Makamu wa Pili wa Rais Mhe.Hemed Suleiman Abdulla ametoa agizo kwa uongozi wa Kampuni ya Lancet kuhakisha ndani ya mwezi mmoja kitengo cha wagonjwa walio katika uangalizi maalum (ICU) katika hospitali ya Wilaya ya Magharibi “B” Mwanakwerekwe Ijitimai kinatoa huduma ili kuondoa usumbufu wa ongezeko la wagonjwa katika hospital ya Rufaa ya Mnazi Mmoja.
Ameyasema hayo wakati alipofanya ziara ya kutembelea na kukagua maendeleo ya utowaji na upatikanaji wa huduma za Afya kwa wananchi katika hospital ya Wilaya ya Magharibi “B” Mwanakwerekwe Ijitimai na Hospital ya Taifa ya Rufaa ya Mnazi Mmoja Mkoa wa Mjini Magharibi.
Amesema kuwa Kampuni ya Lancet ina wajibu wa kuhakikisha huduma zote muhimu zinapatika kwa ubora na haraka kwa wagonjwa wanaofika katika hospitali zote za Wilaya ili kuondosha msongamano wa wagonjwa katika hospital za Rufaa ya Mnazi Mmoja.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amesema Serikali ya Awamu ya Nane imelipa kipaombele suala la kuboresha miundombinu ya Afya ili kuzidi kutoa huduma bora za kitabibu kwa Wananchi hivyo wananchi wanapaswa kuunga mkono juhudi zinazochukuliwa na viongozi katika kuwaletea maendeleo ikiwemo upatikanaji wa huduma bora za Afya.
Mhe. Hemed amewasisitiza madaktari kudumisha nidhamu katika kazi kwa kufuata miiko, miongozo na maadili ya kazi zao na kuachana na tabia ya kuwatolea lugha chafu wagonjwa hasa wahuduma za Dharura ili kuendelea kuilinda heshima ya wananchi ambapo Serikali haitamvumilia mtu yoyote atakae kwenda kinyume na maadili ya kazi na itamchukulia hatua za kisheria na kinidhamu kwa haraka .
Aidha Makamu wa Pili wa Rais amezitaka kampuni ya Lancet na NSK zinazotoa huduma katika hospital za Wilaya na Hospital ya Rufaa ya Mnazi Mmoja kuhakikisha changamoto zote za vifaa, wataalamu na kiutendaji zinapatiwa ufumbuzi kwa haraka ili kupunguza malalamiko kwa wananchi ambao wameipa Imani Serikali yao ya kiwatumikia na kuwaletea maendeleo.
Sambamba na hayo amewasisitiza wananchi kuendelea kuzitumia Hospitali za Wilaya katika kutafuta matibabu ambazo zinatoa huduma zote za kitabibu ili kupunguza wingi wa wagonjwa katika hospitali za Rufaa.
Makamu wa Pili wa Rais amesema kuwa Serikali kuu itahakikisha inatatua chamgamoto zote zinazoikabili Sekata ya Afya zitapatiwa ufumbuzi wa haraka ili kuendelea kutoa huduma bora na stahiki kwa wananchi bila ya ubaguzi wa aina yoyote.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Hospital ya Rufaa ya Mnazi Mmoja Dkt. MUHIDDIN ABDI MAHMOUD amesema katika kupunguza changamoto ya wataalamu katika Hospitali za Wilaya na Rufaa Wizara ya Afya imeamua kusomesha wafanyakazi wake kwa kuwalazimisha kusomea zile kada ambazo zina upungufu wa madaktari ili kuweza kutoa huduma zilizo bora na kwa wakati.
Amesema kuwa Wizara ya Afya imepanga kuandaa utaratibu wa kuwashauri na kuwashawishi wanafunzi wanaojiunga na vyuo vikuu kusomea kozi ambazo zina uhaba wa wataalamu ikiwemo ICU, Ganzi na Usingizi pamoja na Huduma za dharura ili kuweza kulisaidia Taifa kupata wataalamu wazawa.
Kwa upande wao wananchi waliofika hospitalini hapo kwa ajili ya kupatiwa matibabu wameishukuru Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kuwajengea hospitali za Wilaya na kuwasogezea huduma za matibabu karibu na makazi yao zinazotoa huduma bora na kwa wakati sambamba na kuwashukuru Madaktari kwa huduma bora wanazowapatia wagonjwa wanaofika hospitalini hapo.
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
09-12-2025
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
09-12-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
09-12-2025
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
09-12-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
09-12-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
09-12-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
09-12-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
09-12-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
09-12-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
09-12-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
09-12-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
09-12-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
09-12-2025
TAARIFA KWA UMMA
09-12-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
09-12-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
09-12-2025