Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla ameitaka Kampuni ya Fuchs Contraction Ltd ambayo imepewa dhamana ya kujenga skuli nane (8) za Gorofa kuhakikisha wanakamilisha ujenzi huo ndani ya muda uliopangwa na kiwango kilichokusudiwa ili kutoa nafasi kwa wanafunzi kusoma katika mazingira mazuri
Ameyasema hayo katika ziara ya kutembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa skuli zinazojengwa na Kampuni hiyo ikiwa ni muendelezo wa ziara yake ya kutembelea Miradi ya Maendeleo.
Mhe. Hemed amemuagiza Mkandarasi wa majengo hayo kuongeza nguvu kazi na kufanya kazi mchana na usiku ili kuhakikisha Miradi hio inakamilika kwa wakati na kiwango kilichokusudiwa ili kuwaondolea changamoto wanafunzi ya kufata elimu masafa ya mbali jambo ambalo linapunguza umakini na ufaulu kwa wanafunzi hao.
Amesema mtazamo na adhma ya Rais Dkt Hussen Mwinyi ni kujenga skuli za kisasa zenye viwango na zenye kuendana na wakati sambamba na kuweka vifaa vya kutosha vya kufundishiia ili kupunguza msongamano wa wanafunzi madarasani pamoja na kuingia mkondo moja tu kwa wanafunzi wote wa Zanzibar.
Makamu wa Pili wa Rais amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itatoa kila aina ya ushirikiano kwa wakandarasi hao na kuwahakikishia kuwa kiwango cha fedha kilichobakia kitalipwa ndani ya siku chache zijazo ili kuharakisha umalizikaji wa ujenzi huo na wanafunzi waliopangishwa katika maskuli jirani waweze kurejea maskuli mwao.
Nae Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe. Ali Abdulghulam Hussein amesema ziara ya kutembelea Miradi ya Ujenzi wa Skuli za gorofa zinazoendelea kujengwa itatoa matokeo chanya ndani ya muda mfupi ujao na uongozi wa wizara utahakikisha majengo yote yanamalizika kwa kiwango cha hali ya juu.
Naibu Waziri Ghulam amesema vifaa vyote kwa ajili ya maskuli yanayojengwa Zanzibar vipo tayari na Wizara imetenga Bajeti kwa ajili ya kuyafanyia ukarabati mkubwa maskuli yote yaliyoanza kuchakaa ili yaendane na hadhi ya majengo yanayojengwa sasa.
Kwa upande wake Mwakalishi wa mmiliki wa Kampuni ya Fuchs Contraction Ltd Ndugu YASIN FEISAL IBRAHIM amesema Kampuni imejipanga kufanya kazi usiku na mchana na kuahidi kukamilisha ujenzi wa maskuli hayo kwa ubora na viwango vya hali ya juu ifikapo mwishoni mwa mwezi wa nane(8).
Mkandarasi Feisal amesema kulikuwa na changamoto ndogo ndogo ambazo zilikwamisha ujenzi huo lakini kwa sasa kila kitu kipo sawa hivyo watahakikisha wanapambana ili waweze kukabidhi kwa wakati na kutumia fursa hio kuiomba Serikali kuwamalizia malipo ya fedha zilozobaki ili kazi iendelee kwa haraka zaidi.
Mapema Mshauri elekezi kutoka wakala wa majengo Zanzibar (ZBA) MOH'D NAHODA MOH'D amesema makubaliano ya awali na Kampuni ya Fuchs ni kukamilisha Ujenzi huo mwishoni mwa mwezi wa saba(7) lakini imekuwa tofauti na ujenzi huo unaonekana kusuasua jambo ambalo linachelewesha mipango ya Serikali ya kuboresha miundombinu ya Sekta ya Elimu kama ilani ya Chama cha Mapinduzi inavyoelekeza.
Mkandarasi Nahoda amesema endapo kampuni ya Fuchs itashindwa kukamilisha kwa wakati miradi hio ZBA kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali watangali ni kwa namna gani wanaweza kufanya maamuzi ya kisheria dhidi ya kampuni hio ili kuwaweka sawa wakandarasi wengine waliopewa dhamana ya kujenga miradi ya Serikali.
Katika ziara hio makamu wa pili wa rais wa Zanzibar ametembelea ujenzi wa skuli za ghorofa ikiwemo CHUMBUNI, MAUNGANI, MWERA, REGEZAMWENDO, KIJICHI, CHUMBUNI na MUUNGANO
𝐒𝐇𝐔𝐋𝐄 𝐘𝐀 𝐌𝐒𝐈𝐍𝐆𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐒𝐀𝐃𝐀𝐋𝐀 𝐘𝐀𝐎𝐍𝐃𝐎𝐀 𝐊𝐄𝐑𝐎 𝐘𝐀 𝐊𝐔𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐀 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐌𝐄𝐓𝐀 𝟏𝟐 𝐊𝐖𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐈
31-05-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐀𝐀𝐍𝐙𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀𝐍𝐈 𝐇𝐀𝐈, 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
31-05-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐀𝐀𝐍𝐙𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐇𝐀𝐈 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
31-05-2026
𝐍𝐈 𝐌𝐔𝐃𝐀 𝐖𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐇𝐀𝐈-𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎 𝐒𝐀𝐒𝐀
31-05-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐌𝐏𝐀 𝐁𝐀𝐉𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐒𝐈𝐇𝐀 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐘𝐄 𝐔𝐋𝐄𝐌𝐀𝐕𝐔 𝐖𝐀 𝐌𝐈𝐆𝐔𝐔
31-05-2026
MAWENZI YAVUNJA REKODI: MITUNGI 3,313 YA OKSIJENI YAZALISHWA KWA MIEZI 6, ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 126 ZAOKOLEWA!
31-05-2026
MAFURIKO YA WANANCHI WA SIHA KWENYE MKUTANO MKUBWA WA HADHARA
31-05-2026
MAPOKEZI YA KATIBU MWENEZI WA CCM NDUGU KENANI L KIHONGOSI MKOANI KILIMANJARO
31-05-2026
🔰 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐒𝐇𝐈𝐍𝐃𝐎 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
31-05-2026
CCM INAWATAKIA HERI YA SIKUKUU YA EID AL ADHA
31-05-2026
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
31-05-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
31-05-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
31-05-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
31-05-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
31-05-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
31-05-2026
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
31-05-2026
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
31-05-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
31-05-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
31-05-2026