WASIRA- VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VIENDESHWE KWA KUZINGATIA MAHITAJI
MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira, amesema vyama ya ukombozi kusini mwa Afrika viendeshwe Kwa kuzingatia mahitaji ya wakati huu bila kusahahu shabaha ya kuanzishwa kwake.
Amesema kuwa vyama hivyo vilipigania uhuru kuzikomboa jamii za waafrika ambayo ndani yake ina vizazi vilivyopo na vinavyokuja.
Wasira alieeleza hayo leo alipokuwa akifungua semina kwa viongozi vijana kutoka vyama vya ukombozi Kusini mwa Afrika iliyofanyika katika Shule ya Uongozi ya Julius Kambarage Nyerere, Kibaha mkoani Pwani.
Vyama hivyo ni FRELIMO (Msumbuji), MPLA (Angola), ANC (Afrika Kusini), SWAPO (Namibia), ZANU-PF (Zimbabwe) na CCM ya Tanznaia ambapo katika mapambano ya ukombozi vilishirikiana kwa karibu na Chama cha Kikomist cha China (CPC).
Alisema lengo la semina hiyo ni kuimarisha vyama hivyo ambapo anaamini mifumo ya siasa inabadilika kutoka chama kimoja kwenda vyama vingi na lazima kutafuta mbinu ambayo itavifanya vyama hivyo kujiimarisha kutoka chini, visiwe vyama vya watu wachache hatua ambayo inalenga kuhakikisha vinaendelea kuongoza nchi zao.
“Mbinu za kuongoza nchi zao ni kuhakikisha mabadiliko yoyote ya dunia hayayumbishwi lakini pamoja na kwamba ni lazima washirikiane na dunia nyingine wasifanye dunia ikawa badala ya shabaha yao, maana duniani hapa kuna mambo yake vilevile.
“Vyama hivi shabaha yake ni ya muda mrefu ambayo ni kuona dunia ina maisha bora kwa watu wake ambao wanazaliwa kila siku, hata kama kuna mabadiliko mengi yanatokea shabaha inabaki ile ile kuona watu wetu katika nchi hizi wanapata maisha mazuri na hii ndio shabaha ya msingi na haina mwisho, huwezi kusema maisha sasa yametosha,” alisema.
Akizungumzia nafasi ya vijana, alisema ndio warithi halali wa vyama hivyo, hata yeye alikuwa kijana na hiyo inamaanisha kuwa hakuna kuendelea bila kijana.
Kwa mujibu wa Wasira, urithi wa vijana ni muhimu kwa maendeleo ya vyama hivyo na kwamba kama haikufanyika hivyo vitakuwa vyama vya wazee ambao wakiondoka na vyama vinaondoka “ni lazima kurithisha vijana ili wachukue nafasi yao katika kuongoza vyama hivyo.”
“Sio kila kijana anaweza kurithi, wanatakiwa vijana wanaojua historia, wanaojua sababu ya hivi vyama kwa nini wazee wao walipigana hadi wakafa, wakijua hivyo wataendeleza shabaha iliyowaua wale.
“Tumeanza tunachukua chipukizi na UVCCM kuwapeleka Ihemi, Iringa kuwafundisha, hapa katikati tulikuwa tumeacha hiyo program lakini sasa tumejua bila mafunzo tutapata tabu kurithisha uongozi unaoeleweka, tunawafundisha itikadi ya vyama hivi na shabaha yake,” alisema.
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
07-01-2026
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
07-01-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
07-01-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
07-01-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
07-01-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
07-01-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
07-01-2026
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
07-01-2026
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
07-01-2026
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
07-01-2026
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
07-01-2026
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
07-01-2026
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
07-01-2026
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
07-01-2026
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
07-01-2026
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
07-01-2026
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
07-01-2026
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
07-01-2026
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
07-01-2026
TAARIFA KWA UMMA
07-01-2026