ALICHOSEMA KATIBU MKUU WA CCM SAKATA LA CHADEMA KUSHIKILIWA POLISI
“Nimesikia kule Mbeya kulikuwa na tafrani kidogo kati ya Chadema na Polisi, na sisi kwa staili ya Rais wetu Samia Suluhu Hassan, anapenda sana mambo yawe yanamalizwa kwa kuzungumzwa, badala ya kukimbizana kimbizana kila mahali.
“Kwa hiyo nilifanya jitihada za kuwatafuta viongozi wenzangu wa vyama vingine ili nizungumze nao makatibu wenzangu, lakini nikaambiwa yule mmoja wa Chadema ni katika waliokamatwa.
“Sasa nikasema kwa kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani uko hapa, mambo ya sheria, siyo ya kutolea maelekezo Kiongozi wa Chama cha siasa, au siyo? Lakini nitumie nafasi hii, mwambie Waziri wako, kwamba tunaomba, muone uwezekano wale viongozi wa vyama vya siasa waachiliwe.
“Ili mtupate nafasi ya kuzungumza nao. Waachiliwe tupate nafasi ya kuzungumza nao, kwa sababu tunajenga taifa moja. Tunapenda kuwa na taifa tulivu.
“Kama kuna mahali wamekosea wao au tumekosea sisi, tukae tuzungumze. Tuijenge nchi yetu. Kwa hiyo huu ni ujumbe, mwambie Waziri wako kwamba Chama Cha Mapinduzi kinaamini kwamba kuzungumza ni jambo zuri zaidi.
“Kabla vyombo vya sheria havijafanya mambo ya sheria basi mtupe nafasi kidogo sisi wanasiasa kwanza tuzumgumze," Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, Katibu Mkuu wa CCM.
Balozi Nchimbi amezungumza hayo leo Agosti 12, 2024, kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Uwanja wa CCM Katoro, mkoani Geita akiwa kwenye mwendelezo wa ziara yake ya siku 3, mkoani humo, aliyoanza Agosti 11, 2024.
Katibu Mkuu wa CCM huyo, katika ziara yake hiyo aliyoanzia Mkoa wa Kigoma, kisha Kagera na sasa yuko mkoani Geita, ameambatana na Wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Ndugu Issa Haji Usi Gavu, Katibu wa NEC - Oganaizesheni, Ndugu Amos Gabriel Makalla, Katibu wa NEC - Itikadi, Uenezi na Mafunzo na Ndugu Rabia Hamid Abdalla, Katibu wa NEC - Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, ambapo kesho anatarajiwa kuzungumza na wananchi Mjini Geita, kwenye mkutano mkubwa wa hadhara utakaofanyika katika Uwanja wa Nyankumbu.
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
11-03-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
11-03-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
11-03-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
11-03-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
11-03-2026
πππ¦πππ‘ππ’ πππ πππ§. π ππππ₯π’ ππππ£π’πππππͺπ ππͺπ π¦πππ‘ππͺπ πππ₯ ππ¦ π¦πππππ
11-03-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
11-03-2026
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
11-03-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
11-03-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
11-03-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
11-03-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
11-03-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
11-03-2026
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
11-03-2026
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
11-03-2026
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
11-03-2026
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
11-03-2026
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
11-03-2026
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
11-03-2026
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
11-03-2026