BALOZI NCHIMBI: MALEZI YA WALIMU NI MUHIMU KATIKA UJENZI WA TAIFA IMARA
Atoa wito kwa viongozi wa dini kuiombea Tanzania dhidi ya vurugu
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, amesema malezi na mafunzo wanayopata wanafunzi shuleni, hasa yanayosisitiza nidhamu na uwajibikaji, ni msingi muhimu katika kujenga taifa imara lenye uzalendo.
Aidha, ametoa wito kwa viongozi wa dini na madhehebu mbalimbali kuendelea kuiombea Tanzania ili iendelee kuwa na amani na kuepuka athari za watu wanaotaka kuingiza nchi katika vurugu.
Balozi Nchimbi aliyasema hayo wakati wa kikao cha umoja wa wanafunzi waliosoma Shule ya Sekondari ya Uru Seminari, kilichofanyika Moshi, mkoani Kilimanjaro, baada ya ibada na mazishi ya aliyewahi kuwa Baba Gombera wa seminari hiyo, Padri Canute Mkwe Shirima AJ, mnamo Machi 20, 2025.
“Hakuna aliyesoma Uru Seminari asiyetambua mchango wa kipekee wa Padri Shirima. Tulifundishwa nidhamu, uwajibikaji, bidii kazini, na umuhimu wa kufuatilia mambo kwa umakini. Mafundisho hayo yametufanya kuwa watumishi bora katika nyanja mbalimbali za maisha,” alisema Balozi Nchimbi.
Aliongeza kuwa malezi ya walimu yana mchango mkubwa katika kujenga jamii yenye maadili na uzalendo, akisisitiza kuwa Taifa linapaswa kuthamini juhudi za walimu katika kujenga kizazi chenye maadili.
Katika kuendeleza maadili na mshikamano wa kitaifa, Balozi Nchimbi aliwasihi viongozi wa dini waendelee kuliombea Taifa na viongozi wake ili Tanzania iendelee kuwa nchi yenye utulivu.
“Nawaomba viongozi wa dini muendelee kuikabidhi nchi yetu kwa Mungu. Tuendelee kuiombea Tanzania, viongozi wake wa Serikali, CCM, na hata wa upinzani, ili Mungu aendelee kutuongoza. Kuna watu wenye nia ya kusababisha vurugu, hivyo ni muhimu sana tukaendelea kuilinda amani yetu,” alisema.
Aidha, alitoa pongezi kwa umoja wa wanafunzi waliosoma Uru Seminari kwa mshikamano waliouonyesha katika msiba wa Padri Canute, akiwahimiza kuendeleza umoja huo kwa manufaa ya jamii na Taifa kwa ujumla.
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
09-12-2025
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
09-12-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
09-12-2025
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
09-12-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
09-12-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
09-12-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
09-12-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
09-12-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
09-12-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
09-12-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
09-12-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
09-12-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
09-12-2025
TAARIFA KWA UMMA
09-12-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
09-12-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
09-12-2025