CCM KUFADHILI KITABU CHA MZEE SONGAMBELE KUENZI HISTORIA YA NCHI, CHAMA NA SERIKALI
Balozi Nchimbi atoa neno, akimwakilisha Dkt. Samia msibani
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi amesema kitabu alichoandika Alhaj Mzee Mohamed Mustafa Songambele kitakuwa mojawapo ya rejea adhimu za historia ya Tanzania.
Balozi Nchimbi amesema kuwa kitabu hicho kiitwacho “Safari ya Karne”, kina utajiri wa maelezo kuhusu mapambano ya kutafuta uhuru wa Tanganyika, kupatikana kwa nchi na taifa la Tanzania na kuundwa kwa CCM.
Dkt. Nchimbi amesema hayo alipokuwa akitoa salaam za pole na rambirambi kwenye msiba wa Hayati Alhaji Mzee Songambele, akimwakilisha Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, mjini Songea, mkoani Ruvuma, leo Jumatatu tarehe 2 Juni 2025.
“Kutokana na heshima na mchango mkubwa wa Mzee Songambele kwa nchi yetu, taifa letu na chama chetu, Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuguswa sana na msiba huu, ameniagiza rasmi kumwakilisha na ameagiza Chama na Serikali kuchukua gharama zote za msiba huu.
“Mzee Songambele amefariki akiwa amemaliza kuandika kitabu chake. Hadi mwezi Machi mwaka huu, alikuwa amekiita jina la “Swahiba wa Nyerere”, lakini miezi miwili iliyopita akabadili, nadhani aliona atatimiza miaka 100, akakiita “Safari ya Karne,” amesema Balozi Nchimbi na kuongeza;
“Kutokana na umuhimu wa kitabu hicho, ambacho aliniomba niandike dibaji na niliandika, humo ameelezea mengi kuhusu yeye na Nyerere, harakati za uhuru, utaifa wetu na CCM pia, Chama Cha Mapinduzi kitasimamia ili kitabu hicho kitoke ili Watanzania wapate kujifunza historia vizuri,” alisema Balozi Nchimbi.
Aidha, Balozi Nchimbi alisema Mzee Songambele pia alikuwa mmoja wa viongozi waliotoa mchango mkubwa kwa nchi, taifa, chama na serikali kutokea Mkoa wa Ruvuma, akisisitiza kuwa hilo ni jambo linalostahili kuenziwa na viongozi wa kizazi cha sasa kwa kuwa waadilifu, wanaowajibika, wazalendo kwa nchi na kuwatumikia watu.
Hayati Alhaji Mzee Songambele, mwanasiasa na kiongozi mkongwe nchini, ambaye alifariki usiku wa kuamkia Jumapili ya tarehe 1 Juni, mwaka huu, alizikwa Jumatatu Juni 2, 2025 katika makaburi ya familia yaliyoko Bombambili, mjini Songea.
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
12-03-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
12-03-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
12-03-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
12-03-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
12-03-2026
πππ¦πππ‘ππ’ πππ πππ§. π ππππ₯π’ ππππ£π’πππππͺπ ππͺπ π¦πππ‘ππͺπ πππ₯ ππ¦ π¦πππππ
12-03-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
12-03-2026
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
12-03-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
12-03-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
12-03-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
12-03-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
12-03-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
12-03-2026
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
12-03-2026
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
12-03-2026
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
12-03-2026
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
12-03-2026
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
12-03-2026
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
12-03-2026
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
12-03-2026