na kampuni yoyote itakayokuwa tayari ili kuanza hatua za upembuzi yakinifu.
Pia, Rais Dk. Mwinyi amesema Zanzibar inahitaji utafiti wa kina wa uzalishaji, usafirishaji na usambazaji wa nishati hizo kwa kuangalia zaidi uwekezaji na huduma za uhakika.
Dk. Mwinyi ameikaribisha kampuni ya “WAPCOS Limited” endapo inavutika kufanya kazi na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inakaribishwa.
Alisema, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na ya India ni wadau wakubwa kwenye huduma za jamii na imekua ikishirikiana kwenye nyanja mablimbali za Maendeleo ikiwemo elimu.
Akizungumza kwenye hafla hiyo, Mwenyekiti na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya “WAPCOS Limited, Rajni Kant Agrawal amesema kampuni yao imejika zaidi na kutoa huduma za ushauri hasa kwenye nishari za umeme, maji na miundombini na kueleza kuwa wako tayari kusirikiana na Serikali kwenye uwekezaji wa sekta hizo.
Alisema, kwa Tanzania tayari kampuni hiyo inafanyakazi maeneo ya Dar es Salaam, Bagamoyo na maeneo mengine ya nchi ikiwemo Zanzibar.
Kampuni ya “WAPCOS Limited” yenye makao makuu yake mjini New Delhi, India ni watoa huduma za ushauri kwa nyanja za rasilimali maji, nishati na miundombinu. Ilizinduliwa rasmi June 26, mwaka 1969, mjini New Delhi.
Ni kampuni yenye miradi kadhaa kote India, Asia na Afrika, iko chini ya umiliki wa Serikali ya India kwa usimamizi wa Wizara ya Jal Shakti nchini humo.
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐌𝐏𝐀 𝐁𝐀𝐉𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐒𝐈𝐇𝐀 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐘𝐄 𝐔𝐋𝐄𝐌𝐀𝐕𝐔 𝐖𝐀 𝐌𝐈𝐆𝐔𝐔
30-05-2026
MAWENZI YAVUNJA REKODI: MITUNGI 3,313 YA OKSIJENI YAZALISHWA KWA MIEZI 6, ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 126 ZAOKOLEWA!
30-05-2026
MAFURIKO YA WANANCHI WA SIHA KWENYE MKUTANO MKUBWA WA HADHARA
30-05-2026
MAPOKEZI YA KATIBU MWENEZI WA CCM NDUGU KENANI L KIHONGOSI MKOANI KILIMANJARO
30-05-2026
🔰 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐒𝐇𝐈𝐍𝐃𝐎 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
30-05-2026
CCM INAWATAKIA HERI YA SIKUKUU YA EID AL ADHA
30-05-2026
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
30-05-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
30-05-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
30-05-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
30-05-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
30-05-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
30-05-2026
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
30-05-2026
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
30-05-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
30-05-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
30-05-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
30-05-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
30-05-2026
𝗞𝗜𝗦𝗛𝗜𝗡𝗗𝗢 𝗖𝗛𝗔 𝗗𝗞𝗧. 𝗠𝗜𝗚𝗜𝗥𝗢 𝗖𝗛𝗔𝗣𝗢𝗞𝗘𝗟𝗘𝗪𝗔 𝗞𝗪𝗔 𝗦𝗛𝗔𝗡𝗚𝗪𝗘 𝗗𝗔𝗥 𝗘𝗦 𝗦𝗔𝗟𝗔𝗔𝗠
30-05-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
30-05-2026