WASIRA- VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VIENDESHWE KWA KUZINGATIA MAHITAJI
MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira, amesema vyama ya ukombozi kusini mwa Afrika viendeshwe Kwa kuzingatia mahitaji ya wakati huu bila kusahahu shabaha ya kuanzishwa kwake.
Amesema kuwa vyama hivyo vilipigania uhuru kuzikomboa jamii za waafrika ambayo ndani yake ina vizazi vilivyopo na vinavyokuja.
Wasira alieeleza hayo leo alipokuwa akifungua semina kwa viongozi vijana kutoka vyama vya ukombozi Kusini mwa Afrika iliyofanyika katika Shule ya Uongozi ya Julius Kambarage Nyerere, Kibaha mkoani Pwani.
Vyama hivyo ni FRELIMO (Msumbuji), MPLA (Angola), ANC (Afrika Kusini), SWAPO (Namibia), ZANU-PF (Zimbabwe) na CCM ya Tanznaia ambapo katika mapambano ya ukombozi vilishirikiana kwa karibu na Chama cha Kikomist cha China (CPC).
Alisema lengo la semina hiyo ni kuimarisha vyama hivyo ambapo anaamini mifumo ya siasa inabadilika kutoka chama kimoja kwenda vyama vingi na lazima kutafuta mbinu ambayo itavifanya vyama hivyo kujiimarisha kutoka chini, visiwe vyama vya watu wachache hatua ambayo inalenga kuhakikisha vinaendelea kuongoza nchi zao.
“Mbinu za kuongoza nchi zao ni kuhakikisha mabadiliko yoyote ya dunia hayayumbishwi lakini pamoja na kwamba ni lazima washirikiane na dunia nyingine wasifanye dunia ikawa badala ya shabaha yao, maana duniani hapa kuna mambo yake vilevile.
“Vyama hivi shabaha yake ni ya muda mrefu ambayo ni kuona dunia ina maisha bora kwa watu wake ambao wanazaliwa kila siku, hata kama kuna mabadiliko mengi yanatokea shabaha inabaki ile ile kuona watu wetu katika nchi hizi wanapata maisha mazuri na hii ndio shabaha ya msingi na haina mwisho, huwezi kusema maisha sasa yametosha,” alisema.
Akizungumzia nafasi ya vijana, alisema ndio warithi halali wa vyama hivyo, hata yeye alikuwa kijana na hiyo inamaanisha kuwa hakuna kuendelea bila kijana.
Kwa mujibu wa Wasira, urithi wa vijana ni muhimu kwa maendeleo ya vyama hivyo na kwamba kama haikufanyika hivyo vitakuwa vyama vya wazee ambao wakiondoka na vyama vinaondoka “ni lazima kurithisha vijana ili wachukue nafasi yao katika kuongoza vyama hivyo.”
“Sio kila kijana anaweza kurithi, wanatakiwa vijana wanaojua historia, wanaojua sababu ya hivi vyama kwa nini wazee wao walipigana hadi wakafa, wakijua hivyo wataendeleza shabaha iliyowaua wale.
“Tumeanza tunachukua chipukizi na UVCCM kuwapeleka Ihemi, Iringa kuwafundisha, hapa katikati tulikuwa tumeacha hiyo program lakini sasa tumejua bila mafunzo tutapata tabu kurithisha uongozi unaoeleweka, tunawafundisha itikadi ya vyama hivi na shabaha yake,” alisema.
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
06-11-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
06-11-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
06-11-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
06-11-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
06-11-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
06-11-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
06-11-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
06-11-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
06-11-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
06-11-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
06-11-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
06-11-2025
TAARIFA KWA UMMA
06-11-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
06-11-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
06-11-2025
MONGELLA AONGOZA MAZISHI YA KADA WA CCM JIJINI MWANZA
06-11-2025
ASIYETII SHERIA, KATIBA NA KUWA TAYARI KUUA KWA MASLAHI BINAFSI HUO NI UGAIDI’
06-11-2025
πππ π¬ππ¦ππ¦ππ§πππ πͺπππ’π πππ ππ¨πππππππͺπ ππͺπ ππ¨πππ‘πππ§ππ π¨πͺπππ’, π¨πππππ‘ππ’ π‘π π¨πππππππ¨, π¬ππππ ππ π πππ¨π‘ππ - πππ. πππ©π¨
06-11-2025
KAENI KIMYA KAMA HAMJUI NCHI ILIKOTOKA - WASIRA
06-11-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amefungua kiwanda cha kutengeneza mabomba ya maji na uchakataji pamba cha MOLI Oil Mills Co. Ltd kilichopo Bariadi Mkoani Simiyu tarehe 16 Juni, 2025.
06-11-2025