KINANA ASHAURI WATUMISHI, WATAALAMU SERIKALINI WASITOE AHADI BILA MIPANGO.
MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Abdulrahman Kinana ameeleza kuwa, ni vema Watumishi, wataalamu wa serikali kutotoa ahadi ambazo wanajua hazitatekelezeka au utekelezaji wake utachukua muda mrefu kukamilika kwani imekuwa ikikwamisha shughuli za maendeleo na kusababisha malalamiko kwa wananchi.
Kinana meeleza hayo alipokuwa akizungumza na wananchi wa Bunda Mjini wilayani Bunda mkoani Mara baada ya kupokea malalamiko ya wananchi kuwa serikali imewataka wahame katika maeneo yao kupisha ujenzi wa mradi wa maendeleo.
Pia, wananchi hao walionesha kukerwa na kitendo cha maeneo yao kuchukuliwa, nyumba kubomolewa na kupewa sharti la kutoendeleza maeneo hayo likiwemo eneo la Kijiji cha Nyantwale.
"Viongozi wa serikali kabla ya kuwahamisha wananchi ni vema wakaeleza ni lini ahadi hiyo itatekelezwa, kama ni fidia, lini fidia hiyo itatolewa, kama ni watu kuhama watahama lini, kama watu ni kupewa fidia watapewa lini," amesema.
Aliongeza kuwa, hakuna sababu ya kutoa ahadi ambayo inachukua miaka mingi kutekelezwa na kila kiongozi anayekuja anatoa ahadi anaondoka.
Kinana alishauri watendaji wa serikali kabla ya kufanya uamuzi unaohusu kuhamisha watu, kufidia au kufanya jambo lolote linalohusu wananchi, ni vyema wafanye utafiti wa kutosha kupata uhakika kuhusu malipo ya wananchi, fedha zipatikanaje ndipo watoe kauli, na si vyema kauli itangulie kabla ya kutanguliza fidia.
Makamu Mwenyekiti Kinana alisema kuwa, kumekuwapo na tabia ya kuwaeleza wananchi kuhusu kuhama au kutohama halafu hakuna kinachoendelea.
Kinana alifafanua zaidia kwa kueleza kwamba, “viongozi na watendaji acheni utaratibu wa kutoa ahadi bila ya kujiandaa, ni muhimu mkajipanga kwanza ili mnapotoka na majibu muwe na uhakika na mnachosema.”
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
22-03-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
22-03-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
22-03-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
22-03-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
22-03-2026
πππ¦πππ‘ππ’ πππ πππ§. π ππππ₯π’ ππππ£π’πππππͺπ ππͺπ π¦πππ‘ππͺπ πππ₯ ππ¦ π¦πππππ
22-03-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
22-03-2026
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
22-03-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
22-03-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
22-03-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
22-03-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
22-03-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
22-03-2026
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
22-03-2026
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
22-03-2026
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
22-03-2026
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
22-03-2026
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
22-03-2026
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
22-03-2026
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
22-03-2026