CCM NDIYO YENYE MKATABA NA WANANCHI KATIKA KUISIMAMIA SERIKALI - BALOZI DKT. NCHIMBI
> Awataka viongozi wa serikali kutambua kuwa CCM ndiyo yenye dhamana ya kuisimamia na kuiendesha serikali
> Atoa pongezi kwa ushirikiano mzuri wa chama na serikali mkoani Mbeya
> Awashukuru na kuwapongeza wananchi wa jimbo la Mbeya mjini kwa kuendelea kuwa na imani na Dkt. Tulia Ackson kwakuwa ameliheshimisha Taifa
Katibu Mkuu wa Chama Chama Mapinduzi (CCM) Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi , amesema chama chochote cha siasa kinapokwenda kwenye uchaguzi ni lazima kipeleke ilani yake kwa wananchi na wananchi wakiikubali na kukichagua maana yake wanakipa dhamana na unakuwa mkataba wa kuiendesha na kuisimamia serikali kuhakikisha ilani ile inatekelezwa.
Balozi Dkt. Nchimbi amesema bahati mbaya kuna wakati mwingine unakuta baadhi ya maeneo kuna viongozi wa serikali wanashindwa kutambua kwamba CCM ndiyo yenye mkataba na wananchi wa kuiendesha serikali hivyo amewataka viongozi kutambua hilo na kuwa ni wana wajibu wa kuitekeleza ilani ya CCM kwa kishindo na kwa wakati.
Kulingana na hilo, Balozi Dkt. Nchimbi ametoa pongezi kwa Uongozi wa CCM na Serikali katika Mkoa wa Mbeya kwakuwa na ushirikiano mzuri hali iliyopelekea kutekelezwa kwa miradi mingi ya maendeleo pamoja na kuwahudumia wananchi ipasavyo.
" Tunapokwenda kwenye uchaguzi, chama chochote cha saisa kinakuwa kinapeleka ilani yake na ndivyo CCM tulivyofanya na wananchi wakatuchagua maana yake CCM ndiyo yenye mkataba wa kuisimamia na kuiendesha serikali...bahati mbaya wakati mwingine unakuta kuna maeneo viongozi wa serikali wanashindwa kutambua kwamba CCM ina mkatana na wananchi wa kuiendesha serikali, hapa Mbeya hongereni sana kwa kutambua hilo kwakuwa mmekuwa na ushirikiano mzuri kati ya Viongozi wa Chama na Serikali "
Pia, Balozi Dkt. Nchimbi ametoa pongezi kwa viongozi wa CCM mkoa wa Mbeya kwa usimamizi madhubuti wa utekelezaji wa ilani kwakuwa maeneo mengi yamevuka hadi asilimia 100%.
Aidha, Balozi Dkt. Nchimbi ametoa zawadi ya Tsh Milioni 2 kwa vijana wa hamasa mkoa wa mbeya kwa kufanya kazi kubwa ya kuendelea kuhamasisha watanzania kukiamini na kukipenda chama cha mapinduzi lakini kwa kuwa na maneno ya vionjo yaliyobeba jumbe zenye kueleza utekelezaji wa ilani.
ποΈ17 Aprili, 2024
πJijini Mbeya
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
05-01-2026
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
05-01-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
05-01-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
05-01-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
05-01-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
05-01-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
05-01-2026
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
05-01-2026
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
05-01-2026
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
05-01-2026
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
05-01-2026
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
05-01-2026
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
05-01-2026
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
05-01-2026
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
05-01-2026
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
05-01-2026
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
05-01-2026
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
05-01-2026
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
05-01-2026
TAARIFA KWA UMMA
05-01-2026