Makamu wa Pili wa Zanzibar Alhajj Hemed Suleiman Abdulla amewaasa wanafunzi wa kidato cha sita kuzidisha jitihada katika masomo ili kuweza kupata viongozi bora na weledi wa baadae watakaoliletea heshima Taifa letu
Ameyasema hayo kwakati akikabidhi futari kwa wanafunzi wanaoishi dahalia mbali mbali kisiwani Pemba kwa lengo la kuwarahisishia upatikanaji wa ftari katika kipindi hichi cha mwezi mtukufu wa ramadhani.
Amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inayoongozwa na Rais Dkt Hussen Mwinyi imeamua kuftari na wanafunzi wanaoishi katika madahalia kwa njia ya kuwapeleka futari kwenye maskuli yao jambo ambalo litawasaidia kukidhi mahitaji yao hasa katika mwezi mtukufu wa ramadhani.
Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar amesema kuwa mkakati wa Serikali ya Awamu ya Nane(8) ni kuhakikisha wanafunzi wanaoishi katika madahalia na sehemu nyengine wanasoma kwa utulivu ili Taifa liweze kupata wataalamu bora na viongozi wazuri wa baadae.
Mhe. Hemed amesema Serikali itaendelea kulipa kipao mbele suala la elimu kwa kuimarisha miundombinu ya elimu sambamba na kuboresha mikopo ya elimu ya juu kwa wanafunzi wanaojiunga na vyuo vikuu kwa lengo la kuhakikisha Zanzibar inapata matokeo mazuri pamoja na kuzalisha wataalamu wenye uweledi katika kada mbali mbali.
Sambamba na hayo Mhe. Hemed amesema Serikali inaangalia uwezekano wa kujenga dahali ya kisasa katika skuli ya Madungu Sekondari pamoja na kuijenga ya ghorofa skuli ya Sekondari ya Shamiaani ili kupunguza changamoto ya uhaba wa madarasa sambamba na kuweka mazingira bora ya kusomea na kujifundishia kwa wanafunzi skulini hapo.
Kwa upande wake Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe. LELA MOHAMMED MUSSA amesema kuwa Serikali itaendelea kutoa misaada ya aina mbali mbali kwa wanafunzi kwa lengo la kuwaondolea changamoto wanazokumbana nazo wakiwa maskulini hasa wanafuzi waoishi katika madahalia.
Waziri LELA amemshukuru Makamu wa Pili wa Rais kwa msaada alioutoa kwa wanafunzi hao na kuahidi kuwa utatumika kama ulivyokusudiwa na kuwataka wanafunzi waliopatiwa msaada huo kuongeza bidii katika masomo yao na kupata matokeo mazuri katika mitihani yao ili Taifa liweze kupata wataalamu wazalendo watakaolipigania Tifa lao.
Akitoa shukrani kwaniaba ya wanafunzi wenzake mwanafunzi wa Kidato cha Tano (5) Skuli ya Sekondari ya Fidel Castro OMAR MOHAMMED SHAALI ameishukuru Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kuwawekea miundombinu mizuri ya kujifunzia sambamba na kuwapatia msaada huo jambo ambalo linapelekea kuondosha changamoto zinazowakabili wakiwa mashuleni hasa kwa wanafunzi wanaoishidahalia.
Aidha mwanafuzi OMAR amemuahidi Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar kuwa watahakikisha wanasoma kwa bidii na maarifa ili waweze kufaulu vizuri katika masomo yao na kutimiza malengo waliojiwekea. .
Miongoni mwa skuli zilizopatiwa ftari hio ni pamoja na Skuli ya madungu sekondari,Fidel Castro, Chuo Cha Kiislamu Kiuyu, Dkt. Amani Micheweni, Idrisa Abdulwakili Kizimbani, Utaani, Wete Sekondari pamoja na kituo cha kulelea yatima Micheweni Pemba.
Wakati huo huo Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar amekabidhi futari kwa wafanyakazi wa Kitengo cha Uratibu wa shuhuli za Chama cha Mapinduzi, Viongozi na watendaji wa Chama hicho katika Mikoa miwili ya kichama.
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
06-01-2026
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
06-01-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
06-01-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
06-01-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
06-01-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
06-01-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
06-01-2026
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
06-01-2026
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
06-01-2026
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
06-01-2026
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
06-01-2026
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
06-01-2026
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
06-01-2026
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
06-01-2026
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
06-01-2026
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
06-01-2026
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
06-01-2026
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
06-01-2026
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
06-01-2026
TAARIFA KWA UMMA
06-01-2026