BALOZI NCHIMBI: CCM KUENDELEA KUIMARISHA USHIRIKIANO WA NDANI NA NJE
BALOZI NCHIMBI: CCM KUENDELEA KUIMARISHA USHIRIKIANO WA NDANI NA NJEChama Cha Mapinduzi (CCM) kimesisitiza dhamira yake ya kuendeleza na kuimarisha ushirikiano wa ndani na kimataifa chini ya uongozi wa Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan.
CCM ambacho ni chama tawala nchini kimeeleza kuwa kitasimamia Serikali ili kuendeleza uhusiano mzuri na mataifa na taasisi mbalimbali, ndani na nje ya nchi, kwa lengo la kuleta maendeleo kwa wananchi.
Kauli hiyo imetolewa na Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, alipokutana kwa nyakati tofauti na mabalozi wa Korea Kusini, Norway na Uingereza katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, jijini Dar es Salaam, leo Alhamisi, tarehe 13 Februari 2025.
Katika mazungumzo yake na Balozi wa Korea Kusini nchini Tanzania, Mhe. Ahn Eunju, Balozi Nchimbi alisisitiza umuhimu wa kuimarisha uhusiano wa kihistoria kati ya Tanzania na Korea Kusini, hasa katika nyanja za maendeleo ya kiuchumi na teknolojia.
Kwa sasa, Tanzania inanufaika na mkopo nafuu wa Dola bilioni 2.5 kutoka Korea Kusini kwa ajili ya sekta za elimu, afya na miundombinu, huku mojawapo ya miradi mikubwa ikiwa ni ujenzi wa Bandari ya Uvuvi Bagamoyo yenye thamani ya Dola milioni 156.5. Pia, nchi hizo mbili zinaimarisha ushirikiano katika sekta ya madini, hususan utafiti na uchimbaji wa madini mkakati kama nikeli na lithiamu.
Katika mazungumzo yake na Balozi wa Norway nchini Tanzania, Mhe. Tones Tinnes, Balozi Nchimbi alibainisha kuwa Norway ni mshirika mkubwa wa maendeleo wa Tanzania, huku uhusiano wao ukiwa umejengwa katika misingi imara kwa miongo mingi.
Katika uendelezaji wa ushirikiano huo, Norway inashirikiana na Tanzania katika utekelezaji wa miradi ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi, ikihusisha sekta za kilimo, nishati, maji na afya.
Vilevile, katika mazungumzo yake na Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Mhe. Marianne Louise Young, Balozi Nchimbi alisema kuwa uhusiano wa kihistoria kati ya Tanzania na Uingereza, pamoja na ushirikiano wa karibu na Serikali ya Chama cha Labour, unalenga kuhakikisha wananchi wa pande zote mbili wananufaika na maendeleo ya kiuchumi na kijamii.
Kwa nyakati tofauti, katika mazungumzo yao na Katibu Mkuu wa CCM, mabalozi hao walipongeza maamuzi ya Mkutano Mkuu Maalum wa CCM uliomchagua Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Balozi Nchimbi kuwa mgombea mwenza, na Dkt. Hussein Ali Mwinyi kuwa mgombea wa Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM.
Katika kuhitimisha, Balozi Nchimbi imesisitiza kuwa CCM itaendelea kusimamia ushirikiano wa kimataifa kwa kuzingatia misingi ya amani, utulivu na uongozi bora, ili kuhakikisha Tanzania inaendelea kunufaika na ushirikiano wake na mataifa mbalimbali duniani.
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
09-12-2025
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
09-12-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
09-12-2025
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
09-12-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
09-12-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
09-12-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
09-12-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
09-12-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
09-12-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
09-12-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
09-12-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
09-12-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
09-12-2025
TAARIFA KWA UMMA
09-12-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
09-12-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
09-12-2025