RAIS WA ZANZIBAR MHE.DK.HUSSEIN MWINYI AZUNGUMZA NA NA BALOZI WA NORWAY NCHINI TANZANIA MHE. ELIZABETH JACOBSEN IKULU ZANZIBAR
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi ameishukuru Serikali ya Norway kwa jitihida zake za kuendelea kuiunga mkono Tanznia ikiwemo Zanzibar kwenye masuala mbalimbali ya maendeleo.
Dk. Mwinyi ametoa shukurani hizo Ikulu, Zanzibar alipozungumza na Balozi wa Norway nchini Tanzania, Elizabeth Jacobsen aliyefika kuaga baada ya kumaliza kipindi chake cha utumishi nchini.
Rais Dk. Mwinyi alimueleza Balozi Jacobsen kwamba, Zanzibar imenufaika na fursa nyingi kutoka Norway zikiwemo sekta za Afya, Umeme na Elimu.
Amesema uhusiano wa Norway na Tanzania utakumbukwa zaidi kwa kuinufaisha Zanzibar kupitia sekta ya umeme, hasa wa kutoka Tanga hadi Pemba na Dar es Salaam hadi Zanzibar ambapo Dk. Mwinyi alieleza, Norway ilitoa mchango mkubwa kuunga mkono juhudi za serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzaznia katika kuwafikishia huduma bora wananchi.
“Tunaishukuru Serikali ya Norway kwa kuendelea kutuunga mkono Tanzania, hasa kwenye sekta za Afya na umeme, tunashukuru Norway imetuungamkono kwenye sekta ya umeme, ilisaidia kueneza umeme visiwani Zanzibar” alisifu Rais Dk. Mwinyi.
Aidha, Dk. Mwinyi alimueleza balozi huyo dhamira ya Zanzibar kutaka kujitegemea kwa umeme wake wenyewe ili kuwapatia huduma ya uhakika wananchi wa Unguja na Pemba badala ya kutegemea umeme kutoka Tanzania Bara.
“Kwa hatua tuliofikia sasa, Zanzibar inataka isimame wenyewe ijitegemee wenyewe umeme wake utakaozalishwa hapa hapa Zanzibar” alieleza Dk. Mwinyi.
Pia alisifu Rais Dk. Mwinyi, alisifu ushirikiano ulipo baina ya Norway na Tanzania hasa kwenye nyanja za afya na elimu na kueleza Serikali ya Norway imetoa mchango mkubwa kwa Tanzania kwa kuwajengea uwezo Watanzania wengi kupitia vyuo vikuu vya nchi hiyo.
“Hatunabudi kuishukuru Serikali ya Norway, kupitia vyuo vikuu vya afya vya huko vimewajengea uwezo watu wetu kupitia sekta za Umma na binafsi” alisifu Dk. Mwinyi.
Akizungumza na Rais Dk. Mwinyi, Balozi Elizabeth ameisifu Tanzania kuendelea kuwa nchi ya amani, yenye raia wenye upendo, ushirikiano, umoja na utulivu wa kisiasa akieleza kuwa Tanzania ni kielelezo cha nchi ya mfano barani Afrika na kwengineko duniani kuwa ni taifa lenye demokrasia kwa kutekeleza na haki za binaadamu na siasa safi.
Balozi huyo alimuahidi Rais Dk. Mwinyi, kwamba Serikali ya Norway daima itaendelea kuiungamkono Tanzania ikiwemo Zanzibar kwenye sekta za Maendeleo.
Alisema Serikali ya Norway inajivunia uhusiano wa muda mrefu wa diplomasia uliopo baina yake na Tanzania na kusifu zaidi ya miaka 50 yaushirikiano wao kwenye masuala mbalimbali iliwemo ushirikiano walionao baina ya vyuo vikuu vya Norway na Tanzania ni chachu iliyokuza urafiki baina ya watu wa mataifa wawili hayo kwenye nyanja mbalimbali za jamii na uchumi.
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
09-12-2025
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
09-12-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
09-12-2025
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
09-12-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
09-12-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
09-12-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
09-12-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
09-12-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
09-12-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
09-12-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
09-12-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
09-12-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
09-12-2025
TAARIFA KWA UMMA
09-12-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
09-12-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
09-12-2025