RAIS SAMIA AMEAMUA KUIFUNGUA MIKOA YA KUSINI KIUCHUMI
Ni barabara ya uchumi Mtwara- Tandahimba- Newala- masasi( 210Km)
MTWARA: Katibu wa Halmashauri Kuu (NEC), Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), CPA Amos Makalla Rais Samia Suluhu Hassan ameamua kuifungua mikoa ya Kusini kiuchumi kwa kutenga kiasi cha Sh bilioni 234 kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya kiuchumi yenye umbali wa kilometa 210.
Makalla alieleza hayo leo Aprili 15,2025 wakati akizungumza na wananchi wa Wilaya ya Tandahimba mkoani Mtwara, ikiwa ni muendelezo wa ziara yake ya siku 10 mkoa wa Lindi na Mtwara.
Aidha, Makalla amesema kuwa Rais Samia amemtuma apite kukagua barabara hiyo ambayo imetajwa kuwa ya kiuchumi na kueleza kuwa hadi sasa kilometa 50 tayari zimekamilika na alijiridhisha kuwa ujenzi bado unaendelea kufanyika kwani amewakuta wakandarasi wakiendelea na maandalizi ya kuikamilisha.
Makalla amesema kuwa Rais Samia anania njema na wananchi wa Kusini mwa Tanzania na katika kutaka kuiimarisha mikoa hiyo kiuchumi ametenga kiasi hicho cha fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara hiyo itakayosaidia katika kuendeleza uchumi.
Akifafanua sababu za barabara hiyo kuwa ya kiuchumi Makalla alisema Rais Samia amefungua mikoa hiyo akiwa na lengo la kuiboresha iweze kukua kwa kuanza na kutoa kiasi cha Sh bilioni 157 kwa ajili kuboresha na kupanua bandari ya Mtwara ambayo itasaidia na kurahisisha usafirishaji wa Korosho kutoka Mtwara kwenda katika maeneo mengine.
Pia amesema kuwa hapo awali Rais Samia alifika Mtwara na kuweka jiwe la msingi katika barabara hiyo inayotoka Newala, Tandahimba hadi Masasi ambayo inakwenda kuunganisha Mtwara na maeneo mengine ya Mchuchuma na Mbamba Bay ambayo.
“Rais Samia amenituma, Mwenezi ukienda huko ukague na hiyo barabara ya kilometa 210, kilometa 50 zipo tayari angalia kama ujenzi unaendelea nimethibitisha nimempita mkandarasi maandalizi yanafanyika vipande viwili kilometa 100 amepewa mkandarasi mmoja, kilometa 60 kapewa mwingine zote 210 mpaka Masasi zinajengwa,” amesema Makalla.
Ameongeza kuwa ili bandari iweze kufanya kazi vizuri na kuleta tija ni baada ya kukamilika kwa barabara hiyo ambayo kusaidia kuimarika kwa uchumi katika mikoa yote ya kusini ambayo ni Lindi, Mtwara na Ruvuma itakuwa imefunguka vizuri.
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
14-03-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
14-03-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
14-03-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
14-03-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
14-03-2026
πππ¦πππ‘ππ’ πππ πππ§. π ππππ₯π’ ππππ£π’πππππͺπ ππͺπ π¦πππ‘ππͺπ πππ₯ ππ¦ π¦πππππ
14-03-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
14-03-2026
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
14-03-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
14-03-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
14-03-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
14-03-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
14-03-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
14-03-2026
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
14-03-2026
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
14-03-2026
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
14-03-2026
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
14-03-2026
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
14-03-2026
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
14-03-2026
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
14-03-2026