WAZIRI BASHE AMTHIBITISHIA BALOZI DKT. NCHIMBI KUWA SERIKALI ITAFUNGUA MAGHALA YA (NFRA) KUANZA KUNUNUA MAZAO KWA WAKULIMA
> Asema ruzuku ya mbolea kuendelea kutolewa kwa kuzingatia maelekezo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan
> Asema wizara inatekeleza agizo la Katibu Mkuu Dkt. Nchimbi kulipa madeni ya nyuma ya wakulima.
> Abainisha kuwa serikali imepiga marufuku vyama vya ushirika kukoa fedha kwakuwa mzigo wanaangushiwa wakulima pasipo kushirikishwa katika hatua za ukopaji wa fedha hizo
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, amempigia simu Waziri wa Kilimo Ndugu. Hussein Bashe na kumtaka kutolea ufafanuzi kuhusu suala la changamoto ya mahindi ya msimu uliyopita ambayo bado yapo kwenye (store) zao wakulima kwakuwa hayajanunuliwa hadi sasa na msimu mpya unaenda kuanza jambo litakalopelekea kuwa na mahindi mengine hivyo ombi lao kwa serikali ni kuona namna gani itawasaidia kuhakikisha wanapata soko la mahindi yao.
Akizungumza kwa njia ya simu kwenye mkutano wa hadhara Mbinga Mkoani Ruvuma, Waziri Bashe ameanza kwa kusema kuwa Wizara ilipokea maelekezo yake Katibu Mkuu ya kulipa madeni ya msimu huu uliobaki walipokuwa wakinunua na kumueleza kuwa kwa sasa wapo hatua ya mwisho kumaliza kulipa madeni hayo na kuwahakikishia wakulima wote wa Mbinga na Ruvuma kwa ujumla na mikoa yote ya kilimo cha mahindi nchini kwamba serikali itafungua tena maghala NFRA (wakala wa Taifa wa hifadhi ya chakula) kama walivyonunua mwaka jana na mwanzoni mwa mwaka huu itanunua mahindi kwa bei nzuri na kuwataka kutoa hofu katika hilo.
Pia, Waziri Bashe amesema baada ya bajeti kupita mwezi wa 5 mwaka huu, wizara itatangaza tarehe ya NFRA kuanza kununua mahindi yakiwemo ya mwaka jana waliyobaki nayo.
Vilevile , Waziri Bashe amemthibitishia Katibu Mkuu kuwa ruzuku ya mbolea kwa wakulima itaendelea vilevile kwa kulingana na maelekezo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwamba mpaka 2025/2026 serikali kuendelea kutoa ruzuku ya mbolea kama kawaida.
Aidha, Waziri Bashe amebainisha kuwa wakulima wa kahawa wa Mbinga , katika kikao walichofanya hivi karibuni, amemuelekeza Mrajis wa vyama vya ushirika kwenda kupitia upya mfumo wa vyama vya msingi kukopa fedha kwa niaba ya wakulima na mwisho wa siku mzigo wa madeni unabebeshwa kwa wakulima, kwahiyo watapitia mfumo na serikali imepiga marufuku vyama vya ushirika kukopa fedha halafu mzigo kubambikiziwa wakulima wa wa kahawa bila hata wao kuambiwa.
Bashe ameendelea kusisitiza kuwa serikali inaenda kubadilisha bei wanayobebeshwa wakulima ya kulipia magunia ya kahawa baada ya bunge la bajeti utatangazwa mfumo mpya wa uuzaji wa kahawa.
ποΈ22 Aprili, 2024
πMbinga - Ruvuma
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
09-12-2025
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
09-12-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
09-12-2025
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
09-12-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
09-12-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
09-12-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
09-12-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
09-12-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
09-12-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
09-12-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
09-12-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
09-12-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
09-12-2025
TAARIFA KWA UMMA
09-12-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
09-12-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
09-12-2025