Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar Dkt.Mohamed Said Dimwa,amesema Serikali inakopa fedha kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo ya Wananchi wote na sio kwa maslahi ya watu wachache
Hayo ameyasema katika mwendelezo wa ziara yake wakati akizungumza na wanachama wa katika Tawi la CCM Mafufuni Jimbo la Bumbwini Wilaya ya Kaskazini "B" Kichama Mkoa wa Kaskazini Unguja.
Dkt.Dimwa, alisema kauli za baadhi ya wanasiasa wa vyama vya upinzani kuilaumu Serikali juu ya masuala ya mikopo ya fedha kutoka kwa wadau wa maendeleo inatakiwa kupuuzwa kwani fedha hizo ni kwa ajili ya kuimarisha miradi ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa miundombinu ya barabara za lami,maji safi na salama,ujenzi wa Skuli za kisasa,hospitali,viwanja vya ndege vya kisasa pamoja na bandari za kisasa.
Alifafanua kuwa katika bajeti ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 2024/2025 iliyopitishwa hivi karibuni, zaidi ya asilimia 63 ya fedha za bajeti hiyo zimeelekezwa katika uimarishaji wa miradi ya maendeleo kwa ajili ya kukabili changamoto za wananchi wote wa mijini na vijijini.
"suala la kukopa fedha kwa ajili ya maendeleo sio la Zanzibar tu wala Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bali nchi mbalimbali duniani zinakopa na kwa mujibu wa takwimu kutoka shirika la fedha duniani (IMF) nchi zilizoendelea kiuchumi mfano marekani,urusi,ufaransa na zingine ndio zenye madeni makubwa hivyo hao wanasiasa nawashauri wajiongeze kwa kufanya utafti wa kujua mwenendo wa uchumi wa dunia unaendaje.
Wito wangu kwenu tuendeleeni kuwaombea dua njema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan pamoja na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Mwinyi Mwenyezi Mungu awajaalie nguvu,busara na imani ili nchi iendelee kupiga hatua kubwa za kimaendeleo katika nyanja kiuchumi na kijamii",alisema Dkt.Dimwa.
Katika maelezo yake Dkt.Dimwa, aliwataka Wanachama wa CCM na Jumuiya zake kwa ngazi za Mashina na Matawi kufanya vikao vya mara kwa mara ili kujadili masuala ya maendeleo,changamoto na mikakati ya pamoja ya kuimarisha taasisi hiyo.
Naibu Katibu Mkuu huyo Dkt.Dimwa, aliwasihi Viongozi,Watendaji na wanachama kwa ujumla kuhamasisha wananchi na wafuasi wa Vyama vya upinzani kujiunga na Chama ili kuongeza idadi ya wapiga kura wa Chama Cha Mapinduzi.
Mapema Dkt.Dimwa akizungumza na wanachama,viongozi na watendaji wa Chama na Jumuiya zake baada ya kuwasili katika Mkoa huo,aliwapongeza kwa kazi kubwa ya kusimamia kikamilifu utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM mwaka 2020-2025 ndani ya Mkoa huo.
Naye Katibu wa Kamati Maalum ya NEC,Idara ya Organazesheni CCM Zanzibar Omar Ibrahim Kilupi, aliwasisitiza Wanachama hao kuhakikisha wanapata kadi za kupiga kura ili wawe na uhalali wa kukipigia kura nyingi Chama Cha Mapinduzi.
Alitoa shukrani Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM ya Mkoa huo, Haji Juma Hajialiahidi kuwa wamejipanga vizuri kuhakikisha CCM inapata ushindi mkubwa wa majimbo yote ya Mkoa huo katika Uchaguzi Mkuu ujao
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐌𝐏𝐀 𝐁𝐀𝐉𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐒𝐈𝐇𝐀 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐘𝐄 𝐔𝐋𝐄𝐌𝐀𝐕𝐔 𝐖𝐀 𝐌𝐈𝐆𝐔𝐔
31-05-2026
MAWENZI YAVUNJA REKODI: MITUNGI 3,313 YA OKSIJENI YAZALISHWA KWA MIEZI 6, ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 126 ZAOKOLEWA!
31-05-2026
MAFURIKO YA WANANCHI WA SIHA KWENYE MKUTANO MKUBWA WA HADHARA
31-05-2026
MAPOKEZI YA KATIBU MWENEZI WA CCM NDUGU KENANI L KIHONGOSI MKOANI KILIMANJARO
31-05-2026
🔰 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐒𝐇𝐈𝐍𝐃𝐎 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
31-05-2026
CCM INAWATAKIA HERI YA SIKUKUU YA EID AL ADHA
31-05-2026
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
31-05-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
31-05-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
31-05-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
31-05-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
31-05-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
31-05-2026
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
31-05-2026
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
31-05-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
31-05-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
31-05-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
31-05-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
31-05-2026
𝗞𝗜𝗦𝗛𝗜𝗡𝗗𝗢 𝗖𝗛𝗔 𝗗𝗞𝗧. 𝗠𝗜𝗚𝗜𝗥𝗢 𝗖𝗛𝗔𝗣𝗢𝗞𝗘𝗟𝗘𝗪𝗔 𝗞𝗪𝗔 𝗦𝗛𝗔𝗡𝗚𝗪𝗘 𝗗𝗔𝗥 𝗘𝗦 𝗦𝗔𝗟𝗔𝗔𝗠
31-05-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
31-05-2026