Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.Samia Suluhu Hassan amechangia kiasi cha Shilingi Milioni Hamsini katika Ujenzi wa Majengo ya Taasisi ya Elimu ya Maawal Islamiya iliyopo jijini Tanga ikiwa ni muendelezo wa Serikali wa Awamu ya Sita kuunga mkono jitihada za wadau katika kutoa elimu
Kiasi hicho cha fedha kimewasilishwa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni wakati akihutubia mamia ya waumini wa kiislamu waliokusanyika kusheherekea kuanzishwa kwa taasisi hiyo na kumbukumbu ya Muanzilishi,Sheikh Shabaani Mohamed Hariri ambapo pia alifikisha salamu kwa waumini hao kutoka kwa Rais Samia huku akigusia kuwepo kwa mporomoko wa maadili unaosababisha uhalifu katika sehemu mbalimbali za nchi.
‘Naomba nitumie fursa hii kuwasilisha salamu za Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan wakati nakuja nilimuaga amesema niwasalimie sana na ametoa kiasi cha Shilingi Milioni Hamsini ikiwa ni mchango wake katika ujenzi wenu wa majengo ya madarasa unaoendelea hapa niwaombe pia mumuombee dua ili aweze kuiongoza nchi yetu kwa salama na amani lakini kumekuwepo na mmomonyoko wa maadili niwaombe viongozi wa dini muendelee kutumia sehemu zenu za ibada kuiasa jamii iachane na mila na tamaduni ambazo zipo kinyume na mafundisho ya dini zetu’ alisema Waziri Masauni
Wakizungumza wakati wa hafla hiyo,Sheikh wa Mkoa wa Dodoma,Mustafa Rajab Shabaani na Sheikh wa Mkoa wa Pwani,Alhaji Khamis Mtupa walisisitiza kulindwa kwa maadili katika jamii ambayo yameendelea kuporomoka katika jamii huku wakiwataka waumini kuendelea kuwa karibu na watoto ili kufahamu changamoto mbalimbali wanazokutana nazo.
‘Jamii imekumbwa na mabalaa mbalimbali watu wamekua na unyama usiomithilika mpaka imefikia sasa hivi wazazi kuambiwa kuwakagua watoto katika maumbile yao kila wanapotoka shuleni sasa tuitake jamii iwe karibu na watoto ili kuweza kubaini changamoto zao mbalimbali wanazokutana nazo kwani kutokua nao karibu upelekea watoto hao kukumbana na mabalaa lakini kutokuwepo ukaribu kati ya mzazi na mtoto upelekea mtoto kukaa kimya wakati tayari ashaathirika.’alisema Sheikh Mtupa.
Taasisi hiyo ya Maawal Islamiy ina miaka 44 tangu ianzishwe na Sheikh Shabaan Hariri ikijikita zaidi katika kutoa elimu,misaada kwa watu mbalimbali wenye uhitaji na huduma za afya.
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
09-12-2025
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
09-12-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
09-12-2025
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
09-12-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
09-12-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
09-12-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
09-12-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
09-12-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
09-12-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
09-12-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
09-12-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
09-12-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
09-12-2025
TAARIFA KWA UMMA
09-12-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
09-12-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
09-12-2025