Wazazi na walezi wametakiwa kutoa ushirikiano kwa walimu wa madrasa na walimu wa skuli pamoja na kujua taarifa na mienendo ya watoto wao ili kupata wataalamu na wanazuoni wabobezi wa baabae.
Hayo yamesemwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Alhajj Hemed Suleiman Abdulla wakati akiwasalimia waumini wa Masjid IITISWAM uliopo TUNGUU KWA SHEMEGO Wilaya ya Kati Unguja mara baada ya kumaliza Ibada ya Sala ya Ijumaa.
Amesema kuwa kuwafatilia vijana katika suala zima la kupata elimu zote mbili kutapelekea kupata walaalamu watakao weza kulisaidia Taifa katika kusimamia miradi mbali mbali ya kimaendeleo pamoja na kupata wanazuoni watakao watakaoitetea dini ya kiislamu kwa ushahidi wa Qur-an na Sunna.
Alhajj Hemed amesema suala la wazazi na walezi kuwasiamamia vijana katika mambo mema yakiwemo suala la Elimu na Ibada ni suala la lazima kwani kufanya hivyo ni kutimiza wajibu wao na kujiweka huru na masuala mbele ya M.Mungu kwani kila mzazi ni mchunga juu ya mtoto wake.
Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar amesema kuwa maisha ya duniani ni mapito tu hivyo ni lazima kujiandaa kwa kufanya Ibada pamoja na kuwaandaa watoto katika suala zima la kuwapatia elimu yenye manufaa hapa duniani na kesho akhera.
Sambamba na hayo Alhajj Hemed amewataka wazazi na walezi kuwafuatilia watoto wao wanaoingia skuli katika mkondo wa jioni kwa skuli ambazo bado wanafanya hivyo kwani serikali ya awamu ya Nane (8) inayoongozwa na Dkt. Hussein Ali Mwinyi inahakikisha inaendelea kujenga skuli za ghorofa kila sehemu ili kuwawezesha wanafunzi kusoma mkondo mmoja tu na kupata elimu iliyobora kwa maslahi ya taifa.
Mapema akitoa Khutba katika Sala ya Ijumaa, Ustadh. RAJAB R’DHAN CHOUM amewaasa waumini wa Dini ya Kiislam hasa wale waliomo kwenye Ndoa kuacha tabia ya kutoa Talaka kiholela jambo ambalo linamkirihisha sana Allah (S.W) na kupelekea kuwasambaratisha watoto na kukosa malezi yaliyo bora kutoka kwa wazazi wawili.
Amesema kuwa kumekuwa na tabia kwa baadhi ya wazazi kususiana watoto wanapoachana huku wakijua kuwa kufanya hivyo ni kuwakosesha haki zao za msingi na kupelekea Taifa kuwa na watoto wengi wa mtaani na kuongezeka kwa mambo maovu na machafu baina yao.
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
24-10-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
24-10-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
24-10-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
24-10-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
24-10-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
24-10-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
24-10-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
24-10-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
24-10-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
24-10-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
24-10-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
24-10-2025
TAARIFA KWA UMMA
24-10-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
24-10-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
24-10-2025
MONGELLA AONGOZA MAZISHI YA KADA WA CCM JIJINI MWANZA
24-10-2025
ASIYETII SHERIA, KATIBA NA KUWA TAYARI KUUA KWA MASLAHI BINAFSI HUO NI UGAIDI’
24-10-2025
πππ π¬ππ¦ππ¦ππ§πππ πͺπππ’π πππ ππ¨πππππππͺπ ππͺπ ππ¨πππ‘πππ§ππ π¨πͺπππ’, π¨πππππ‘ππ’ π‘π π¨πππππππ¨, π¬ππππ ππ π πππ¨π‘ππ - πππ. πππ©π¨
24-10-2025
KAENI KIMYA KAMA HAMJUI NCHI ILIKOTOKA - WASIRA
24-10-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amefungua kiwanda cha kutengeneza mabomba ya maji na uchakataji pamba cha MOLI Oil Mills Co. Ltd kilichopo Bariadi Mkoani Simiyu tarehe 16 Juni, 2025.
24-10-2025