CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar kimempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan,kwa juhudi zake za kuimarisha diplomasia inayoongeza fursa za kiuchumi zinazoleta tija na mafanikio kwa pande zote za Muungano.
Kauli hiyo imetolewa na Katibu wa Kamati Maalum ya NEC,Idara Idara ya Itikadi,Uenezi na Mafunzo CCM Zanzibar Khamis Mbeto Khamis,wakati akitoa tathimini na uchambuzi wa fursa na mafanikio ya Tanzania Kimataifa kupitia mahojiano yaliyofanyika katika Kituo cha Radio ya Bahari FM,kilichopo Migombani Zanzibar.
Mbeto,alifafanua kuwa Rais Dkt.Samia,ameendelea kuipaisha Tanzania kiuchumi ili ifike katika kilele cha maendeleo endelevu sambamba na kupata hadhi ya nchi iliyoendelea kiuchumi Barani Afrika.
Alisema Chama Cha Mapinduzi kwa upande wa Zanzibar kinapongeza kwa dhati juhudi,maarifa,ubunifu na uchapakazi wa Rais wa Dkt.Samia na kwamba utendaji huo uliotuka ndio kibali cha Wananchi kumpa ridhaa ya kushinda kwa kishindo Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.
Katika maelezo yake Katibu huyo wa NEC,aliwasihi Wananchi bila kujali tofauti za kisiasa,kidini na kikabila kumuunga mkono kwa kila hatua anayopiga katika kutafuta fursa mbalimbali kupitia ziara,makongamano na mikutano ya kimataifa.
Katibu huyo mwenezi alisema kupitia ziara zake amekuwa akitangaza fursa za Utalii kupitia dhana za Royal Tour na Uchumi wa Buluu zinazofafanua kwa kina rasilimali zilizopo nchini zikiwemo mbuga za wanyama,Bahari,mito,maziwa,vivutio vya mambo ya kale ili raia wa kigeni waje kwa wingi nchini kwa ajili ya Uwekezaji na utalii.
" Najua wapo baadhi ya watu wachache wanakosoa na kubeza juhudi hizi za Rais Dkt.Samia,wakidai anafanya ziara nyingi nchi za nje lakini tukumbuke kuwa ziara hizo sio za kifamilia bali anaenda kutafuta fursa za kiuchumi na kuimarisha mahusiano mema ya kidiplomasia yakiambatana kuingia na mikataba mikubwa yenye tija kwa nchi.
Alisema bajeti Kuu ya Tanzania kwa mara ya kwanza imefikia kiasi cha zaidi ya Trioni 41 ambapo asilimia 35 imeelekezwa katika miradi ya maendeleo inayowanufaisha Wananchi.
Mbeto,akizungumzia ziara za Rais Dkt.Samia,Makao Makuu ya dhehebu la dini ya Kikiristo Vatican,amesema imejenga mahusiano makubwa na kudhihirisha kuwa kiongozi huyo hana ubaguzi anajali imani za dini za wananchi wote.
Alieleza kuwa pamoja na hayo ziara hiyo ya kukutana na Papa Francisko wamekubaliana kuongeza miundombinu ya kijamii na kiuchumi ikiwemo ujenzi wa skuli,vyuo vikuu,hoteli kubwa za kitalii na viwanda vitakavyowanufaisha wananchi wote.
Pia ziara nyingine ya nchini Norway imeendelea kufungua fursa mpya za kiuchumi zikiwemo Uwekezaji katika Sekta za uvuvi pamoja na kuingia mikataba ya kushirikiana katika teknolojia ya masuala ya Gesi na Mafuta nchini.
Mafanikio hayo yanatokana na utekelezaji wa makubaliano na Wananchi kupitia Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020/2025 ibara ya 132 (a)-(e) imeelekeza katika kipindi Cha miaka mitano ijayo,CCM itahakikisha kuwa mahusiano ya nchi kikanda na kimataifa yanaendelea kuimarishwa lengo Kuu ni kuhakikisha Tanzania inaendelea kuwa mstari wa mbele katika kuimarisha Amani,uhuru na maslahi ya Taifa katika nyanja za kimataifa.
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
10-03-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
10-03-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
10-03-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
10-03-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
10-03-2026
πππ¦πππ‘ππ’ πππ πππ§. π ππππ₯π’ ππππ£π’πππππͺπ ππͺπ π¦πππ‘ππͺπ πππ₯ ππ¦ π¦πππππ
10-03-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
10-03-2026
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
10-03-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
10-03-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
10-03-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
10-03-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
10-03-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
10-03-2026
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
10-03-2026
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
10-03-2026
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
10-03-2026
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
10-03-2026
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
10-03-2026
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
10-03-2026
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
10-03-2026